KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Nne (4)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
“Halo.kutoka hapa hadi Care lodge ni kiasi gani cha pesa?”

“Dola tano.Karibu”

“Sikuweza kubishana sana kwani niliamini kauli ya ‘nipunguzie bwana’ ni huku kwetu.Alinifungulia mlango wa mbele, nilivuta mguu wangu wa kulia na kuingia ndani mlango wa mbele kulia mwa dereva.Gari hilo lilikuwa ‘Left hand’.Nilienda moja kwa moja kwenye hoteli iliyoitwa CARE LODRGE .Dereva alitumia kama dakika nne kuingia lango la hoteli hiyo.Nilipofika, nilimlipa ujira wake, nikaelekea ofisi za kupokelea wageni(Mapokezi). Sikutaka kwenda kufanya biashara kwa wakati huo. Niliamua kujipumzisha kutokana na uchovu wa safari, jambo la kushangaza nilichokiona mbele ya macho yangu sikuweza kuamini macho yangu kama yalikuwa sawa sawa ama vipi, nilijaribu kupikicha macho pengine ni ule ukungu wa kutokuwahi kupenda. Lakini cha ajabu moyo wangu ulisimama kama sekunde kadhaa, kisha ukaendelea mapigo yake yakawa ya taratibu mno, ambayo sikuweza hata kuyasikia. Nilihisi jasho jepesi likitiririka, kwanza nilijitazama kisha nikamtazama mtu huyo, hata hivyo sikuamini kwamba kwa uzuri wake kamwe ningependwa mtu mweusi tena Mtanzania?.

Niliona mwanadada mmoja aliyekuwa amekaa karibu na muhudumu wa mapokezi katika hoteli hiyo, msichana huyo alikuwa Mzungu si mzungu, muhindi si muhindi, mwarabu si mwarabu hata kwenye weusi hakuwepo. Baada ya dakika tano, nikiwa nimemtumbulia jicho la matamanio, alinisalimia .

“Kaka habari yako”

“Nzuri, sijui nyie”nilijibu salamu kwa wote,nikiwa bado sijabandua jicho usoni mwake.Sikushughulika na huyu mwingine,macho yangu tayari yalishapata chakula.Nilimtizama hamu haikuniisha nikatabani abaki pale pale macho yangu ya shibe.

“Mimi mzima”aliitikia msichana huyo na aliyefuata ni wamapokezi.

“Hata mimi mzima pia” walinisalimia.

Sikupenda kukaa na ule mzigo wenye thamani kubwa niliandikisha jina langu na kuchukua chumba namba kumi.Kila nilipotaka kuondoka kuelekea chumba nilicholipia ,nilisita na kubakia mdomo wazi,mwili ulibweteka nikitamani kufahamiana zaidi na mwanadada yule.Niliamua kujilazimiza kuondoka ingawa nafisi ilitukutika,nilipofungua mlango wangu,niligeuka kumtizama yule mlimbwendekama vile nikihakikisha kama atakuwa pale.Nilimuona nae akinitizama.

“Mtoto mtoto,Duu!.Tembea uone mengi”Niliongea akilini nikiwa nafungua mlango,katika kuzungusha funguo mlango ukatii sheria ,ukanipa nafasi ya kuingia.Nilihifadhi Breefcase yangu haraka na kufungua mlango kutoka nje.Nilikuwa nimeshikilia funguo,nikajikuta nikiziachia bila kujijua.Yote ni baada ya kumwona yule binti akiwa ametoka chumba kilichokuwa mkabala na changu.

“Kumbe chumba nilichochukua kilikuwa karibu na chumba cha Binti yule niliyesalimiana nae muda mfupi tangu nifike pale.”Nilijisemea moyoni kiwa nimeacha mdomo wazi ,nikimtizama ,alikuwa kajifunga taulo nyepesi kabisa.Tayari kwa sasa alikuwa kanipa mgongo,kila alipovuta hatua , makalio yake yalitikisikia kama mawimbi ya maji baharini.Miguu yake minene iliyobeba umbile la wastani lilijivuta kwa madaha.Nilijikuta nikimtizama hadi alipoishia.

Kwa kweli nilimpenda na niliamini angenifaa kuwa mwezi wangu na pambo la ndani. Hata hivyo niliumia moyoni je kama akinikubali nitafanya nini kama baba na mama watakuwa wamenipatia mchumba wa kumuoa?.Wazo hilo lilinijia na nikaamua kulitupilia mbali. Lakini ngoja nisiumize kichwa sijui nitakubaliwa au laa! Kwani nitese nafsi yangu? Nilizidi kuwaza wakati namalizia kufunga chumba. Pasipo kutegemea mara nambona tena akiwa kashikilia mafuta ya lotion. Safari hii alikuwa anakuja kwa mbele,niliweza kufaidi kuisawiri sura yake vema, ilioonyesha umahiri wa muumba.Tembe yake ungeweza kudhania kachoka vile,lakini hapana ukweli halisi.Ule ndio mwendo wake halisi,ikafikia hatua nikadhani hakanyagi chini, kwa jinsi alivyotembea utafikiri anaionea aridhi huruma. Nikajikuta moyo ukinipasuka “paaa” nikiwa na mshangaa nae alinitolea tabasamu nono! lililoshamiri usoni mwake.Tena likiwa limeambatana na mwanya mzuri.Nilishikwa na butwaa kama dakika kadhaa, nikajikuta ubongo ukifa ganzi. Tulibaki macho pima, hapo nilijua dhahiri kama kunapimana hivi.Nikajitizama na kumtizama kwa mara ya pili. Mapigo y a moyo yakaanza kupungua.Hata hivyo nilishindwa kuvumilia yote niliyoyaona kwa safari hii.

“Samahani dada naweza kujua jina lako”alikuwa kesha nikaribia.

“Yaa!. Jina langu ni Jeniffer John”

“Sawa . Ahsante unajina zuri. Naitwa Sweedy Kachenje” nilijitambulisha nikilamba midomo yangu kuua aibu flani iliyochomoza kama mshale wa sekunde na kupotea.

Tuliongea mengi na Jeniffer nae hakuwa mvivu wa kujibu maswali na chochote nilichomuelezea, niliamini ndoto yangu ilitimia, yule mwanamke niliyempata angeweza kufunika pengo kubwa maishani mwangu. Hata hivyo katika mazungumzo yetu alinitamkia kwa kinywa chake kuwa nae ananipenda sana, kuliko hata mimi ninavyompenda. Ni binti aliyeukonga moyo wangu na kuuteka kila sehemu ya viungo vya mwili wangu, “Kweli subira huvuta heri” niliongea kimya kimya kwenye mtiririko wa mawazo.

INAENDELEEEA
Powered by Blogger.