KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi na nne (14)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Zikawa zimepita Siku mbili toka nilipookolewa na Mke wangu,Getruda pale nilipokuwa najiua kifo cha taabu.

“Mume wangu nilikuwa nikikutania . Tafadhali usijaribu kujiua tena. Nimekubali mlete huyo rafiki yako leo nimuone kama sura yake ina tapisha au laa!” Getruda hakupenda kufanya hivyo aliamua kukubali ili kuninusuru kifo. Sauti ya Getruda ilipenyeza kwenye ngoma ya masikio yangu fundo kali la sononeko liliingia moyoni.Nikajivuia kulia kwa nguvu zote lakini nilijikuta machozi yakichuruzika taratibu bila kujua.

“Sawa mke wangu utamuona nitakapomleta jioni,” Ilikuwa asubuhi na mapema, majira ya saa moja na nusu.

“Mmmm! Lakini Getruda unanipenda.Isingekuwa wewe basi nilikuwa mfu”Nilimweleza Getruda.

“Kumbe unalijua.Mkojo ulishaanza kukutoka”

“Masihara hayo.Inamaana nilikikojolea kama mtoto”

“Ndio”Getruda alinijibu akainuka kitini na kuelekea kwenye jokofu ambako alilifungua na kunipatia Juisi baridi ya machungwa.

“Karibu mpenzi”

“Ahsante mpenzi”Niliipokea na kumtolea tabasamu,lakini nilipokumbukla kwamaba nahitajika kumtambulisha bosi wangu.Moyo ulisingaa na kunyauka kama jani la tumbaku lililosubiri kusagwa.

“Mpenzi nataka kwenda kujipumzisha kidogo”

“Sawa,ila usisahau kwenda kumleta rafiki yako jioni”Nilishituka na kutulia kama sekunde kadhaa ,kisha nikageuka kumtizama mke wangu.

“Utaniamsha baada ya saa moja.

Ok, bye”Nilijikaza kutoa tabasamu ambalo pengine lilionekana dhahiri la kulazimisha, huku moyo ukiniuma kama kutu inavyokula chuma taratibu na kukiozesha chote.

“Nije tujipumzishe wote?”Getruda alinieleza wakati nikiwa nimempa mgongo.

“Poa. Ukipenda”Nilimjibu damu zikienda mbio ,ungeweza kuhisi nimekimbia umbali mrefu bila kupumzika.

Getruda alinifuata chumbani kama alivyoomba.Nilijitupa kitandani kiuvivu uvivu nae akajibweteka kwenye sofa moja lililomo chumbani.Ingawa nilifumba macho lakini sikuwa hata na lepe la usingizi, mawazo yangu yalimezwa na taswira ya maisha ya unyumba.Nilijiuliza bila kupata jawabu sahihi kwamba ugonjwa huwa niliupata wapi na nani aliyenipa?.

Nikiwa nimelala nilihisi vidole laini zikitalii mwilini mwangu.Hata hivyo sikushituka kwani nilihiosi alikuwa mke wangu.Vidole hivi vilizunguka huku na kule bila kupumua,nilihisi kama kero ama mdudu fulani akinitembelea akini kwarua. Sikuona raha zaidi za mateso tu.

“Hallo Sweedy”

“Na..a.amu”Nilikokoteza maneno,nikiwa nimetulia utadhani mbwa anayetolewa kupe.

“Unanipenda?”

“Saaana tu”

“Kwanini hunipi haki yangu kama kweli unanipenda?”

“Haki ipi?.Si una jua matatizo yangu sasa unataka nini tena”

Nilihisi Getruda akinitibua akili yangu.Niliinukla na kutoka nje.

“Getruda unanitesa. Tumepanga nini na wewe unataka nini?”

Nilitulia kidogo nikaendelea, “Moyo wangu unasononeka sana. Laiti ningelijua nisingeoa, maisha gani haya yananitesa kiasi hiki?”Nilijikuta nikilia ovyo kama toto jinga lenye kudeka ovyo.Kilio changu lilikuwa rohoni.na aliyejua alikuwa muumba pekee.Getruda alikuja kunibembeleza kwa hofu kwamba ningechukua maamuzi ya kijinga tena. Aliniandalia chakula mezani.Tulisali kisha tukala .

Saa nane mchana baada ya kupata mlo wa mchana nilimuaga Getruda nikiwa naelekea ofisini kumueleza Mzee Jophu yaliyosibu katika unyumba wangu. Lakini cha kushangaza Mzee Jophu baada ya kumueleza kila kitu,nilimuona uso ukiwa umejawa furaha badala ya kunionea huruma. Hali hiyo aliisubiri kwa hamu hata hivyo alishanga kuona mimi kuchelewa kumuelezea shida zangu toka mwanzoni.Alijifanya kama hataki kuchangia mapenzi ilinimuone mtu mwema,

“Sasa Jophu unakataa nini na wakati nimekuambia mke wangu hajaguswa”



“Inamaana siku zote hizo mlikuwa mkilala tu?”

“Ndio”nilimjibu nikahisi machozi yakinilengalenga, hata hivyo nilijikaza kiume.

“Matatizo haya yalikupata muda gani?”

“Siku ya kwanza toka nifunge ndoa na mke wangu”

“Usinitanie Sweedy. Ulijaribu kwenda hospitali?”

“Ndio.Nilichunguzwa kwa makini.Daktari alinieleza kwamba nilipigwa sindano yenye sumu.Nilikataa kwani sijawahi kupigwa sindando yeyote toka uliponiajiri. Na sasa ni miaka karibu ishirini na tano. Nakumbuka sindano ya mwisho nilichomwa nikiwa na chuoni. Na siku nyingine niile nilipokuja kutolewa damu”

“Kutolewa damu si kupigwa sindano labda una matatizo mengine kiafya.Vipi kuhusu chango?”

“Sina chango,mzee”Nilimjibu nikiwa nimetizama chini.

“Mzee, naomba unisaidie kuokoa jahazi la ndoa yangu”Nilimweleza nikimpigia magoti.Sikuwa najua kwamba mzee Jophu ndiye aliyetuma watu wanipige sindano ya kuua uume wangu.Wakidai wana nitoa damu ilinikapimwe virusi vya ukimwi.Hata hivyo ilikuwa kazi kumgundua mbaya wangu,jinsi alivyoonyesha kutokutaka kuchukua jukumu la kumridhisha mke wangu.

“Mkeo atakubali kwenda kupima damu zetu?”

“Sina uhakika kama atakubali au laa. Ni vizuri kimpigie simu”Nilitoa simu yangu ya kiganjani na kubonyeza namba za Getruda, mke wangu.

“Hallo, mpenzi”alipokea tu baada ya kuona namba zangu juu ya kioo cha simu yake.

“Oooo!, vipi upo salama.”

“Ndio. Sijui wewe”

“Shwari kabisa.Mmmm…utakubali kupima Virusi vya ukimwi?”

“Tangu lini kigori akawa na Ukimwi?”

“Sijambo la ajabu kwani ukimwi unaambukizwa kwa kujamiana tu?”Getruda aitafakari akajiona kweli alibugi sana.

“Sawa, nimekubali kupima afya kwa manufaa yetu sote”

“Ok, jiandae nakuja sasa hivi nyumbani”

“Ok, bye bye”Alinaga na kukatasimu.

“Nilimtizama mzee Jophu na kumwambia, “Amekubali kupima”

Kwambali niliona tabasamu la mzee Jophu lililonifanya nione meno yake ya rangi rangi, nafikiri kutokana kunywa maji ya Arusha tokea utotoni mwake.

“Sasa Sweedy”Alitulia kidogo na kukohoa kinafiki,nilimtizama kwa makini niwezekujua alichotaka kusema,aliendelea “Kwa vile wewe ni rafiki yangu sina budi kukusaidia.Ila nakuomba usimweleze mtu yeyote ‘Especial my wife’,Umenielewa. Narudia tena naomba iwe siri moyoni mwetu”

“Sawa, mzee.Usihofu kitu”nilimjibu kwa upole kabisa.

Mzee Jophu aliongea moyoni akiwa amejawa furaha kubwa mno, “Kile nilichokitaka kimekamilika. Sasa kazi kwangu kurina asali nitakavyo””

Mzee Jophu kunajambo la muhimu nimelikumbuka. Nilimdanganya kuwa nilimwagikiwa na tindikali. Akikuuleza mueleze ni kweli”Nilitulia kidogo, ingawa alijaribu kuficha furaha niliiona , Nikatulia kama niliyewaza kitu ,Machozi yakaniwakia pale nilipokumbuka nguvu zangu nilipokuwa Nchini Thailand “Lakini boss na shindwa kujua ugonjwa huu niliupata wapi na nani aliyeniletea”

“Usijali muombe mungu akuondolee. Hatamimi ninafanya tu, kwa vile wewe rafiki yangu wa damdam, lakini kwa maulana ni dhambi kuzini nje ya ndoa,” Mzee Jophu aliongea ilinimuone mtu wa busara kama alivyoonekana kuwa ni mtu wa busara kumbe ni muungwana wa ngozi tu, lakini rohoni ni muuwaji. Maneno yake ilikuwa vigumu kumgundua kuwa yeye ndiye mbaya wangu, aliyeamua kunitesa iliamfanye mke wangu wake.

Mazungumzo yetu ya ofisi yalikuwa ya muda mrefu. Tulipo maliza jioni iliwadia tuliongozana na Mzee Jophu moja kwa moja hadi nyumbani kwangu.

“Lakini Sweedy kama ameoa mke mwenye uso wa mbuzi mimi sitamkubali atakuwa wako mwenyewe”

“ Hakika mke wangu utamkubali. Amekamilika kila idara. Utamsahau mama Jacob nakuambia” Nilimueleza.

“Yote tisa, kumi tutaona. Nitaamini unajua kuchagua,”

“Lako jicho, yanini ni kusifie?” Niliposema, nilitamani Mzee Jophu ardhike na ombo la Getruda, lakini kitu kilichoniuma zaidi ni jinsi gani ningemuunganisha mwanaume mwenzangu na mke wangu niliyemlipia mahari.

INAENDELEA
Powered by Blogger.