KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi na tano (15)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
“Inawezekana huyu mshenzi akamkataa mke wangu. Midomo yake imejaa dharau”nilijisemea kimoyomoyo huku nikibonyeza kitufe cha geti.

Getruda Kimario alifika getini na kufungua, mtu wa kwanza kuingia akiwa Mzee Jophu.Shauku yake haikufichika ,alimtupia Getruda jicho la lilo jaa ubembe.Ni hapo ndipo nilipohisi Mzee Jophu kumkubali mke wangu. Alikuwa na shauku ya kumbusu Getruda, nikipindi kirefu toka wapoteane pale ofisini kwake, na Getruda alimkumbuka kuwa yule alikuwa yule aliyempa mama yake mzazi shilingi laki tano za kitanzania iliamuowe yeye. Walitupiana macho yaliyojaa furaha macho ya matamanio ya Getruda yalizidi kumchanganya Jophu. Aliyekuwa na shauku kuupitisha usiku mwanana na binti aliyemlipia shilingi laki tano. Aliamini alikuwa na haki yakujivinjari jasho lake.

Mwanzoni nilihisi hawakumbukani,kumbe kumbukumbu alikuwa nazo na alishuhudia mama yake akipokea hizo hela.

Ulifikia muda muafaka wakuweka mambo hadharani ili nitatuliwe shidayangu. Kabla sijazungumza chochote nilipandisha pumzi na kushusha kwa nguvu kama mtu aliyechoka na pilika pilika za kutwa nzima ,”ooooooophhhh!”Kisha nikasema kwa sauti ya chini kama mgonjwa,ni kweli niliyotaka kusema yaliniuma sana.

“ Nafikiri mke wangu nilisha wahi kukutajia jina la rafiki yangu kipenzi. Ila ni vema nikalirudia leo ukiwa una muona . Aliye kaa hapa mbele ndiye Mzee Jophu. Sio Mzee kweli ni kwaajili ya mali zake ndio maana watu wanampa jina la heshima ya mzee. Huyu ndiye mwa ndani wangu ukimuona yeye ndio umeniona mimi. Shida zake ni zangu, zangu ni zake,”Nilikohoa kidogo ni kumgeukia mzee Jophu. Kijasho kilizidi kuchuruzika kwa kasi kuliko mwanzoni, nilihisi midomo kufa ganzi na kuwa mizito, nilijikuta sauti ikipotea ghafla pale nilipofikiria kumuachia mzee Jophu mke wangu.Tena hajawahi kuguswa na mtu yeyeto maishani. Kwa kweli inatia uchungu sana heri ningekuwa nimezaliwa na udhaifu huo kuliko kunikuta nikiwa mtu mzima.

“Mzee Jophu huyu ni mke wangu, kwa upande mwingine naweza kusema ni mkeo. Nina matatizo ya,,,,,,” hasira kali iliniingia moyo nikashindwa kumaliza, nilijikuta nikiangua kilio. Moyo uliuma sana.

“Kweli kweli na muachia Jophu kigoli wangu?”Nilimtizama Getruda kama vile nikimuaga, sikuweza kukwepa jambo hilo tena.Kwa kuwa lilishakuwa kero katika familia yetu.

“Naomba uwe karibu na mke wangu, kama ulivyo karibu na mkeo, lakini,,,,,,,,,,naomba unifichie siri yangu, heshima iwepo msije mkachukulia muda huo kunidharau, nami sikupenda kuwa hivi,,,”Nilikokoteza maneno kwa ujasiri .

“Ok, nashukuru kumfahamu mkeo, na nitaendelea kumfahamu vizuri, zaidi kadri siku zinavyo zidi kwenda” Mzee Jophu aliongea huku akinyanyuka kuelekea alipo Getruda. Alinishika mkono na kuunyanyua usawa wa midomo yake, hakuchelewa nilisikia sauti ya busu kwenye kiganja cha mke wake wangu. Busu hilo lilimchanganya mke wangu na kujikuta mwili ukimsisimka, vinyweleo na nywele zilisimama kwa shoti ya busu la mzee Jophu.Nilibaki nimeduwa, midomo ikiwa wazi kama sekunde kadhaa.Bila hofu wala haya, walijikuta wamekumbatiana na Mzee Jophu alisogeza midomo yake karibu kabisa na sikio akimnong’oneza.

“Kweli kwenye miti hakuna wajenzi, nitakutunza kama mlima Kilimanajaro unavyotunza Seluji yake, nitakupa chochote unachotaka, ikiwezekana nitakuoa kabisa, nakupenda siko tayari kukuacha, naamini unanipenda” Sauti ya Mzee Jophu ilizidi kumtekenya Getruda, alijikuta akitikisa kichwa ishara ya kukubali.Alishindwa kujizuia kutoa sauti za kizizima, taratibu kwa jinsi maneno ya Jophu yaliyokuwa yakipenyeza sikioni angali yana uvuguvugu, kwa wimbi lenye joto nadhifu.Mzee Jophu alimwachia na kuketi karibu nae.

Mambo yote niliyaona. Kwa jinsi roho ilivyoguguna niliondoka sehemu ile na kuingi chumbani, nilimpenda sana mke wangu, sikupenda awe mke wa shirika wala sikupenda kuona akishikwa shikwa na mtu zaidi yangu. Japo nilikuwa na wivu lakini nilishindwa kwa sababu nilipata udhaifu, ikanilazimu kuvumilia na kuhamisha macho, na kutizama pembeni.Pia hilo lilinishinda nikaamua kujiondokea kiunyonge kama kifaranga asiye na mama.

Kuondoka kwangu, ulikuwa mwanya wa Jophu na mke wangu kupanga mambo yao.

“Oke nimeamini umeumbika sawa, kama asingekuwa Sweedy basi ningekuoa mimi. Bado sija chelewa. Nina nafasi kubwa ya kukuoa”Huo ndio ulikuwa mwanzo wa usaliti wa ndoa.

“Hata mimi nakiri umbo lako ni zuri na lakuvutia. Najuta kuolewa na huyu mchovu asiye na umuhimu wowote ndani ya ndoa”

Mzee Jophu alidakia “Ni kweli, sio vyote ving’aavyo dhahabu. Vingine aluminiamu ama bati,”alitulia kidogo na kumkodolea macho yaliyojaa ubembe, kisha akanyanyua mkono wa Getruda na kumbusu kiganjani, akakohoa kidogo na kusema “Sawa, tupange tukutane wapi?”Ilikuwa ni sauti ya nzito ya Jophu ikinguruma varandani kwangu.

“Mimi naona tukutane Hoteli yake Sweedy mwenyewe, pale sea breez inn hotel ili tuwaonyeshe watu na hata wafanyakazi wake kuwa Sweedy ni dhaifu”Mke wangu alianza dharau akitaka wakutane kwenye hotel yangu, ili kunidhalilisha.

“Kesho saa kumi jioni, nafikiri utakuwa muda muafaka wa kujipumzisha,”Getruda alizungumza huku akimtolea Jophu macho ya kurembua na ya unyenyekevu.

“Aaaa!, kesho mbali. Ok kumbe saa hizo karibu giza. Sawa usikose mpenzi”Walipigana mabusu ya kuagana na Mzee Jophu alimalizia .

“Niote njozi njema usiku. Tena zilizo jaa mahaba”

“Usijali mpenzi, zote nzuri zitakuwa juu yako”Mzee Jophu alitoka na mke wangu alirudi na kunifuata kule chumbani, kwa kusema kweli moyo wangu ulipata sononeko la roho, nilibaki nikiyaganga maumivu ya moyoni.

Walipanga sehemu ya kukutana bila ya kukosa, wote walikuwa na shauku moja. Ilikuwa jioni tulivu watu walikuwa wana kunywa na kula. Alionekana Mzee Jophu akiingia na mke wangu SEA BREEZ INN HOTEL. Waliongozana hadi mapokezi, na kuandika jina la kunikashfu kwenye kitabu cha wageni, bila aibu mbele ya wafanyakazi wangu. Hata kama walifanya hivyo wasingefanya kwenye hoteli yangu, wangeenda sehemu wasio julikana.Yote walionifanyia ni kunidhalilisha.

“Jina tuandike nani Mzee” muhudumu aliongea kwa wasiwasi, baada ya kumwona mke wangu, ambaye alikuwa kama bosi wake.Mzee Jophu aligeuza shingo kumtizama Getruda, Kabla hajajibu kitu mke wangu alidakia “Andika Sweedy dhaifu”

“Hapana bosi, anatakiwa kuandika jina lake kamili .Hilo sio jina kamili” aliongea kwa sauti ya chini huku akitetemeka. Alihisi mawili, kupokea tusi ama kibao.

“Sio jina kamili.Unafahamu jina lake?”

“Sifahamu”

“Kama hufahamu , mbona unasema si jina lake kamili?”Yule kijana akaanza kutizama chini kwa hofu.

“Nimekuambia uandike jina nililokutajia,upesi”

“Mama .Siwezi kuandika jina hilo”

“Wee, mpumbavu nini!.Nimekuambia andika, kama hutaki huna kazi. Fungasha virago uondoke,”Getruda alizidi kumuamrisha sambamba na kidole alichoelekeza jichoni.

INAENDELEAA
Powered by Blogger.