KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi na nane (18)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Tukiwa sebuleni nilianza kumueleza Getruda. Moyo uliniuma kila nilipo kumbuka aliyonifanyia “Mke wangu kama ingenipasa kusema, nini kinacho ikera nafsi yangu ni kuni dhalilisha ndani ya kadamnasi, sio wafanyakazi wangu wa wageni, wote wanafahamu ulilolifanya, na isitoshe ile ni hotel yangu unadiriki kufanya mapenzi ukitoa kashfa ili kuinufaisha jamii, kumbuka aibu si yangu pekee, ni yetu wote.”

Sijui ni mkate sikio au nimpe kilema kwenye via vya uzazi ni mchome na moto wa umeme (hita)asiweze kufanya tendo la ndoa maisha?.Ndio itakuwa fundisho,kiherehere kitamuisha”wakati na waza cha kumfanyia, nilikatishwa na sauti.

“Mume wangu kumbuka wewe ndio uliyenitafutia mwanaume wa kuniridhisha kimapenzi, ilinijisikie nina mume, basi kama ni hivyo nami sitaki penzi la mtu mwingine wa nje. Nataka penzi lako nilikubali kwa kukuheshimu. Mwanamke kawaida hatafutiwi mume, anatafuta mwenyewe, hisia zote nilizoweka kama nipo na wewe, iweje useme na kudhalilisha, kama utashindwa leo kesho nataka talaka yangu,asubuhi na mapema, umenielewa?”Getrudaalinisemesha kwa ukali.

“Sio nimekukataza usiwe naye, kinachonikera ni kunidhalilisha na kutoa siri ya unyumba wetu, sina wivu na mapenzi yako.Ninachotaka unihifadhie siri moyoni mwako”niliinamisha kichwa chini kama kobe.

“Mume wangu nakutunzia heshima kuliko mtu yeyote duniani, nashangaa!unapo sema nainfaisha jamii. Kama angekuwa msichana mwingine asinge vumilia hata wiki moja, na washukuru wazazi kunifundisha uvumilivu ndani ya nyumba”Aliendelea kuongea,asijue nina mawazo nini moyoni.

Tukiwa kwenye mazungumzo,nilisikia simu ikiita,nilijipapasa kama ilikuwa simu yangu.Nilipotizama pembeni nilimuona Getruda akitoa simu yake kwenye pochi ndogo ya rangi nyeusi iliyojaa nakishi nyingi.

“Hallo, uko wapi?”Getruda alipokea tu,baada ya kuona jina juu ya kioo cha simu.Niligutuka nikahisi mtu huyo anamfahamu,ndio maana alimuuliza aliko.

“Aaaa..nipo Makutano bar hapa napata moja baridi moja moto.Vipi mume bwege yupo?”

“Yupo anakusalimia”Getruda alisema na kunitupia jicho ,akacheka kidogo na kuendelea, “Utakuja kutusalimia?”Getruda aliongea akiniongoa wasi wasi.

“Ninani huyo unaongea naye?”Nilijikuta nikisema wakati Getruda anaongea na simu.

“Wivu umekuzidi mume wangu.Kila kitu unataka kujua hebu chukua basi uongee naye”Getruda aliibadilikia kwa ghafla,alinyoosha mkono wake akitakakunikabidhi simu.

“Sihitaji kuongea nae,nimekuuliza kwani vibaya?.Nilifikiri ni mama amekupigia simu”

“Hapana.Nirafiki yangu”Kisha akaendelea kuongea nae.

“Samahani kwa usumbufu uliojitokeza.Mume wangu anwivu ilembaya”

“Sasa wivu wanini wakati hayawezi?”Sauti nzito upande wa pli ilisikika ikisema.

“Hata mimi nashangaa!”Getruda alidakia na kuangua kicheko kikubwa.

“Mpenzi sikia…..naomba ufike sasa hivi hapa Makutano bar”

“Mama anaumwa sana!.Ehhe mmempeleka hospitali?”Getruda aliongea maneno hayo akiwa tayari kesha kata simu.Aliendelea kuongea simu ikiwa imekatika ilimradi anipumbaze “Ana umwa na nini hasa?” alitulia sekunde mbili hivi akaendelea, “Ooo! My god .Kuna uwezekana wa kupona?”

alitulia tena sekunde kadhaa hivi, “Sawa.Ninakuja sasa hivi huko”Akajidai kukata simu.

“Vipi mbona jasho linakutoka?.Mama anaumwa na nini?”

Nilimwuliza sekunde chache alipokata simu. “Mama alidondoka ngazi akiingia kanisani”Getruda aliongea kiupole kabisa, akionekana kujizuia kulia.

“Kanisani?”

“Ndio.Na hivi sasa yupo amepelekwa hospitali ya Kcmc kwa matibabu” Safari hii alifura na alifanya kulalamika chini chini.

“Ooo! Pole sana mke wangu.Unaonaje nikaoga tukaenda wote?”

“Utanichelewesha sana”

“Basi siogi tena. Ngoja nivae twende,tena nina siku nyingi sijaenda kumsalimu”Niliongea nikiamka kitini, tayari kwa safari.

“Hapana.Nitakuletea taarifa ya hali yake.Nyumba tutamuachia nani?”

“Hilo halina shida.Nisubiri”

“Sitaki bwana. Wee kila mahali unataka kuongozana na mimi.Nimeshachoka, ngoja niende kisha kesho nikirudi nitakuja kukuchukua kwani hata kupajua hupajui.Unapafahamu pale tulipokuwa tukiishi zamani” Nilisimama kama mlingoti ,nikavuta pumzi na kuzishusha kwa nguvu.Nikatikisa kichwa na kusema “Sawa.Kama hutaki nikapajua kwenu leo ….hata kesho nitapajua”

Niliona Getruda akitoa tabasamu kubwa ,hakuishia hapo alinifuata nakunibusu shavuni “Mwaaaa”Kisha akaokota kipima joto chake,na kutoka kwa haraka akionekana mwenye wasi wasi mkubwa.Alipofika mlangoni aligeuka na kunitizama kama akinihurumia vile,sikugundua kitu ,nilibaki nimeduwaa.Akanipungia mkono na kusema “Bye bye”Nami nikapunga kono langu zito kigoigoi bila tabasamu.

Getruda alimpigia simu mteja wetu wa kila siku katika usafi,si mwingine bali Jangala. “HalloJangala tafadhali naomba unichukue hapa nyumbani”alisema baada ya simu kupokelewa.

“Sawa.Namshusha abiria hapa mjini nakuja”

“Ok”Alijibu na kukata simu.

Kama kawaida yake Jangala huwa hakaidi na hana tamaa.Aliingia na kusimama mbele ya Getruda binti Kimario.

“Shem vipi.Wapi leo pa kula kuku.Si unaelewa wiki end”Jangala alimtania Getruda.

“Ndio. Wiki end lakini kwangu imenijia vibaya .Nimepata taarifa mama yangu mgonjwa.Naomba unifikishe karibu na Makutano bar nikampe taarifa shangazi yangu.Kisha utaendelea na safari yako.Mimi nitakupigia kama nitakuhitaji tena”Getruda alidanganya.

“Sawa.Riziki ndogo ndogo hizi usininyime shem.Pole sana kwa kuuguliwa na mama yako”

“Nishapoa shem”Alimjibu kiunyonge.Getruda hakuuguliwa wala nini.Alipokuwa akienda ni Makutano bar kukutana na Mzee Jophu Kundy.

Katika mazungumzo yao walijikuta kufika Makutano bar, “Tafadhali nishushe hapa.Kuna uchochoro gari haliwezi kuingia huko.Shilingi ngapi?”

“Elfu nne zinatosha shem”Jangala alisema akimtizama Getruda.

“Punguza shem.Hujui mimi mteja wako?”

“Petroli imepanda bei sana shem. ‘Any way’ nipe tatu unusu”Jangala alisema .

Getruda alimpatia Jangala elfu tatu na mia tano,akashuka garini. “Usihaike shem.Nitafunga mwenyewe mlango.Mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema baada ya kumuona Getruda anataka kufunga mlango. Getruda alijidai kama anaingia uchochoroni ili Jangala aondoke zake.Alipogeuka aliona gari la Jangala likiishia bali kabisa.Aligeuka na kurudim kuelekea kule Makutano bar.

*****************

INAENDELEA
Powered by Blogger.