KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi na tisa (19)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Ndani ya makutano bar,alionekana mwanaume wa makamo.Kwa kumtizama ungeweza kukisia anamiaka hamsini ama hamsini na tano.Kichwa chake kilikuwa na mvi za kuhesabika.Uso wake ulisha anza kuwa na makunyanzi ya uzee.Alivaa suti ya kahawia,na viatu vya pembe nne ‘Four angile’.Shingoni alinyonga tai ya bluu iliyozidi kumfanya maridadi.Mkononi alivaa saa ya seiko 5 ya dhahabu.Meza aliyoketi ilijaa vyakula na vinywaji.

Mara kwa mara aliinua mkono wake wa kushoto akitizama muda,alipomaliza aligugubia glasi ya bia mdomoni na kuirudishia glasimezani.Pia muda wa kuiacha pombe ishuke vema tumboni alitupa macho yake lako la kuingilia wateja.Safari hii ilikuwa mara ya kumi kutizama lango hilo,alipohamisha macho aliyapeleka kwenye glasi ya kinywaji,akaona kama bia ilishaisha glasini,alikamata chupa ya bia na kumimina kiasi kwenye glasi ya bia.Hakuchelea aligugubia kama mikupuo miwili bila kuishusha mezani,alipomaliza akacheua kama mara tatu hivi,alihisi kilevi kikipanda vema ndani ya ubongo.Akajikuta akicheka mwenyewe

“Mimi ndiye.Mwingine hakuna”Alisema nakutizama simu yake.Aliiokota nakujaribu kupiga,simu aliyopiga iliita bila kupokelewa.

“Shiit.Kwanini hapokei?”alipayuka kwa ghadhabu.

Hakuchoka akapiga mara ya pli,iliita tena,akasikia ikipokelewa “Hallo Prety girl.Uko wapi mbona hupokei simu yangu?”

“Nakaribia jengo la Makutano hapa”

“Sawa. Nakusubiri kwa hamu wa moyo”Walikata simu.Mzee Jophu akawa habandui macho lango la kuingilia,alitaka kumwona Getruda akiingia kwa madaha.Ghafla aliona mlimbwende akiingia kwa mapana na kumfanya kila aliyeko mle ndani kumtupia jicho.Getruda hakuwa mzuri sana wa sura,lakini umbo lake na makalio ndio kichochezi kwa wanaume rijali.Kila alipovuta hatua ,makalio yake yalitikisika mithili ya mawimbi baharini.Nafiki jambo hilo ndilo lililomfanya Mzee Jophu ammezee mate mke wangu.Si kwamba na msifia kwa vile ni mke wangu,hapana.Njoo kwangu Arusha ushuhudie, ukweli wangu.Lakini kwa sasa ni mzee sana.

“Kaaaa, kakaka!”alionekana kijana mmja aliyeko nyuma ya mzee Jophu akihamaki,mfdomo ukiwa wazi kwa mshangao na mkono ukiwa umeshika mdomo wa chini,Jicho likiwa limemtoka kama ndulele iliyoiva.

“Mkindu wavona ilo ibora ledha aho”Kijana huyu alimwambia mwenzake kwa kilugha.

Akimaanisha “Mkindu umeona lisichana hilo linalo kuja hapo?”

“Nikirumo ilo!”Mkindu alijibu.

“Hilo ni balaa!” Wakacheka.

Mzee Jophu alimsindikiza Getruda kwa macho ya matamanio hadi alipomkaribia kabisa.

“Vipi.Mbona umechelewa ?”

“Mume bwege alikuwa akinichelewesha”Getruda aliongea akivuta kiti kilicho wazi.

“Achana nae.Ukisha mkabidhi fisi bucha unamatarajio gani?”

“Kuokota mifupa”Getruda alidakia.

“Hakuna kinachobaki.Fisi gani anakuachia mfupa!”Wakacheka na kupigana mabusu.Kisha akagonga meza.

“Muhudumuuu”aliita.

“Nakuja”sauti ilisikika kwa mbali kidogo.

“Kuja haraka.Watu wanapesa zao hazina pakwenda”Alisema akijiamini kabisa.Getruda alimtizama akagundua mzee Jophu alishaanza kulewa.

“Mpati wa moyo wangu kinywaji chochote anachotaka upesi”Muhudumu akaitikia sawa.

“Dada nikupatie kinywaji gani?”

“Henken ya kopo.Usisahau mrija tafadhali”

“Ya baridi au moto?”

“Aaaa! Vuguvugu.Nitapata?”

“Usihofu,utapata”Muhudumu aliondoka.

“Mpenzi nimekuita nina jambo muhimu la kukueleza,hivyo basi naomba uwemsikivu”Alitulia kidogo na kuokota glasi ya bia,hakuchelewa alimimina bia yote na kurudisha glasi tupu.Akacheua mara mbili nakuendelea “Kwanza kabla ya yote. Napenda unihakikishie kwamba unanipenda”

“Nakupenda sana mpenzi inamaana hujagundua bado?”

“Ninyi wanawake mnabadilika sana.Lazima kila tunapokutana tuulizane jambo hili”

“Si wote bwana.Unajua ninyi wanaume mkionyeshewa kama mnapendwa sana vichwa huvimba na kujiona mna matilaba ya kufanya lolote juu ya mwanamke”

“Ni baadhi ,si mimi Jophu”Akasema na kusogeza kiti jirani na Getruda.Kabla hajaendelea tayari vinywaji vililetwa,Henken ya Getruda na safari ya Mzee Jophu.

“Karibuni”Muhudumu alisema.

“Ahsante”Getruda akajibu.

“Wee binti mwite mchoma nyama tafadhali”Hakukawia kufika mchoma nyama. “Kata nyama ya kidari,ile laini…umeelewa?”

“Ndio,bosi”

“Haya futikaa”Alisema kiulevi ulevi.Akamgeukia Getruda, “Wife,sasa tuendelee na mazungumzo yetu”

“Kama umenidhihirishia unanipenda utakuwa upande wangu kwa lolote lile,si ndivyo”

“Ndivyo”

“Nikisema kitu kwa manufaa yetu lazima tusaidiane,sivyo?”

“Ndivyo”alijibu kiupole hakujua ni jambo gani anataka kuelezwa wakati huo.Kwa sasa Mzee Jophu akapunguza sauti akamweleza Getruda kwa sauti ya chini kabisa.Nafikiri alihofu watu kung’amua maneno yake.

“Getruda naomba iwe siri kubwa sana.Nataka tumuondoe Sweedy Duniani”Getruda alishituka sana kama aliyeamshwa usingizini. “Heee!”

“Usishituke laazizi wangu.Nimeamua hivyo kwa manufaa yetu pia.Kila siku kujiiba iiba ,tutajiiba mpaka lini?.Heri afe tupate uhuru….”

“Haiwezekani Jophu.Unajua dhambi ya kuua lakini?”Getruda aliuliza.

“Acha ujinga, nani kakuambia kuna dhambi.Nani aliyeenda akarudi akasema kuna adhabu kali?.Niambie”

“Kwenye maandiko takatifu,maneno hayo yapo.”Getruda alijibu akimtizama Jophu.

“Kumbe nimaandiko yaliyotungwa kama hadithi tu.Nitajie nani alikufa akafufuka na kutuonyeshea adhabu alizopata ahera?”

“Bwana acha mizengwe yako.Uhusiano wetu hauwezi kuzuilika kwa sababu ya Sweedy”

“Nitakupa chochote lakini tumuue Sweedy.Uko tayari?”Getruda alikaa kimya,safari hii alishindwa kijibu. “Nijibu basi?”Mzee Jophu alimhimiza.

“Nikujibu nini?”

“Kwani hujui.Sina jibu lolote.”Akamtizama Mzee Jophu ,na kuvutakumbukumbu ya siku ya kwanza tulipokuwa kanisani,alikumbuka maneno mengi ya mchungaji.Akanikumbuka nilipompiga busu la kwanza nikiwa namvisha pete ya ndoa.Pia akakumbuka maneno ya mama yake akimweleza juu ya unyumba wetu.Machozi yakamtiririka mashavuni bila kujijua.Akapandisha mkono wa kuume ulioshika leso na kujifuta. Mzee Jophu alinyoosha mkono na kumpatia funguo Getruda.

“Kuanzia dakika hii.Land cruiser iliyoko nje ni mali yako.”Getruda alishangaa hakuamini kile alichokuwa akikiona wakati huo.

“Mpenzi ni kweli ama ni mipombe inakusumbua akili?”

“Sijalewa wa moyo.Ninachohitaji sasa hivi, ni kutoa uhai wa huyu hanithi”Akatulia kama nukta tano hivi ,kisha akasema,“Sawa sawa?”

“Sawa”Getruda alijibu mapigo ya moyo yakimwenda mbio.Alifikiri na kuona kwanza alishachoka kukodi teksi kila siku.Naye alitaka kutembelea gari la kifahari.Alitamani akawatambishie mabinti wenziye aliosoma nao pale Mkuu Rombo.Watajuaje kwamba naye nitajiri pasipo kutembea na gari la kifahari?.Aliamini mtu akiwa na pesa huheshimika kuliko hata kitu chochote duniani.Akajikuta moyo ukipamba na furaha kali, “Acha afe bwana kwani nini bwana. Mtu kama furushi la nguo, heri afe , wangapi wameuawa na kuwaacha wake zao na mapesa kibao.Mungu nisamehe”aliwaza akilini.

Waliendelea kunywa na kula nyama choma pale.Getruda alimaliza bia yake na kuongezwa zingine mbili,tayari ubongo ukafa ganzi.Alianza kuongea sana,tena bila kujali kwamba alisikiwa na watu. “Mpenzi wangu nasema hivi…nitamuua kwa mikono yangu mwenyewe.Haina haja ya kuishi wakati hana sifa ya kumfanya hai. Eti mume, mume gani bwege kilasiku hapandi kitandani mpaka nishikwe na usingizi ndio nae apande!!!!”

“Hatakama ingelikuwa mimi.Ningetumia akili hiyo hiyo.Unafikiri ni kazi ndogo hiyo…fedheha bwana!”

Mzee Jophu na Getruda alikunjwa na kuondoka zao.Walielekea nyumba moja ya wageni ambako waliingiza gari la Gertuda na kujipumzisha.

**************
INAENDELEA
Powered by Blogger.