KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi na sita (16)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Ilimbidi akubaliane na matakwa ya bosi wake, kwa kuwa hakuwa na sauti na alijua Getruda ni mke wangu, asingefanya hivyo kibarua kingeota nyasi haraka.Walichukua chumba, kila aina ya vinywaji viliingizwa chumbani humo bila ya aibu.Kijana alishindwa kuvumilia yote aliyoyaona.Aliumia rohoni na kuona kama yaliyotendwa alitendewa yeye.Hakupenda kuona mke wa tajiri yake akifanya mambo ya kishenzi, tena ofisini kwake bila aibu.

Chumba changu kilijaa utulivu uliovunjwa na muziki wa taratibu uliosikika redioni.Nilikuwa nimejipumzisha kitandani chali, nikiwa nasikilisa mwambao ambao uliniwezesha kusikia mtu ambaye angeponyeza kitufe cha kengele getini. Mawazo yangu yalilenga matatizo yaliokabili mwilini mwangu.Hasa gonjwa ambalo limenifanya nimruhusu mke wangu awe na bosi wangu. Mara simu ilianza kuita,nilishituka na kutizama mahala nilipoiweka.Nilipoiona, nikanyoosha mkono kwenye droo ya kitanda na kuiokota upesi.Sikutizama hata kwenye kioo kuona namba za aliyepiga,niliipokea mara moja na kuipeleka sikioni.

“Hallo Sweedy hapa. Nani mwenzangu?”

Nilisikia upande wa pili ukijibu kwa kuhemea juu juu.“Mimi John naongea, Mzee nimemuona mama amechukua chumba yupo na Mzee mmoja, ameandika jina la mgeni Sweedy dhaifu” sauti ya John iliingia lakini hata hivyo nilihisi masikio kuchuja herufi.Nilishituka na kubaki mdomo wazi nikiwa nimetoa macho kwa mshangaa mkubwa.Nilihisi mapigo ya moyo yakienda kasi zaidi.

“Umesema umemuona mke wangu wapi?”

Sikuamini nilirudia kwa ukali kidogo.

“Hapa hotelini kwako,mzee”

“Khaa,nisubiri nakuja.Wala usiwashitue”

“Sawa,mzee”

Nilikata simu kwa ghadhabu kali.Sikupenda kupoteza muda, nilichukua bastola na kuificha kibindoni. Nilifungua mlango kwa upesi na kutoka varandani, nilionekana kuchanganyikiwa .Nilipofika varandani nikajikuta sikuwa nimevaa viatu.Ndipo niliporudi kuvaa.Nikiwa nje ya jengo ,nilimpigia simu dereva wa teksi niliyefahamiana nae aje kunichukua.Haikuchukua muda , niliona gari jeupe lililo pigwa msitari mweusi katikati likiegeshwa nje kwangu,nilitambua ni gari la bwana Jangala, yule dereva mashuhuri wa teksi pale soko kuu Arusha.

“Bw.Jangala naomba unifikishe hotelini kwangu.Nimesahau kidogo,hivi nikiasi gani?”

“Mzee,umsahaulifu kweli.Unaonekana mwenye mawazo mengi.Kutoka hapa njiro mpaka pale Sakina ni sh,elfu tano tu,mzee”

“Hakuna tabu.Washagari twende.Samahani nina haraka,hivyo ikakupasa kutembea mwendo wa kasi”

“Sawa, mteja kwangu ni mtukufu”Jangala alisema akikanyaga mafuta, wakati huo gari likizunguka ‘Kiplefti’ ya kwanza kutoka kijenge juu.Nilielekea moja kwa moja ilikushuhudia uzalilishaji.

“Ama zangu ama zao, heri niwaue nami nife”Nilitulia kidogo nikitafakari ,nimbinu gani nitumie ilikuwa kuwanasa wote kwa mpigo.Yaani kumkabidhi Jophu imekuwa nongwa.Ajabu ni kwamba hazijapita hata siku mbili ananidhalilisha? Kweli rafiki mkia wa fisi.

***********



Nilionekana kuchanganyikiwa badala ya kuingia chumbani nilijikuta naingia chooni nilistuka ndipo akili ilipo rejea vema. Nilichomoa bastola yangu na kuelekezea mbela tayari kwa vitachumba walichochukua kilikuwa cha mwisho kabisa. Nilipokaribia chumba, nilisikia sauti za kilio kikubwa chumbani humo.

“Oooooo! Jophu unaniumiza unaniua jamani!niachecheeeee!…nakufa!”Sauti ilikuwa nzito ilioitikia

“Tulia mpenzi niku………kuku…….tengeneze.Unana……najua….wewe ..ni mzuri sana lazima nikuoe”Mzee Jophu alikokoteza maneno kwa kigugumizi kikali akiwa kifuani mwa Getruda.

Sauti hiyo ilinilegeza viungo,nikajikuta kuishiwa na nguvu.Machozi yalianza kuchururuzika kwa kasi nilijaribu kuyafuta kwa leso lakini bado haya kukoma.Nilipitisha mkono kuhakikisha kwenye mpini wa bastola kuhakikisha kwamba ipo.Nilipoigusa nikahisi ipo,nikaitoa na kuitizama kwa uchungu sana.Nikasogeza risasi kwanye kifyatuo cha kuruhusu itoke,ilipoitikia ‘Katan’g..katan’g’Nilitikisa kichwa kwa fuhara ya kukusudia kufanya lile nililofikiri kulifanya kwa wakati huo.Nilitembea kwa hadhari mpaka dirishani walimo Getruda na Mzee Jophu.Nilijaribu kuchungulia lakini sikufanikiwa kuona ndani kwakuwa kulikuwa na pazia nzito.Lakini kwa kelele zile ,nilifikiri nikipiga risasi kwa kuhisi ningewaua kwa pamoja.Nilipozidi kusikiliza kelele zao ,niligundua walikuwa karibu na lile dirisha niliposimama.Niliuelekeza mdomo wa bastola yangu aina ya G3 rafles dirishani.Nikaingiza kidole ambacho nilitegemea kuwaulia .Kabla sijafyatua risasi,nilishikwa mkono na mtu aliyekuwa nyuma yangu.

“Kaka usiwaue.Utajiingiza matatani bure.Nenda kapumzike nyumbani,hasira hasara kaka”

Mtu huyo alinisihi akiwa ameing’ang’ania bastola.Kwanza aliniomba nitoe risasi zote zilizomo ndani ya bastola.Nilipofikiri nikaona hakukuwa na ulazima wa kubishana nae.Nilizitoa,akasema “Kaka naomba unipatie hizo risasi .Najua unahasira unaweza kufanya lolote”Nilimpatia nikijua kama ni kujiua basi naweza kutumia njia nyingine.Nilipompatia alizihifadhi mfukloni mwake. Kila nilipofikiria, niliona kuwa sio suluhisho heri kufa mimi kwa aibu niliondoka eneo lile, wahudumu walikusanyika wakinitazama kwa huruma, wengine waliniomba niende niachane nao.

Waliendelea kuvuta raha na wote waliyafurahia mapenzi yao, hasa Getruda aliamini amepata mwanaume bora, ambaye asingemdhulumu haki ya unyumba. Alitumaini na alitamani kuzaa na mzee Jophu ili kuondoa maneno ya mtaani kuwa ni mgumba, alitegemea msaada mkubwa na juhudi za Mzee Jophu ili naye aitwe mama.

Niliona Dunia chungu mithili ya shubira, kila nilipo kumbuka maneno ya Getruda na Mzee Jophu nilitamani nisitishe uhai wangu, sikuwa njia nyingine ya kuwepuka aibu ile, wakati na waza nafasi nyingine ilininyima kufanya uamuzi huo na kunitaka niwe na subira. Niliamua kunywa pombe ili kupunguza mawazo lakini mawazo yalizidi kutawala ubongo wangu kadri nilivyokunywa, niliamua kusitisha kilevi, Sononeko liliendelea kunitawala, nikajiona ni mtu dhaifu kuliko watu dhaifu wote duniani. Muda mwingine nilijaribu kufariji kuwa ipo siku mungu atasikia kilio changu na kunipa nguvu za ajabu,Maneno, “MUNGU UNAJUA MATESO YANGU” yakawa gumzo akilini kila siku.

“Yaani mke wangu ananidhalilisha kiasi hiki? Kweli yote haya ni kwasababu ya udhaifu wangu,naamini mungu atasikia kilio cha mja wake na ataniponya gonjwa hili na kunipa nguvu ili kuinusuru ndoa yangu isivunjike”Niliongea huku nikiwa nimefumba macho, kichwa nikiwa nimekiinamisha, kikiwa kina saidiwa kushikiliwa na viganja vya mikono.

Pamoja na mawazo, hasira za kudhalilishwa. Bado nilikuwa na mpenda mke wangu, nilimsubiri aje tukajipumzisha chumbani na kuongea utofauti uliojitokeza. Kila nilipotizama saa ya ukutani, niliona mshale kama unaenda mbele na kurudi nyuma, hali ile iliniadhiri kisaikolojia. Nilikuwa nikiingia chumbani na kutoka, chooni na kutoka bila kufanya chochote. Nilitamani kulala lakini sikupata hata tepe la usingizi. Nilijikuta kutomlaumu tena mke wangu,kwani yote ni kwa sababu sikuweza kumtimizia haki yake, nafsi nyingiune ilipinga na kusema “Matendo aliyofanya ni ukosefu wa adabu na kutoheshimu unyumba, kwanini asifanye siri?”.Kila nilipokumbuka macho yalijaa machozi.

*****************

INAENDELEA
Powered by Blogger.