KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi (10)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Getruda alisema kwa hasira baada ya kunitengea chai mezani.

Nilishindwa hata kuokota kikombe nikabaki nimeduwaa. Nikanyamaza kimya, nilishindwa niongee uwongo gani,kwani kila siku nilikuwa muongo wa kupindukia,mara naumwa, mara nimechoka kazini, mara sijisikii,zote hizo zilikuwa njia za kukwepa aibu.

“Sema”Mke wangu alifoka kwa kunihimiza.

“Kwani baada ya ndoa ni haki kunitendea hivi?Kila siku hupandi kitandani mpaka mimi nishikwe na usingizi………”

Nilinyamaza kwa muda dakika tatu, kichwa nikiwa nimekiinamisha kama kondoo, kisha nikameza mate na kulamba mdomo, kila nilipotaka kuongea nilijikuta machozi yakitiririka kwa kasi,nilihisi labda nililogwa na walimwengu,kweli imani ya kishirikina ilitawala ndani ya ubongo.Niliamua kujikaza na kuanza kuongoa uwongo.

“Mke wangu shughuli zangu nzito sana, halafu ni za usiku mno!huwa nachoka nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.

“Eti nini? kwa hiyo kuna wengine unaofanya nao?. Si ndio, hao machangu wa shule ndio wanakusababishia unione kama mboga zilizochacha eee!.Eti nashindwa kufanya tendo la ndoa na wewe”.Mke wangu aliongea kwa kufoka huku akibana sauti na pua akiniigiza nilivyo sema.

“Hapana mke wangu” nilimjibu kwa sauti ya kidhaifu iliojaa uwoga na simanzi. Nilikuwa niiingia baa na kunywa, niliporejea nyumbani uliku usiku wa manane nikiwa chakari. Mke wangu hakuweza kugundua mapema, hata mimi mwenyewe sikujua ugonjwa huu niliupata wapi.

“Mume wangu”



“Naam mke wangu”Nilimwitikia nikiwa nimeangalia chini,kwa mbali mapigo ya moyo yalinidunda.

“Eti unasubutu kuniitikia.Wewe mwanaume kweli?”

Sikutegemea maneno hayo.Nikahisi mwili kufa ganzi.Nilijiona ninaye dhalilisha hapa ulimwenguni.

“Unafurahia nikuite mume wangu,sivyo?”

“Ndio”Nikaitikia kwa sauti ambayo hata mimi mwenyewe sikuisikia vizuri.

Nikanyamaza,nilijikuta machozi yakinitoka.Kwa kweli moyo uliniuma lakini sikuwa na lakufanya.

“Sasa unataka nikuite mume wangu wakati huwezi?”

“Getruda siwezi nini?”

“Kwani umenioa ilinikupikie tu?”

“Hapana”Nilijibu kwa hofu.

“Sasa unategemea mimi nitaishi vipi?”Safari hii Getruda alishika kiuno.

“Mke wangu vuta subira,nitapona”

“Kwani unaumwa?”

“Ndio, sin’shakuambia naumwa?”Nilikuwa na kila sababu ya kumnyenyekea.

“Hivi Sweedy unataka kunifanya mtoto.Kwa taarifa yako nimeshajua siri zako.Juzi umeshikwa ugoni na mwanafunzi ukatozwa laki saba.Na nimepata tetesi kwamba unapenda hawa wa kusoma”Getruda alinishikia kibwebwe.

“Huu ni uzushi wa watu wasipenda niwe nawe.Naomba usisikilize maneno ya wafitini”

“Sio wafitini.Niwatu wanaokujua kwa ukaribu tabia yako”



Zogo lilikuwa kubwa ambalo lilichukua masaa sita.Baada ya hapo mke wangu akaondoka kwenda mjini.

Hakuwa na safari bali aliamua kwenda mjini kununua gazeti la Mwanasport, lililoandikwa mwongozo wa kumridhisha mwenzi kiunyumba, na kuliweka kwenye meza makusudi ilinilione.

“Haya nakuuliza umesoma gazeti nililokuwekea kwenye meza?”

“Gazeti lipi mke wangu?” nilimuuliza kwa sauti ya chini.

“Hili hapa” mke wangu alinionyesha huku akinipatia nisome.

“Mwongozo wa njia za kumridhisha mwenzi kiunyumba”

“Aaaaa! Gazeti hili, kipengele hiki nisha soma….” Nilijaribu kuchangamka kijanja, lakini huzuni ilibaki pale pale.

“Uongo” Getruda alinishupalia

“Haki ya Mungu, nimesoma kipengele hicho tena kinasisitiza swala la unyumba, mume amtendee haki mkewe na mkewe amtendee mume haki yake, tena hii hapa….” Nilijaribu kujitetea kwa unafiki.

Nilichukuwa gazeti lile na kupitisha macho juu juu kwa haraka na kumwambia nimesoma ndani vizuri. Nilifahamu sana nia yake haswa ilikuwa ni nini? Nilimtizama mke wangu kwa masikitiko na kumuonea huruma, lakini ningefanya nini ili kumridhisha, nae aridhike japo mara moja.

“Samahani mke wangu siku hizi na choka kwa shughuli nzito si mchana wala usiku, hata nimesahau kufanya mapenzi nawe”

“Hivi wewe unavyosema siku hivi, ina maana toka tufunge ndoa, tumeshafanya chochote na sasa karibu miezi miwili na nusu?”

“Basi ni samehe mke wangu”

“Nikusamehe kwa lipi?. Usinipotezee muda ninachoomba ni haki yangu bwana”



ITAENDELEA

Powered by Blogger.