KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Tisa (9)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Kwanini usingenieleza kabla, umenitesa naunaendelea kunitesa. Utafanya nini ilikunisaidia, najisikia vibaya sana mwenzio” aliongea kwa sauti ya chini akiwa anadondosha machozi, mwili wake ulikuwa umelegea, macho mekundu na ya kurembua, hakuweza kuvumilia zaidi ya kulia kwa kwikwi, alitamani niondoe hali ya ubikira na kumpeleka kwenye utu uzima. Maneno ya Getruda yaliniumiza moyo wangu, nilimuonea huruma alivyokuwa akijigaragaza kitandani. Machozi yalichuruzika kwa kasi nilizidi kuwaza.

“Au ni kwa vile ndio mara ya kwanza kukutana naye nini?. Lakini hapana sijapaniki” labda ni uzuri wake unanichanganya nini? . Au ni chango la tumbo limesababisha nini?.Sasa tatizo hili litaniumbua” Nilijiuliza bila kupata muafaka wala sikuweza kuhisi kitu chochote zaidi ya ugonjwa wa kawaida. Tuliupitisha usiku huo usio na ladha ya mapenzi, si mimi wala Getruda wote tulihuzunika.

************

Kwa ujumla maisha ya ndoa niliyaona machungu kama shubiri na pengine machungu kama mitishamba. Nilishindwa kuelewa ugonjwa huo ulitokea wapi na umesababishwa na nini? Nyumbani kwangu nilipaona kama jehanamu, sikuona raha kuwa nyumbani kwani mke wangu alikuwa ananilalamikia kila siku , kila dakika kuhusu ndoa yetu. Tofauti na ndoa nyingine zikiwa changa, watu huwa wanatamani wapate hata likizo ya miezi kadhaa ili wawe pamoja na wandani wao, hapo nasemea kwa wale wafanyakazi kama mimi.Mimi Sweedy kama mtu mwenye uwezo wa kutunga uongo basi nilijitahidi kumridhisha kwa maneno matamu niliyoamini yangemfariji. Uwongo una mwisho wake kumbuka hapo. Lakini hata hivyo ni mtu gani atasikiliza uwongo kila siku. “Kuumwa kuumwa ni kuumwa gani hukokusikoisha?”.

Nilikuwa natoka kazini saa kumi jioni, lakini cha ajabu nilikuwa nikitafuta sehemu ya kupoteza muda ili mradi nirudi nyumbani usiku. Nikiamini mke wangu atakuwa amelala. Siku zote nilitumia njia hiyo, hata kunywa pombe nikajifunza ilimradi nikwepe kugungulika udhaifu wangu.Si mitishamba wala hospitali za kawaida kote nilienda bado ikawa si kitu.

Siku moja mke wangu aliamua kuelekea kazini kuuliza kuhusu ratiba ya kazi zangu. Alimkuta Mzee Jophu mwenyewe.

“Shikamoo baba” Mke wangu akamsalimu pale alipofungua mlango wa Mzee Jophu.

“Marahabaa mchumba mzuri”Mzee Jophu akaitikia salamu kamavile anamuona mke wangu mtoto mdogo.

Hata hivo Getruda ,mke wangu hakujali aliona ni utani tu kwani anajua dhahiri ni shemeji yake.

“Shemeji nimekuja ninashida”Getruda akasema na kusubiri kitu ambacho angeelezwa. Mzee Jophu alionekana kutingwa na shughuli nyingi pale ofisini.

Aliinua kichwa chake na kumtizama Getruda kwa macho ya huba.

“Shida gani shemeji?”

“Wala usishituke ni shida ndogo tu”Getruda akasema akiweka pete yake ya ndoa vema.

“Shemu sema kama ni pesa. Nikupatia au nimambo ya familia unataka kunieleza?”

“Ndio, ulijua je?”

“Najua maana nyie wanawake mmeumbwa na aibu sana. Jambo dogo unaweza ukaogopa kumueleza mwanaume”

“Nijambo dogo kwa kulitizama lakini kwa undani nijambo kubwa”

“Sawa ulitaka tukalizungumzie faragha kidogo?”

“Hapana shem. Naomba nikueleze hapa hapa”

“Sawa nimekuruhusu. Lakini nilipendelea tutoke tukazungumze nje ya ofisi kwani mambo ambayo haya husiani na ofisi tunayazungumzia nje ya ofisi”

“Naomba nizungumzie hapa , ni kwamba sitatumia hata dakika tatu”

“Ok, sema”

“Naomba unieleze, mume wangu anatoka kazini saa ngapi?”

“Wewe kwani kakuambia anatoka saa ngapi?”Mzee Jophu hakujibu swali kama alivyoulizwa bali nae aliligeuza swali upande wa Mke wangu.

“Anasema saa tano usiku”

“Basi inawezekana, kwani mama unaweza kuniambia, maana ya kazi?”

Mzee Jophu alimuuliza swali kwa mtego wa kasa

“Kazi kama ninavyoifahamu ni kitu au ni shuhuli inayoniletea kipato,”

“Ahaa kumbe unajua, mama nenda nitakuambia, maana yake siku nyingine ukiwa na muda.”

“Lakini bado hujanijibu mume wangu hutoka saa ngapi kazi kwako?”

“Saa kumi jioni?”

“Kaaa!. Saa kumi jioni halafu hufika nyumbani saa sita usiku?”

“Inamaana Sweedy hurudi nyumbani usiku?”Mzee Jophu alimtolea Getruda macho ya mshangao, huku akishika kiuno kana kwamba haamini maneno ya Getruda.

“Ndio shemeji”

“Siamini kabisa. Siku zingine huwa na mruhusu saa tisa na siku za jumamosi anatoka saa sita mchana”Mzee Jophu alizidi kuongezea chumvi.Nia yake ni kuvunja ndoa yangu ili afaidi yeye.Alipania kuvuruga ndoa yangu.Siku jua hata nguvu zangu ya kiume zilipoisha ni kwasababu yake.Yeye ndiye alituma watu ambao walivaa kama Daktari kuja kunipiga sindano ya kuua nguvu ya kiume.

“Shemeji inamaana maneno yako niyakweli kabisa”

“Shem nikudanganye iliiweje?.Sitaki kukuvunjia ndoa yako lakini ukweli mumeo hakupendi. Anasema sana kila siku hapa kazini kwamba mpaka sasa hajawahi kufanya tendo la ndoa na wewe.Eti mke gani wa kutafutiwa na wazazi.Anampango wa kukufanya kijakazi pale nyumbani kwake….”

“Eti nini?.Shemeji naweza kuyaamini maneno yako kwani ni miezi miwili sasa hajanigusa kabisa. Kila siku anasingizia kuchoka na kuumwa.Raha ya ndoa iko wapi shem?.Naomba unipe ushauri nimechoka kuvumilia na mateso haya”

“Usichoke shemeji vumilia tabia itabadilika. Yule bwana anapenda watoto wa shule sana na mshahara wake mwingi huishia huko.Juzi tu kashikwa ugoni na mtoto wa shulwe ambapo alitolea faini laki saba, huwezi kuamini lakini ndivyo ilivyotokea. Mumeo ni mkware kweli…Naomab ausije ukamueleza maneno haya naomba ufanye siri, nitakueleza mengi siwezi kuvumilia ukateseka bure binti wa watu”

“Ahsante sana. Leo atanikoma nyumbani”Getruda aliondoka akiwa na mawazo chungu zima.Machozi yalimlenga lenga machoni.Moyo uliuuma sana. Waliagana na Getruda, lakini moyoni Mzee Jophu alibaki na sononeko la upendo kwa mke wangu, Na aliamini kumpata, kwa jinsi alivyo nitumia Daktari wanipige sindano ya kuuwa nguvu za kiume, aliamini njia hiyo aliyotumia ya kuuwa nguvu za uume,wangu ungeshindika kumpata Mke wangu basi angeniuwa kabisa

“Yaani Sweedy ndivyo alivyo?.Nimemtunzia boma langu iliawe wa kwanza kulibomoa lakini hataki, anapambana na watoto wa shule?.Haipiti hata siku moja haachi kusema naumwa sijui kichomi mara nimechoka kumbe anachoshwa na hao makahaba wa shule?”Getruda alizidi kuwaza njia nzima .Hakuwa anaelewa sehemu alipokuwa alisha pita nyumba yetu.

Ilikuwa siku ya juma mosi siku hii aliyotokea kazini,hakuweza kuzungumza chochote na mimi.Alionekana mwenye ghadhabu kali . Hakutaka hata kunikaribia, alikwenda kujipumzisha kitandani.Macho yake fika yalinijulisha kwamba alikasirika sana. Nami niliogopa kumuuliza kwani nilijua lazima alichukia kutokana na matatizo yangu.Sikuwa nalingine kichwani.Wakati wa kulala ulipofika ,nilitoka sebleni ambako nilikuwa nikitizama mkanda wa dini, na kuelekea chumbani.Nilijawa na wasiwasi kwamba usiku huo kungekuwa na kitimtim kikali, dalili niliiona toka mapema kabisa.Sikuwa na amani na maisha yangu, hofu kubwa ilikuwa kwa mke wangu ambaye hakuwa na raha kila aliponiona.Sasa hasira yake ikawa kubwa pale alipopewa maneno ya uchochezi na tajiri yangu.Nilitembea kwa kunyata ilitu asisikie kwamba naelekea kitandani.Kwa sasa nikajongea na kukifikia kitanda.Nilipandisha mguu wa kushoto kwa hadhari sana asishituke. Pia nilihakikisha kitanda hakichezi, jambo hilo nililifanya kwa makini zaidi.Wakati huu napandisha mguu macho yangu yalitizama usoni kwamba mke wangu angeshituka ama vipi. Nilifanikiwa kupandisha mguu wa kwanza, sasa nikajaribu wa pili kuupandisha kitandani. Laiti ningekuwa na uwezo ningejitafutia kitanda changu.Ukweli ndoa yangu niliiona chungu na iliyojaa mateso makubwa sana. Nilikuwa mtu wa wasiwasi tupu.Kitu kingine, nilijiona nisiye na dhamani duniani, nilitamani nife kuliko kuishi kwa shida lakini wasiwasi wangu ukawa huko ahera nikukimbiliako je? Ni kwema aba ndio nitakimbilia mateso mengine?.Nilizidi kuzama kwenye dimbi la mawazo.

Nikafanikiwa kupanda kitandani bila mkewangu kushituka,nilihisi angeshituka angetaka tendo la ndoa wakati huo huo.Sikutaka kulala zaidi ya kulala macho wazi, nilijua nikishikwa na usingizi ningeweza kukoroma ambapo mke wangu angeamka, kwani nilijijua toka niliwa shuleni kwamba nimkoromaji mkubwa hata mtu nyumba ya jirani angesikia.

Sikulala kabisa, nilihakikisha simgusi hata kwa shuka ambapo angeamka na kunisumbua.Saa kumi na robo nilisikia jooo za jirani zikiwika nikajua kwamba kunakaribia kupambazuka. Nikiwa kitandani nilishuhudia miale ya mwanga ikiingia kupitia dirishani.Nikajua tayari palisha kucha.Mpaka wakati huo mke wangu hajazugumza kitu chochote na mimi.

Ilikuwa siku ya Jumapili,siku ya mapumziko,nilikuwa nyumbani na Mke wangu lakini maongezi yetu yalikuwa juu ya unyumba wetu,si kuhusu maendeleo.

“Hivi mume wangu umenioa ili niwe pambo lako au kama TV unitizame tu au laa!.Naomba unieleze nimevumilia vya kutosha”

Inaendeleaah
Powered by Blogger.