KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo: Mwajuma Utamu Sehemu Ya Nne (4)

Ni katika kipindi hicho ambapo kumbukumbu za nyumbani kwetu zikaanza kunijia, nilipakumbuka mno, nilitamani kuambiwa kuwa nilitakiwa kurudi nyumbani kwetu lakini jambo hilo halikuweza kutokea hata mara moja.

Nitaishi maisha ya vitisho mpaka lini? Hili lilikuwa ni swali lililoniumiza usiku na mchana, nilikosa wa kumsimulia maisha niliyokuwa nikiyapitia kwa wakati huo.
Baada ya kupita mwezi mmoja huku nikiendelea kuishi maisha ya vitisho, siku moja majira ya usiku Mama Daniel aliniita na kuniambia kuwa alifahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea, aligundua kuwa nilikuwa nikitembea na mume wake jambo ambalo lilimuumiza mno.

"Mwajuma msaada wangu wote niliyokusaidia katika maisha yako leo umeamua kunilipa kwa kutembea na mume wangu kweli?" aliniuliza, wakati huo machozi yalikuwa yakimbubujika mashavuni mwake.

"Hapana Mama nili...." kabla sijamaliza kuzungumza alinikata kauli, nilishtukia nikipigwa kofi moja zito lililoniyumbisha, wakati nikiendelea kuugulia maumivu ya kofi, hakuishia hapo, alianza kunipiga kila sehemu ya mwili wangu huku akinilaani kwa kitendo nilichomfanyia. Nilipata maumivu makali mno, siwezi kuyaelezea maumivu niliyokuwa nikiyapa, nililia sana, nilimuomba kila aina ya msamaha lakini sikuweza kuambulia jibu lolote zaidi ya kipigo kikali kama cha mbwa koko na mwisho wa siku aliweza kunifukuza.


Nilifukuzwa kama mbwa usiku huo, nilitupiwa begi langu la nguo na kupewa kila kilichokuwa changu. Nililipwa pesa yangu ya mshahara wa mwezi uliyopita niliyokuwa nikidai pamoja na mwezi huo ambao niliweza kulipwa nusu yake.
Hakukuwa na mtu ambaye alinisaidia siku hiyo, nilionekana kuwa mbaya kupita kawaida, niligeuka kuwa adui. Kuna muda nikatamani nimwambie kila kitu kuhusu mume wake lakini nilikosa muda huo, tayari nilishafukuzwa na sikuhitajika tena kuwemo katika familia hiyo.
Sikujua nilitakiwa kwenda wapi usiku huo, nilipolifikiria hilo nikazidi kuchanganyikiwa.

Nilijutia mambo mengi mno lakini kubwa nililolijutia ni hili la kutembea na mume wa mtu, tamaa yangu ya pesa iliniponza na kuniweka katika wakati mgumu ambao sikutegemea kuupitia.

Machozi yalikuwa yakinidondoka muda wote, kila hatua niliyokuwa nikiipiga njiani nilipishana na watu wengi, baadhi yao walinishangaa kutokana na muonekano niliyokuwa nao, ulitosha kabisa kunielezea kuwa nilifukuzwa na muda huo nilikuwa katika safari nisiyoifahamu mwisho wake.

Nilitembea umbali mrefu sana mwisho nilichoka, sikuwa nikifahamu sehemu hiyo au mtaa huo niliyokuwepo uliitwaje.

Niliwaona wanaume wawili wakinifuata nyuma yangu, mwanzo sikutaka kuogopa kitu kwani kulikuwepo na watu wengi niliyopishana nao hivyo niliamini kuwa salama lakini nilipofika eneo hilo nilishangaa nikiwa peke yangu, hakukuwa na mtu niliyepishana naye zaidi yangu na hao wanaume wawili waliyokuwa wakinifuata.
Powered by Blogger.