KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo: Mwajuma Utamu Sehemu Ya Tano (5)


Nilianza kuingiwa na wasiwasi baada ya kuwaona wakizidi kukazana kunifikia, moyo wangu ukalipuka paaa!! hofu ikanitawala, mapigo ya moyo wangu yakaanza kunienda kasi.


"Habari yako binti," alinisalimia mwanaume mmoja huku yule mwingine nikimuona akiangalia huku na kule, nilifahamu hawakuwa na nia nzuri na mimi. Hofu ikazidi kunitawala.

"Nzuri," nilijibu huku nikitetemeka.
"Mbona unaogopa usiogope sisi ni watu wazuri unaitwa nani?" aliniuliza yule mwanaume mwingine.
"Naitwa Mwajuma,"nilimjibu.
Walitazamana kisha wakapeana ishara fulani, sikujua walimaanisha nini ila nikashangaa wakinisogelea, ghafla! yule mwanaume wa kwanza akanirukia na kunikaba, nilishtukia nikipigwa na ubapa wa panga kwenye paja na kuambiwa nisipige kelele na endapo kama ningekiuka agizo hilo ningeweza kuuliwa, niliogopa mno, nilibaki nikiugulia maumivu ya ubapa wa panga pamoja na kabali niliyokuwa nimepigwa.

Yule mwanaume mwingine alianza kunisachi, akachukua simu, pesa pamoja na lile begi la nguo. Alipojiridhisha kuwa alifanikiwa kuchukua kila kitu changu alimpa ishara mwenzake na ndipo hapo alipoweza kuniachia.
"Sasa sikia wewe fala ukipiga kelele tunakuua, kaa kimya hivyohivyo," aliniambia kisha akanitukana tusi la nguoni.

Nikabaki kimya huku nikiendelea kuugulia maumivu niliyoyapata. Wale wanaume wakakimbia eneo hilo.
Wakati nikiendelea kuugulia maumivu huku nikiwa sijui nini nifanye mara akatokea mwanaume mmoja ambapo aliponiona alinifuata na kuniuliza nilikuwa na tatizo gani?
"Nimeibiwa kaka yangu, wameniibia," nilimwambia huku nikionekana kuchanganyikiwa.
"Embu subiri kwanza akina nani hao wamekuibia?" aliniuliza.
"Siwajui, siwajui kaka angu" nilimjibu huku nikianza kulia.
"Usilie sasa taratibu niambie kwanza unatokea wapi na unaitwa nani?"
"Naitwa Mwajuma nimetokea huko nilipokuwa nafanya kazi za ndani."
"Wapi?"
"Kijitonyama."
"Sasa huku umekuja kufanyaje?"
"Wapi?"
"Kwani unajua hapa upo wapi?"
"Hapana sijui kaka angu kwani hapa ni wapi?
" Tandale," alinijibu kisha akaanza kunionea huruma,
"Umesema umetokea Kijitonyama?'
" Ndiyo."

"Kwanini sasa wamekuruhusu kuja sehemu kama hii usiku?"
"Hapana nimefukuzwa," nilimjibu kisha akaonekana kunihurumia zaidi.
Mpaka kufikia muda huo nilikuwa bado sijalifahamu jina lake, alinitazama kama niliumia sana lakini hakukuwa na majeraha niliyoyapata zaidi ya kuugulia maumivu ya ndani kwa ndani. Hakutaka kuona nikiendelea kubaki eneo hilo kwani aliniambia mtaa huo palikuwa na vibaka wengi sana, hakuishia hapo alizidi kunipa sofa mbaya za mtaa huo hivyo kitendo cha mimi kuendelea kuwepo mahali hapo kingeweza kunihatarishia maisha yangu.

Baada ya kusikia kuwa nilifukuzwa na sikuwa na mahali pa kwenda usiku huo, alihitaji kunisaidia. Aliniambia alikuwa akiishi peke yake hivyo kama nisinge jali anichuke na kwenda naye kwake usiku huo.

ITAENDELEA

Powered by Blogger.