KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo: Mwajuma Utamu Sehemu Ya Sita (6)

Kiukweli sikuweza kumkubalia kirahisi, nilihofia mambo mengi mabaya ambayo angeweza kunifanyia lakini baada ya kunohakikishia kuwa ningekuwa salama na kuniondoa hofu ilibidi nimkubalie. Akanichukua na kunipeleka mpaka kwake.
Kilikuwa ni chumba kimoja, nilipofika nilifikiria ni jinsi gani ambavyo ningeweza kulala humo lakini hilo halikuwa tatizo. Yule mwanaume aliniambia kuwa nilitakiwa kulala kitandani na yeye angelala chini na maisha yangeendelea hivyo.


Ngoja nikuambie kitu msichana mwenzangu, kijana mwenzangu unayeisoma simulizi hii. Unajua kwenye haya maisha unaweza ukakutana na vikwazo vingi lakini baadhi ya watu wanaokutazama wakakuchukulia kuwa hayo yote unayopitia ni haki yako, wengine wanaweza kwenda mbali zaidi na kukutukana na kukulaumu kwa ujinga uliyoufanya.

Yote haya yanaweza yakatokea katika maisha na kitu unachotakiwa kukifanya ni kujua ni jinsi gani ambavyo unatakiwa kupambana nayo na si muda wa kujilaumu na kuona kama wewe ni mkosani mbele za Mungu na hutakiwi kusamehewa.
Kwanini nakwambia haya ni kwasababu ya makosa niliyoyafanya katika maisha yangu, ujinga niliyoufanya, sitaki urudie makosa yangu sitaki urudie kufanya ujinga wangu, nataka ujifunze kitu kupitia simulizi hii ya maisha yangu.
Angalia kwa muda ambao niliweza kukutana na mwanaume ambaye hata sikuwa nikilifahamu jina lake tayari nilimuamini, niliukubali msaada aliyohitaji kunipa, bila kufuata taratibu zozote nikajikuta nikiingia ndani kwake na maisha yakaanzia hapo.
Mwanzoni alionyesha moyo wa kunisaidia kweli, aliguswa na simulizi yangu ya kufukuzwa, hakujua nini kilisababiaha ila moja kwa moja aliamini nilionewa hivyo alihitaji kunisaidia.

Maisha yalianzia hapo huku kila siku mwanaume huyo akiniaga kwenda kwenye mihangaiko yake. Aligeuka kuwa msaada mkubwa sana kwangu, alinihudumia kwa kila kitu nilichokuwa nikikihitaji, maisha yalikuwa rahisi kwangu.

CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Ama kwa hakika penzi ni kikohozi kama wasemavyo wahenga, baada ya kupita siku kadhaa nikajikuta nikiwa katika mahusiano na mwanaume huyo ambaye nilifanikiwa kulifahamu jina lake tayari. Nakumbuka alijitambusha kwa jina la Oscar, ni katika penzi hili ambalo lilienda kunipa funzo lingine jipya la maisha yangu.

Nilijikuta nikizama kwenye dimbwi la kimapenzi na Oscar, huyu alikuwa ni mpiga picha, alikuwa akimiliki studio yake ya picha iliyokuwepo Sinza Palestina.
Kimuonekano alikuwa ni kijana mtanashati, kiukweli nilitokea kumpenda kwa moyo wangu wote. Kipindi nipo katika mahusiano naye nilisahau shida na matatizo yote niliyokutana nayo katika maisha yangu, sikutaka kukumbuka kitu chochote kilichotokea nyuma.
Oscar alinipenda sana, ahadi zake za kunioa ndizo zilizonifanya nikazidi kumuamini mara dufu, bila kujali nikamkabidhi mwili wangu ambao aliutumia autakavyo.

Maisha yalibadilika kwa kiasi fulani, nilikuwa nikiishi maisha yenye furaha, Oscar aliendelea kunijali, alinipa matunzo pamoja na mapenzi moto moto.
Kiukweli wazo la kurudi nyumbani kichwani mwangu halikuwepo kabisa kwa wakati huo, niliona ni jambo gumu mno kurudi katika maisha ya kimasikini niliyozaliwa katika familia yetu.
Nilikuwa nikiishi maisha ya furaha yaliyogubikwa na amani tele, sasa kwanini nikumbuke maisha ya kimasikini ya nyumbani kwetu?
Hilo lilikuwa ni jambo gumu mno kutokea.
Siku ziliendelea kukatika huku penzi likizidi kupamba moto, Oscar aliendelea na kazi yake ya upiga picha, muda mwingi aliutumia katika kazi yake hiyo, mwanzoni sikuwa na wasiwasi wowote, niliamini katika mapenzi ya dhati pamoja kazi yake, sikutaka kumuwazia vibaya.

Baada ya kupitia mwezi mmoja nilianza kusikia maneno ya chinichini kutoka kwa majirani ambao tayari nilianza kuwazoea. Waliniambia kuwa Oscar alikuwa ni mume wa mtu na kipindi hicho mke wake alikuwa amesafiri.
Nilipoyasikia maneno hayo sikutaka kuamini hata kidogo, nilihisi walipanga kutugombanisha hivyo sikutaka kuyapa uzito maneno yao.
Maisha yaliendelea huku kila siku maneno yakiwa ni yaleyale. Mwanzoni nilionekana kuyapuuzia lakini nilipoona yamezidi ilibidi nimuulize Oscar.
"Nani kakuambia maneno hayo?" aliniuliza huku akionekana kukubwa na mshangao.

"Kuna watu wameniambia," nilimjibu.
"Nilikwambia usipende kuamini kila unachoambiwa," aliniambia.
Kiukweli ilikuwa ni vigumu kuamini kama Oscar alikuwa akinidanganya, alionekana kumaanisha kila kitu alichokuwa akikizungumza, hakutaka kuona nikiendelea kuyasikiliza maneno ya watu ambayo yangeweza kuvuruga amani ya mapenzi yetu.

Hilo lilizidi kunifanya nimuamini sana Oscar kupita maelezo hata pale nilipokuwa nikitahadharishwa na watu sikutaka kuwasikiliza, niliwaona ni binadamu wenye nia mbaya kwangu, hawakupenda mafanikio yangu.
Powered by Blogger.