KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Ni Shiida! Sehemu Ya Kumi na Tatu (13)

 LOVE STORY: ni shiidaI - 4
Aliongea Juliana huku akiwa ameshaingia ndani na kumuacha mhudumu nje akiwa mdomo wazi. Kitendo cha kuingia kwenye kile chumba alikikuta kitupu, macho ya Juliana yaligongana na nguo za mama yake sambamba na mkoba uliokuwa kitandani pale, hakujiamini mara mbilimbili kama alikuwa ni mama yake.

"Lazima watakuwa wameingia kuoga tu!"
Alijiongelea Juliana huku akipiga hatua kuelekea kwenye bafu ambalo lilikuwa ndani mulemule. Alipokaribia katika mlango wa lile bafu aligundua kuwa haukuwa umefungwa, hivyo akausukuma kidogo na kuchungulia kwa jicho moja. Alimshuhudia mama yake akiwa anamsugua mgongo Bitungu, Bitungu naye akimsugua mama Juliana huku wakifurahia kwa kupigana mabusu.

Baada ya kusuguana kwa muda wakajimwagia maji kuondoa mapovu kisha Bitungu akataka kufanya mambo mulemule bafuni...
"Mhh sasa naona mechi yetu kama tukaihamishie kule kwenye uwanja mkubwa maana nahisi huu si uwanja mzuri..."

"Kwani una nini sweet!"
"Wee huoni, vichuguu kila kona, hata mashuti unayopiga nashindwa kuyadaka vizuri!"
"Ni kweli sweet lakini ngoja kwanza nikijikwaa tu ndiyo tuh..."
"Ukijikwaa nini, sitaki kusubiri mpaka ujikwae, miye nainuka bwana!"
"Hapana Sweet subiri kwanza!"

Muda wote Juliana alikuwa akiwapiga jicho kupitia kaupenyo kadogo kwenye mlango, mzuka ulionekana kumpanda hata lile wazo la kutaka kuwafumania likakaukia kwenye ubongo wake kwa muda mfupi.
"Inamaana Bitungu ndiyo mchezo wake enhh!, kwangu miye anajifanya kunibania kwa mama anampa vyote!"

Aliendelea kujisemea Juliana huku akiwa bado kauinamia mlango.
Ndani ya muda mchache Bitungu na mama Juliana walikuwa katika mapumziko ya mechi yao, mama Juliana alikuwa hoi hajiwezi huku Bitungu akishughulika kwa kumvalisha khanga yake.
"Vaa basi jezi yako, tukapumzikie kule!"
"Baby!"

"Nambie!"
"Usinivalishe hiyo khanga kwanza!"
"Kwa nini?"
"Hivi umeniroga ama nini?"
"Kwani vipi sweet?"

"Yaani haiwezekani hata mechi ya kwenye uwanja mbovu uwe unaijulia kiasi hiki!"
"Nilishakwambia miye fundi wa mipira iliyokufa, kiwanja chochote unachokitaka tunaweza kucheza na nikatoka na ushindi tena ule wa kishindo." Aliongea Bitungu kwa kujisifu.

Maneno yale yalipata kusafiri hadi kwenye ubongo wa Juliana, akayanasa kwa hasira ya hali ya juu sambamba na macho yakimkakamaa.
"Bitungu... Bitunguuuu?"

Juliana alijikuta akitoa sauti ya ukali akilitaja jina la Bitungu kwa sauti ya juu, moyoni mwake alishakubaliana na lolote litokee. Alichokifanya kabla Bitungu na mama Juliana hawajatoka mle bafuni, alifungua kitasa cha mlango ule na kutaka kuingia ndani.
"Unafanyaje chumba hiki?"

Sauti nene na kali ya kiume ilimhoji Juliana. Juliana akageuka na kuisikia sauti ile inapotokea, kisura hakuweza kumfahamu zaidi ya kuambulia kumjua yule mhudumu wa mapokezi aliyekuwa amefuatana naye.

"Nilimwambia chumba hicho kina watu akasema anafahamiana nao," alijitetea yule mhudumu wa mapokezi akimuelezea yule kaka mbele ya Juliana.
"Dada hivi unajua utaratibu katika gesti hii?"
"Jamani si nilishawaambia kuwa nawafahamu?"

"Hata kama unawafahamu ndiyo uwachungulie tena wakiwa bafuni?"
"Haya tusubiri watoke muone kama hawanijui!" Aliongea Juliana kwa kujiamini lakini yule mkaka hakutaka kabisa kuaminiana naye, alichokifanya alimshika Juliana mkono na kumtoa katika kile chumba.
"Nimesema sitoki, hata mfanyaje mpaka wa huku bafuni wanione?"
Aliongea Juliana kwa kujiamini.

"Utatoka tu! Wee nani mpaka usitoke na kwanza hivi umelipia hata chumba humu ndani?"
"Sijalipia lakini sitoki!"
Juliana alitolewa kwa nguvu huku akiburutwa mpaka kwenye korido ya mule ndani ya gesti.

***
Wakati yote hayo yakiendelea si Bitungu wala mama Juliana aliyekuwa anajua kinachoendelea. Ndiyo kwanza mama Juliana alikubali kuendelea na kipindi cha pili baada ya kuchanganywa na mechi iliyopigwa kipindi cha kwanza japokuwa uwanja ulikuwa mbovu.
"Bitu mpenzi!"

"Niambie sweet!"
"Nasikia kuna makelele kweli nje na sauti ya dada kama analia kwa mbali?"
"Achana nao wanaweza wakawa watu wamefumaniana hao lakini kwa hapa, hapana! Sidhani kama kuna mambo hayo!"
"Nina wasiwasi Bitu!"

"Achana nao kwanza hayatuhusu tumekuja kula raha zetu hapa na siyo kufuatilia mambo ya watu."
Aliongea Bitungu huku akimvalisha mama Juliana ile khanga yake. Walikuwa tayari wameshatosheka kwa mechi kali mbili. Kitendo cha kutoka bafuni na kuelekea kitandani ile sauti iliyokuwa ikilia ndiyo kwanza ikazidi.

"Bitu, wacha nikaone anayelia mbona sauti kama ya mwanangu!"
"Mwanako? Afuate nini huku? Embu jifute tuagize chakula tupumzike kidogo urudi hayo mambo mengine waachie hukohuko hayatuhusu."
"Bitu kwangu miye nahisi kama yananihusu."



"Hayakuhusu sweet wangu embu nisikilize basi!"
"Bitu?"
"Nakusikia!"
"Kwa kuwa nakupenda! Nimeamua siendi tena!"
"Sawasawa, ndiyo maana nakupenda sweet wangu!"
Mama Juliana aliamua kutii amri mbele ya Bitungu japokuwa kelele alizokuwa akizisikia kwa mbali zilimaanisha. Alitoa mafuta yaliyokuwepo kwenye mkoba wake na kuanza kujipaka kisha akampaka na Bitungu.

"Haya mpenzi kwa sasa tupumzike."
"Lakini..."
"Lakini nini tena!"
"Hapana itabidi nirudi tu sasa hivi kwani kulala nitachelewa jamani na si unajua kuna mwanangu nimemuacha."

"Najua, wee tulale, nitatega mlio wa kutuamsha hapa kwenye simu baada ya nusu saa ndo utaondoka."
"Sawa mpenzi!"
Aliitikia mama Juliana huku akiachana na dera alilokuwa anataka kuvaa, aliendelea kuishikiza khanga yake kifuani kisha wakavutana na Bitungu hadi wakajikuta wamelala kitandani huku Bitungu akiwa juu yake na baada ya muda kidogo usingizi ukawapitia.
***
Bado Juliana alikuwa katika machungu makubwa, machungu ya kushuhudia mama yake akicheza mechi ya nguvu na Bitungu, tena mechi ya mchangani bila viatu. Bitungu aliyekuwa amemuamini lakini kumbe alikuwa akimficha siku zote.

Kwa muda huu Juliana alikuwa ameshindwa kabisa nguvu na wale wahudumu wa ile Gesti ya Tupendane. Alikuwa amejikalia zake nje ya ile gesti akitafakari huku pembeni yake akiwa na dereva bodaboda.

"Turudi tu nyumbani!" aliongea dereva bodaboda akimwambia Juliana.
"Hapana, siwezi ni bora uniache!"
"Nikuache?"
"Ndiyo niache hujaelewa nini?"
"Hasira zako hukohuko, haya nipe changu nirudi zangu?"
"Sh. Ngapi?"

"Unajifanya hujui bei tuliyokuwa tumeongea? Nipe elfu 10 zangu."
Juliana alikuwa ameshajipanga kwa kiasi hicho cha pesa. Pesa ambazo alikuwa akiwekeza nyumbani kwao kidogokidogo. Alifungua kipochi chake kidogo kilichokuwa na zaidi ya shilingi elfu 50 kisha akachomoa noti ya elfu 10 na kumpatia na kuondoka zake.

Macho, mwili viliashiria Juliana kukata tamaa ya kitu flani, hakuwa Juliana wa kawaida kutokana na kitu kilichomtokea. Alijiapiza na moyo wake asiondoke mpaka amshuhudie mama yake akitoka pale nje na Bitungu."Lazima Bitungu achague moja leo, kati yangu na mama nani anastahili kuwa naye!"
Alijikuta akijisemea mwenyewe Juliana huku akikazia macho eneo la mbele ya ile gesti kwa kila aliyekuwa akitoka ama kuingia.

Baada ya kukaa nje kwa zaidi ya nusu saa, giza lilianza kuomba njia. Juliana wala hakutetemeka kurudi kwani mtu aliyemhofia kama akichelewa kurudi alikuwa ni mama yake na siyo baba yake anayechelewaga kurudi nyumbani.

Hatimaye mama Juliana akatoka akiwa ameongozana na Bitungu. Bitungu aliyekuwa amevalia bukta na tisheti ya bluu huku mkono mmoja ukiwa kiunoni mwa mama Juliana.

Hasira kwa Juliana zilikuwa zaidi ya simba jike mwenye njaa kali. Alitamani kwenda kuwasambaratisha lakini moyo wake uligeuka na kuwa mzito kwa kuona kama mapenzi yake na Bitungu yanaweza kuelekea ukingoni. Macho yake yalibaki njia panda yakiwaangalia tu. Baada ya muda alishuhudia bajaj ikifika eneo hilo kisha mama Juliana akampiga busu Bitungu la kumuaga.
"Bitungu! Bitungu! Bitungu!"

Juliana uzalendo ulimshinda na kujikuta akilitaja jina la Bitungu kwa sauti ya juu. Ndo kwanza Bitungu akawa kama hajasikia zaidi ya kuiachia ile Bajaj ikiondoka na mama Juliana. Juliana alichokifanya ni kumsogelea Bitungu karibu.
http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
"Umefuata nini huku? Na nani kakwambia nipo eneo hili?"
"Unanigombeza au unaniambia?"
"Nakuuliza nani kakwambia nipo huku?"
"Uliniambia mwenyewe kwenye simu!"
"Kuwa?"

"Kuwa upo Bagamoyo kikazi!"
"Ndiyo nipo kikazi na hapa wafanyakazi wenzangu wengine wapo ndani!"
"Hata miye naona maana kuna mfanyakazi mwingine wa kike nimemuona umetoka naye na kumuangushia mabusu kisha akaondoka na bajaj!"
"Unasemaje Juliana?"

"Mfanyakazi mwenzenu wa kike nimemuona tena mnashikana hadi viuno?"
"Acha kunikosea mpenzi hebu kwanza twende tukakae kwanza pale tupate japo kinywaji!"
"Hapana nataka twende ndani!"
"Ndani kuna wafanyakazi wenzangu."

"Ndiyo vizuri ukawatambulishe kwangu au vibaya?" Juliana alikuwa akicheza na akili ya Bitungu kwa makusudi. Alikuwa ameshaujua mchezo mzima hadi chumba walichokuwa wakicheza mechi ya mchangani.
"Haya twende lakini..."

"Hakuna lakini Bitungu miye ndiye mpenzi wako wa pekee hao wengine si wafanyakazi wenzako?"
"Ndiyo!"
Kitendo cha Bitungu kuongozana na Juliana hadi chumbani, Juliana alimuwahi na kumsukuma hadi kitandani na kuanza kumshambulia kwa mabusu kadhaa. Wakiwa katika mahaba mazito mara simu ya Bitungu ikaita...



Kabla Bitungu hajaipokea ile simu, Juliana akawa ameiwahi na kuishika huku akitaka kubonyeza kitufe cha kupokelea.?Nooo! Nipe simu yangu mpenzi!?
?Hapana sikupi mpaka nijue anayekupigia.?

?Sasa sweet tumefikia huko! Najua tu watakuwa ni wafanyakazi wenzangu tu, nipe pliiz!?
?Hata kama!?
?Nipe basi!?

?Nimekwambia sitaki, embu kwanza.?
Juliana alikuwa wa kwanza kujua aliyekuwa akipiga simu ile ya Bitungu. Jina ambalo lilikuwa limeseviwa katika ile simu lilikuwa limemshtua vilivyo. Alichokifanya ni kuangalia tena ile namba mara mbilimbili na kugundua kuwa ni mama yake ndiye aliyekuwa akipiga, akaikata kisha akampa Bitungu.
?Shika lisimu lako!?

Harakaharaka Bitungu aliichukua na kuangalia aliyekuwa akipiga lakini kabla hajapokea ikawa tayari imeshakatika. Hasira zikamshika baada ya kugundua aliyepiga ni mama Juliana, akabaki akimtolea macho Juliana kwa hasira.
?Umeridhika sasa!?
?Kwa kipi hasa??

?Si umekata simu ya mfanyakazi mwenzangu!?
?Mfanyakazi mwenzako??
?Ndiyo! Unajua alichokuwa akitaka kuniambia??
?Ujue mpenzi sipendi kabisa nikuudhi na hata wewe uniudhi.?
?Kumbe unajua hilo! Kwa nini uniudhi??
?Nisamehe basi!?

?Haya nimekusamehe, tupumzike basi!?
?Bitu...?
?Niambie!?
?Mi sitaki kupumzika bwana! Natamani nikukumbatie muda wote tu!?
?Najua mpenzi lakini leo tulikuwa na kikao cha muda mrefu, hapa nilipo nimechoka sana mgongo kwa kuinama kuandika. Acha tupumzike kwanza na hata akili yangu haijakaa sawa...
?Hivi kweli Bitu unanipenda??
?Ndiyo kwani vipi??

?Hapana mtu unayempenda huwezi kumwambia hivi!?
?Lakini...
?Lakini nini??
Wakiwa katika maongezi huku Bitungu akiwa hana dalili ya kucheza mechi ya aina yoyote kutokana na uchovu aliokuwa ameupata baada ya kumaliza kucheza mechi ngumu ya mchangani na mama Juliana. Kila akijaribu kujiweka vizuri ndiyo kwanza alikuwa akichokozwa na Juliana.

inaendelea
Powered by Blogger.