KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Ni Shiida! Sehemu Ya Kumi na nne (14)

 LOVE STORY: ni shiidaI - 4
?Ujue Bitu... nahitajika kurudi nyumbani na hii yote nimekuja kwa ajili yako kwa nini unifanyie hivi... kwa nini uutese moyo wangu jamani, nielewe mpenzi...?
?Sweet, nakuomba kesho uje nitakuwa free kabisa!?
?Basi hata mara moja nirudi nyumbani inatosha!?
?Mara moja nini??

?Mara moja umuagize mwanajeshi wako afanye mashambulizi.?
Bitungu aliendelea kuwa mgumu hali iliyomfanya Juliana aendelee kuumia zaidi kila akikumbuka alivyokuwa akishuhudia mechi kati ya Bitungu na mama yake.

Mechi waliyokuwa wakiichezea mchangani tena wakiwa na jezi. Baada ya kusumbuana kwa muda, Bitu aliamua kumkubalia Juliana ambapo alimuweka sawa na kuanza kufanya mashambulizi ya kupima uwezo wake wa kulicheza gwaride kabla hajavua rasmi magwanda na kuingia vitani.
***
Usiku ulizidi kuingia. Hadi inafika saa mbili za usiku si mama Juliana wala Juliana waliokuwa wamefika. Siku hiyo baba Juliana alijuta kurudi mapema kwani tangu saa kumi na mbili za jioni alikuwa nyumbani akiwasubiri. Homa aliyokuwa akiisikia ilimfanya kuachana na pombe siku hiyo na kuwahi kurudi ambapo alikuta milango yote ya nyumbani kwake ikiwa imefungwa. Hatimaye mama Juliana akatokea na kumkuta mumewe akiwa amekaa kibarazani kwa hasira.

?Umetoka wapi sasa hivi??
?Baba Juliana ndiyo salam kweli hiyo??
?Sitaki salam, kunigandisha muda wote na simu umezima ndiyo nini??
?Simu imezima??
?Ndiyo! Umeamua kunizimia simu siyo??
?Hapana sijazima simu, siyo hii hapa iko on??
?Sipendi upumbavu mama Juliana, haya nifungulie mlango.?

?Kwani umefungwa? Nilimuacha Juliana, au atakuwa ndani amepitiwa na usingizi??
?Angekuwa amelala tangu saa kumi na mbili si angenifungulia, nimegonga mpaka nimechoka. Ujue msiniletee ujinga!?

?Hapana mume wangu, miye funguo zangu za akiba zote niliziacha nikijua nimemuacha Juliana na nilimwambia kuwa asitoke narudi naelekea kwenye vikoba.?

?Leo mtaniambia vizuri mlikuwa wapi, haiwezakani mnifanyie ujinga wa namna hii kwa kunigandisha, kumbe siku zote ninazochelewaga kurudi nyumbani mnajiachia namna hii siyo??
?Hapana mume wangu!?
?Hapana nini??

Mama Juliana alijitahidi kudanganya lakini ndiyo kwanza baba Juliana alizidisha ukali. Hakutaka kusikia lolote zaidi ya kufunguliwa kwanza mlango halafu aelezwe ukweli juu ya Juliana alipo. Woga ulishaanza kumshika huku akitetemeka mwili asijue afanye nini ili mlango ufunguke, akili ya haraka aliichukua simu yake na kutaka kutoka eneo lile.

?Embu ngoja niiulizie hapa jirani kwa mama Latifa,?
?Uulizie nini wakati kote nimeshaulizia wamesema hakuna ufunguo na mtu wa mwisho kuonwa akitoka alikuwa Juliana.?

Mama Juliana aliishiwa pozi, ujanja wote wa maneno ulikuwa umeshamwishia, alishindwa kujiongeza zaidi ya kuamua liwalo na liwe. Aliichukua simu yake na kuanza kumpigia Juliana kwa papara huku akiiweka loud spika ili wote wajue eneo alipo.


Mikono yake ilionyesha wazi kutetemeka hasa maeneo ya vidoleni, muda wote baba Juliana alikuwa pembeni yake akimuangalia tu. Simu iliita mpaka ikakata yenyewe, akajaribu zaidi ya mara mbili lakini bado haikupokelewa.

?Sasa atakuwa ameenda wapi Juliana huyu??
?Hayo maswali usiniulize mimi, ninachotaka kwanza mlango ufunguliwe kisha ndo mnijibu vizuri kwa nini mnaondoka tena na funguo zote!?
?Jamani baba Juliana! Si nilishakwambia funguo zangu zipo ndani!?
?Fungua sasa!?
?Nitafunguaje??

Baba Juliana bado alikuwa na hasira kali. Alichokifanya ni kujisogeza kwenye ukuta na kutaka kukaa kwa mara nyingine, kabla hajakaa wazo likamjia. Akajiongeza!
?Naenda kumuita baba Latifa!?
?Wa nini??

?Aje aubomoe tu huu mlango!?
?Halafu ukishabomolewa??
?Tunaingia, anaurudishia!?

?Jamani baba Juliana embu kuwa mvumilivu basi hata kidogo, Juliana kama ametoka si atakuja kuliko kuanza kumuita baba Latifa aje avunje.?
?Ndo nishasema sasa!?

Baba Juliana hakutaka kusikia lolote zaidi ya kunyanyuka na kuongoza moja kwa moja mpaka kwa baba Latifa ambapo alimkuta na baada ya dakika chache alirudi naye kwake akiwa na vifaa vyote vya kubomolea mlango.

?Fanya uwezavyo, uvunje tu tuweze kuingia halafu utaurudishia!?
?Haina shida bosi!?
?Hapana baba Latifa, Hapana usiuvunje!?
?Wee mwanamke! Embu muache baba Latifa auvunje huo mlango.?
?Baba Juliana kwa nini hutaki kunisikiliza mkeo!?

?Mimi si ndo baba Juliana, baba mwenye nyumba? Haya fundi vunja nimesema na kama pesa nakulipa mimi wala si huyu mwanamke??



ITAENDELEA

Powered by Blogger.