KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Ishirini (20). MWISHOO

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Katika maisha yangu nina kijitabia fulani cha kutotoka siku za mwisho wa wiki,isipokuwa jioni tena nikiwa na mke wangu ,Getruda. Huwa natoka katika matembezi mafupi na kurudi nyumbani.Juma pili hii ilikuwa ngumu kwangu.Kwanza mke wangu hakuwepo,usishangae nikimuita mke wangu japo sikufanikiwa kufanya tendo la ndoa.Ni mke wangu kwa sababu nimefunga ndoa kanisani.

Mawazo bado yalinizonga sana akilini,niliwaza safari ya ghafla ya mke wangu.Nilitamani sana nijue maendeleo ya wazazi wake huko mkuu Rombo.Kingine ni tatizo linaloniletea utata ndani ya ndoa yangu.Nilizidi kuwaza ,kwanini ugonjwa huo uwe kwangu tu.Kwanini usiwe kwa fulani?.Nilitamani kunywa bia lakini lakini nikaona si kutatua tatizo zaidi ya kuliongeza.

Nikiwa kwenye dimbi la mawazo,nilisikia simu ikiita,nilishituka sana.Kwa haraka nikaiendea simu ambayo niliiacha Varandani juu ya meza.Nilifikiri mambo mengi ,nikahisi aliyepiga simu alikuwa mke wangu akinipa habari za mama yake,nilitegemea kupata habari mbaya kutokana na maneno aliyoniacha nayo Getruda jana alipokurupuka akionekana wazi kuchanganywa na hali ya mama yake.Nilipofika nikaiokota simu upesi na kuipokea , “Hallo mume wangu.Umzima ?”

“Ndio.Vipi kuhusu hali ya mama.Anaendeleaje?”Nilimwuliza.

“Kidogo amepata ahueni.Kuna uvimbe gotini unamsumbua”

“Utakuja lini?”

“Aaa kesho jioni.Namsaidia kumuuguza hospitalini”

“Sawa.Nimebaki mwenyewe kama mkiwa”

“Usijali mpenzi.Upo nyumbani, na hutoki leo?”

“Ndio,nipo sitoki bila wewe.Kwanza najisikia vibaya kabisa sijui ni kwanini mpenzi”

“Pole sana mume wangu,bye”

Getruda akakata simu.

*********************



Kulikuwa na kundi la patao watu watano,aliyekuwa msemaji mkuu akiwa mzee Jophu.Pembeni aliketi Getruda na kushoto kwake mwanaume mmoja mwanye umbo kubwa,unaweza ukamfananisha na mcheza mweleka.Mikono yake minene iliyojaa na kujengeka misuli.Kushoto kwa mwanaume yule alikuwepo kijana mwingine,mrefu mwembamba lakini anasura ya kukatili.Ukimuona lazima ungemtambua kama ni muuaji.Huyu aliweka bastola kibindoni,bastola aina ya Revolver.Aliyebaki alionekana mdogo sana,ukitadhimini umri wake ni miaka kumi na tano,alionekana alikulia mitaani.Huyu ni kibaka mzoefu ,achilia mbali bangi ,sigara na dawa za kulevya, kuvuta petroli na gundi ya viatu kwake si tatizo.Mtoto huyu walimtumia sana katika matukio ya ujambazi na upelelezi wa wapi kuna pesa ,wapi tukaibe leo.

Walicheka muda mfupi tu baada ya Getruda kukata simu, “Anasemaje huyo maiti”Mzee Jophu aliuliza akiwa anamtizama Getruda kwa udadisi.

“Anasema leo yupo nyumbani hatoki,ni jambo ambalo liko wazi bila mimi habandui mguu wake.Hivyo kazi yake imeisha”

“Patamu sana hapo.Naomba vijana wangu waingie kazini.Kama nilivyo waelekeza na mfanye kwa tahadhari sana msije kubainika kama ninyi ndio mlioua.Mmenisikia?”

“Mzee usitufundishe hii ndio kazi yetu kama kazi nyingine.Tumeua sana na tutaendelea kuua.Pesa ya kazi mbele”Alisema jambazi mmoja nene lenye kifua kama pipa,lilitambulika kwa jina moja tu ‘Man Kaugo’Man Kaugo ana kasumba moja hataki kufundisha kazi ya uuaji,nasema anaielewa vema na ujuzi huo kwake ume komaa.

“Naona mchukue lita arobaini za petroli.Mzungushie nyumba yake yote na muitie kiberiti”

“Eeee!kuna vitu vyangu vya muhimu.Kwanini msimuue bilakuchoma nyumba”

“Vitu vyako nitakulipa.Tatizo ni nini?”

“Nyumba yamgu.Nilitaka mumuue nibaki na nyumba”

“Nyumba nitakununulia njiro”

“Haya, usinidanganye mpenzi”

“Sikudanganyi.Mimi na wewe kwani wa tani?”

“Hapana”

“Sasa kumbe…” akatulia kidogo kisha akasema, “Nafikiri tumemaliza makomando wangu”

“Pesa zetu bado.”

“Kiasi gani ?”

“Milioni tatu kwa kichwa kimoja”

“Ok,subirini kidogo nakuja.”



Mzee jophu alitia gari moto na kuondoka zake.alielekea benki ambako alichukua milioni tano na kuzihifadhi.Hakuchelewa alirudi. “Kamata milioni tatu hizi.Naomba mharakishe tafadhali”

“Sawa mzee.Utasikia mwenyewe mambo yakijibu”Wale vijana waliondoka zao.

Nilisikia kama watu wakiongea nje ya jengo langu,kila nilipojaribu kutega sikio kwa makini,nilishindwa kun’gamua mazungumzo yao.Nilitunguza redio kabisa ,japo nilikuwa macho lakini nilihisi bado kiko usingizini,watu hao walinikaribia dirishani ,kwambali nikasikia mmoja wapo akisema “Hili ndilo dirisha lake”

Mwingine akasema “Basi hapa tumwage petroli nyingi iliafe haraka”kilikuwa kitendo cha haraka nilisikia petroli ikimwagwa dirishani,nilikurupuka na kushituka ,nilipofungua macho kumbe nilikuwa nikiota njozi mabaya kabisa.Kukurupuka kwangu hata mke wangu Suzan ambaye tulibahatika kupata mtoto wa kiume aitwaye Samji ,alinisikia nikipiga kelele, “Nakufaaaaa”

“Nini mume wangu?”Suzan, mke wangu aliniuliza akiwa na masalio ya usingizi.Nilihisi mapigo ya moyo yakinienda mbio utadhani nilikimbia umbali mrefu bila kupumzika.

“Baba samji,ni nini mbona umepiga kelele kiasi hicho?”

“Ndoa yangu inanitesa”Niliropoka nikipikicha macho, sikuamini yale niliyoyaona nikiwa usingizini.

“Ndoa yako inakutesa kivipi?”

“Nafikiri nilikuwa nikiota ndoto ya mateso kabisa”

“Ndoto?.Nilikusikia hata wakati mwingine ukilia ukiwa usingizini.Nilikutingisha lakini huku shituika, ulikuwa ukisema Getruda Getruda .Getruda ninani?”Nilitulia kidogo nikajaribu kumkumbuka, “Getruda ni huyo mwanamke niliyemuoa, akawa ananitesa”

“Usinidanganye mume wangu.Madhambi unayofanya na mahawara wako ,ndio unayaota usiku?”

“Basi nisamehe mke wangu,ni ndoto tu.Sina mtu nimpendaye zaidi yako.Sijui njozi ya ajabu namna hii imetokea wapi.Yote niliyoota hakuna hata kimoja kilichowahi kunitokea”

Ilikuwa usiku ,majira ya saa kumi na moja.Suzan, mke wangu alinisamehe na tukaanza kusali.


MWISHO
Powered by Blogger.