KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Nane (8)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
Wiki tatu zilitimia na siku ile ya harusi iliwadia. Kila mtu aliisubiri kwa hamu sana siku hiyo hasa wazazi wangu kwani walijisikia furaha kwa mtoto wao wa kiume pekee kufunga pingu za maisha. Nadhani moyoni mwao walijisemea, sasa ule wakati wa kuwaona wajukuu toka kwa mtoto wetu Sweedy umewadia. Mzee Jophu ndiye alikuwa mtu wa kwanza kwa watu walionichangia mchango mkubwa katika kuifanikisha harusi yangu. Sherehe ilipendeza sana, watu walikula na kunywa hadi wakasaza. Namshukuru Mungu sikupata lawama yoyote ya kuhusu sherehe yangu.

Getruda ambaye ndiye ubavu wangu sasa aligubikwa na furaha isiyo kifani. Sherehe iliyopendeza kwa shamrashamra na vifijo, DJ alitumbuiza kwa muziki wa taratibu wa wapendanao hasa kibao kilichopigwa na mwanamuziki Bob rudala nadhani msomaji unaupatapata ule wimbo vilivyo . Utajisikia vipi ukipigwa siku ya harusi yako? “NIMEKUCHAGUA WEWE” nakumbuka baadhi ya maneno yake, “Nimekuchagua wewe uwe wangu, wangu wa maisha wa kufa na kuzikana”msomaji sitaki nikumalizie uhondo tafuta wako na wewe awe wa maisha ili ujiepushe na mengi hasa janga la Ukimwi. MC au Msema chochote watu wa mjini wanavyoita alikuwa anaitwa MR.Kicheche ni kicheche kweli si mchezo ukumbi haukuruhusiwa kukaa kimya siku hiyo watu wote walikuwa wakicheka na kutabasamu kwa wale wasio na bandama. Kwa ufupi sherehe ilipendaza mno, hatukuwa matajiri lakini watu wailiridhika na kila idara ya sherehe.

Sherehe ilipoisha, tulichukuliwa na gari maalumu siku hiyo kwa bwana na bibi harusi na tukaelekea kwenye hotel moja iliyoitwa NGORONGORO HOTEL kujipumzisha. Tulipofika tulikwisha andaliwa kila kitu, chumba kilinukia harufu nzuri za manukato, choo na bafu ndani kwa ndani ilipendeza kwa kweli. Washenga waliondoka tukabaki mimi na mke wangu Getruda Kimario.

Nilikuwa na shauku kubwa ya kukabiliana na binti ambaye alikuwa kigoli, ambaye hakuwahi kuguswa, nilitamani kupata ukweli wa maneno ya baba aliyenieleza kuwa mke niliyeoa alikuwa bikira, na mimi nilitamani kumtoa mwenyewe yaani kama ni gari lilikuwa jipya ‘New model’ na sio mtumba.
Tuliongozana bibi mbele bwana nyuma, wote tukiwa tumefunga taulo tuliingia bafuni na kuanza kuoga. Kweli uzuri wa mke wangu niliufananisha na lulu au tunda Apple. Alikuwa na umbo dogo lenye figa, ambalo lilinifanya nimtamani zaidi na zaidi. Si kifuani, usoni na umbo lote lilinivutia sana. Nilimuogesha nae aliniogesha, tulipomaliza tulijifuta na taulo na kuelekea chumbani.

Tulijitupa kitandani, “Samahani mpenzi nikumbatie, nahisi baridi…nahitaji…..” Ilikuwa sauti ya Getruda iliyojaa mahaba na iliyonisisimua mwili na kuhisi joto .
“Usihofu kila kitu kitakuwa shwari, nitakupa kila kitu unachokitaka” nilimjibu kwa sauti nzito iliyomuingiza kwenye ulimwengu wa mahaba.
“Lakini mpenzi unajua nakupenda sana” Getruda aliongea macho ya udadisi yakiwa yametuwa usoni mwangu.

“Naamini unanipenda mke wangu ndio maana ukaamua tuoane, lakini nahisi mimi ndiye nimezimika kwako zaidi” nilimweleza na hapo hapo tulikumbatiana na mabusu motomoto yalishamiri, si mashavuni, mdomoni na kwenye paji la uso kote tulipeana mabusu ya upendo.

Niliyasikia mapigo ya moyo wake yakienda kwa kasi jasho jepesi lilimchuruzika taratibu nilishindwa kuelewa kwani AC au ‘kipupwe’Kiyoyozi kwa jina letu la kiswahili kilikuwa kinafanya kazi yake kama kawaida. Kila nilipomshika kwenye kona za mapenzi nilimsikia akizizima kwa sauti za mahaba, si kwikwi wala kuweweseka zote zilimburudisha. Niliamua kutulia kidogo baada ya kuona mambo yote nilikuwa namfanyia uume wangu hausisimka hata kidogo, tofauti na siku za nyuma busu moja kila kitu kimesisimka, leo mambo yote sikuona hata dalili.
“Oooh.!!! Sweedy unajua mimi sijawahi kuguswa kabisa!”
“Eti!, samahani sijakuelewa mke wangu”
“ Sijawahi kufanya mapenzi toka kuzaliwa. Naomba unifundishe” sauti nyororo na ya simanzi ya Getruda ilinifanya nilie mwenyewe, sikuwa na nguvu za kiume, bali nilitamana kumkabili mke wangu nilishindwa kujua Ugonjwa wa kupooza kwa uume wangu ulitoka wapi na nitamuambia nini mke wangu, na je atanielewa na wakati nishamchezea kila sehemu, nilizidi kulia sikuwa na la kufanya.
“Unalia nini tena mume wangu?” Getruda aliniuliza akiwa kalala chali, kama mgonjwa aliye mahututi . Mweupe mwili wake ulipendeza na kuzidi kung’ara kila nilipomtazama usiku ule, kwa ufupi alikamilika kila idara,nilitamani nimrukie lakini jogoo wangu hakutaka kuwika kabisa. Nilidanganya “Mke wangu nimeshikwa na kichomi cha tumbo sijui ni hiyo AC “kipupwe” niliongea kidhaifu nikiwa nimeshika tumbo, machozi yakiendelea kuchuruzika taratibu, niliamini kwa maneno ya kusema “Naumwa” Getruda angeridhika na kunionea huruma, aliniangalia kwa huruma na kusema
“Basi mume wangu tuzime usije ukapata matatizo zaidi”. Nikaona duh! Acha nizidi kujitetea “Labda upunguze kidogo”Nilisema nikiwa nimekunja sura na kushika maeneo ya tumbo.
“Pole mpenzi” mke wangu alisema kwa sauti ya utulivu.
“Usiku huu tutapata wapi dawa?. Jikaze usilie”Mke wangu alinionea huruma.
“Usijali mama watoto.Huwa natokewa na tatizo la kichomi ninapofikia hatua ya kufanya tendo la ndoa”
“Kwa hiyo utafanya je?”
“Daktari aliniambia tatizo hili litaisha baada ya kuzoea mwanamke”
“Mwanamke gani, mbona sikuelewi?”

“Wewe, Usijali tatizo hili litaisha”Nilizidi kumpa motisha mke wangu.Lakini moyoni bado wasiwasi ulitanda kuhusu jambo hili geni kabisa mwilini mwangu.
Maneno hayo ndio yaliyomfanya Getruda, mke wangu ainamishe kichwa magotini mwangu kama mtu aliyekuwa akisujudu. Sikujua aliwaza nini akilini mwake, lakini nikahisi yote yalikuwa juu ya matatizo niliyonayo.Muda wa dakika takribani tano nilihisi kitu kama maji maji angali yenye uvuguvu yakidondoka gotini kwa tone moja na moja.Matone hayo nilihisi ni machozi ,nikaamua kuinua uso wake kutizama kwamba ni nini hasa.Kila nilipojaribu kumuinua alikaza shingo.Wazo ambalo nilihisi kwamba alikuwa akilia likajidhatiti akilini na kuhisi sikukosea.Pia nilijaribu kwa mara nyingine kumuinua uso wake, safari hii akanisemesha akionekana kukasirika.
“Mume wangu umeamua kunitesa angali unajua unamatatizo.

Inaendeleah
Powered by Blogger.