KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Shida Sehemu Ya Tatu (3)

Hadithi nzuri ya kusisimua ya shida
MTUNZI JR. BAITA -0755 957515
Asubuhi ya siku iliyofata ilimkuta Shida katikati ya mji wa Dodoma, akaelekea mtaa wa Uwanja wa Ndege na kuchukua chumba katika Hotel moja ya kawaida sana, akajipumzisha, akaanza kuwaza namna atakavyoikamilisha kazi ya kulipa kisasi kwa wote waliomfanyia maisha yake kuwa ya Shida!

Alilala mpaka mchana na kuchukua tax na kuelekea moja kwa moja Benki na kutoa kiasi kikubwa sana cha pesa ambacho aliamin kitaweza kumsaidia kuikamilisha kazi yake

Baada ya hapo akarudi hotelini

"Inabidi kabla ya kuua niwe namfahamisha mchungaji ni nani nayeenda kumuua na kwa nini?" aliwaza

Akachukua simu yake na kubinyeza namba za mchungaji, simu ikaita.

MCHUNGAJI : haloo..... Nani anaongea??

SHIDA . Ni mimi Shida mchungaji

MCHUNGAJI : ooooh! Shida?...... Uko wapi mama?

SHIDA : siwezi kukwambia ila nipo kwenye mkakati wangu, sasa naelekea kwenye mauaji ya mtu wa kwanza

MCHUNGAJI : haaaa! Ni nani huyo?

SHIDA : naelekea kumuua baba yangu mzazi! Baadae ntaenda kumuua baba yangu mlezi!

MCHUNGAJI : haaa!!!!

MCHUNGAJI : naomba kitu kimoja binti yangu?

SHIDA : omba mchungaji, ilimradi kisizuie kazi yangu.

MCHUNGAJI : sawa, basi naomba kabla hujaenda kutekeleza kusudio lako uniambie walichokufanyia watu hao, kwa sababu tangu nimezaliwa sijawahi kusikia mtu anamuua baba yake mzazi na pia mlezi, walikufanyia nini mamangu?

SHIDA : unataka kujua?

MCHUNGAJI : ndio nahitaji kujua,niambie tafadhali!

SHIDA : haina shida nisikilize kwa makin, matatizo yalianzia kwa mama yangu aitwaye Amina!!



Shida anasimulia

MIAKA ISHIRINI NA SITA ILIYOPITA



Amina mtoto wa kigogo aliyezaliwa huko Chamwino mkoan Dodoma aliingia Dodoma mjini kwa minajili ya kutafuta kazi,hiyo ni baada ya kumaliza kidato cha nne huko kijijini kwao

Aliamin badala ya kuishi pale kijijini akihangaika na kilimo ni bora aende mjini akatafute kibarua kidogo cha kumwingizia kipato aweze kuwasaidia wadogo zake waendelee na masomo na pia aweze kujikimu na yeye.

Alifikia kwa mjomba wake anayeishi Area C ambaye kidogo alikuwa na ka uwezo kutokana na kumiliki stationary maeneo ya karibu na Chuo kikuu cha Mtakatifu John!

Amina alianza kufanya kazi katika Stationary hiyo ya mjomba wake huku akilipwa pesa kidogo ambazo zilimuwezesha kujikimu na kumsaidia mdogo wake aliyekuwa kaingia kidato cha kwanza kule kijijini kwao.

Baada ya muda wa miezi mitano Amina akawa na uwezo wa kupanga chumba na kujitegemea mwenyewe

Kazini kwake alikuwa akiwahudumia wanachuo wa chuo cha Mtakatifu John

Kila binadamu ana hisia hali iliyomsababisha Amina ajikute katika mazoea na kijana mmoja kwa jina la Filbet kutoka chuo hicho

"Amina, viip leo nikikutoa dinner?" aliuliza Folbert

"Hahahahaha! Haya bana ila isiwe usiku sana " akajibu Amina!

Jioni ilipofika Filbet alimfata Amina na wakaenda Hotel iliyotulia na kupata chakula cha usiku

"Unayaonaje mazingira haya? Na chakula kwa ujumla?" aliuliza Filbet

"Mazingira yako poa na chakula ni kitamu sana, ila nimepapenda sana, ahsante Fil kwanini umeamua kunileta hapa?" akauliza

"Unataka kujua Amina?" akauliza Fil

"Yes, nataka best angu" akajibu

"Amina, tangu nilipokuona pale kazini kwenu nilivutiwa sana na wewe, nilihisi moyo wangu ukipiga paaaa! Pale pale nikahisi wewe ndiye mke wa maisha yangu, nakupenda, nakupenda kutoka ndani ya moyo wangu naomba ukubali kuwa wangu tafadhali" akamaliza mashairi yake Fil

"Mmmmh! Unanidanganya Fil, na chuo huwaoni? Mbona kuna warembo balaa? Oa hao?" akauliza

"Amina sio kila mwanamke anafaa kuwa mke wa mtu, wengine ni wa kupita tu na wewe ndiye unafaa kuwa wangu wa maisha nakuomba tafadhali" akaomba Filbet

"Mmmmh! Nipe nafsi ya kufikilia tafadhali" akajibu Amina

Walikula na wakanywa baadae wakatoka na Filbet akampeleka mpaka nyumbani kwake kisha akarudi hostel

*************

Baada ya miezi mitatu uhusiano kati ya Filbet na Amina ulikuwa mkubwa sana, walipendana kwa dhati na hakuna aliyekuwa hajui hilo

"Nakupenda sana Amina,sitajuta kukupenda na wewe hutajuta,wewe ni mke wangu " aliongea Filbet

"Nakupenda pia Filbet, tena sana, wewe ndiye mwanamme wa maisha yangu, ntakupenda milele" akajibu Amina.

Mapenzi kabla ya wakati ni dhambi kwa mwenyezi Mungu ila binadamu ila wengi wetu tumekuwa hatutambui hilo. Na siku zote dhambi inazaa,

Baada ya mapenzi moto moto kati ya Filbet na Amina mwisho matokeo yakaonekana

"Baby samahani kwa hili, sijielewi! Mwezi huu nimepitisha siku zangu na mara kwa mara sijisikii kula chakula, sijui nina nini mimi?" akaongea Amina

"Acha msikhara wewe, una mimba?" akajibu Filbet

"Sijui mme wangu mtarajiwa, labda ila sina uhakika" akaongea Amina

"Mmmmmmmmh! Makubwa haya sasa" akaongea taratibu Filbet

Filbert alishtuka kutokana na kile alichokisikia kutoka kwa Amina, hakutarajia na pia hakuwa tayali kubeba majukumu ya ubaba kwa wakati huo

"Baby, naomba kujua uko tayari kuwa mama kwa sasa? Au umejiandaa kuwa mzazi kwa sasa?" akamuuliza.

Amina alifikilia sana kabla ya kujibu swali hilo, alishaona mwenzie alivyombadilikia hivyo alijua lile swali ni la mtego

"Sijajua unauliza ukiwa na maana gani?" akajibu

“Sijaeleweka kivipi?, nimeuliza uko tayari kuzaa kwa sasa?" akauliza tena Fil

"Umri wangu hauniruhusu kuwa mzazi ila pia siwezi kuua kiumbe kisicho na hatia" alijibu kwa kujiamin

Filbert aliinama chini na kufikiria kwa muda kabla ya kuamua aongee nini.

"Unanipenda kiasi gani? " akauliza Fil

"Nakupenda zaidi ya kitu chochote kile" akajibu kwa kujiamini.

"Basi kama unanipenda na unataka nije kuwa mmeo, lazima utoe mimba hiyo" akaongea Filbet kwa kujiamin

"Heee! We mwanamme una wazimu? Hata hatujapima kujua kama kweli nina ujauzito ushaanza kuleta habari za kutoa, umerogwa?" akaongea kwa hasira sana Amina

Yakaibuka malumbano makubwa sana ambayo ilibidi kila mmoja aondoke kivyake kama hawakuja pamoja pale.

Asubuhi ya siku iliyofata Amina kabla hajaamka Filbet alifika pale na kuanza kumbembeleza kwenda kupima

Wakaondoka na kwenda kupima na kwa bahati mbaya majibu yalipotoka yakaonesha kuwa ni kweli Amina ana ujauzito wa wiki saba yaani mwezi mmoja na wiki mbili na nusu.

Njiani hakuna aliyemuongelesha mwenzake chochote

Kila mmoja alikuwa akiwaza cha kufanya ili kukabiliana na tatizo lililojitokeza

Huku Filbet kwenye akili yake akiwaza namna ya kumrubuni Amina aitoe ile mimba

Upande wa Amina yeye alikuwa akiwaza namna ya kukabilian na Filbet ambaye ameshaonesha nia ya kutaka ile mimba itolewe

"Mwanangu, katika maisha yako yote usije kujaribu kufanya kosa la kutoa mimba, nimekutaarifu mapema ili huko mjini uendako uwe makini, Babu yake baba yako alilaani hicho kitendo na pia ni dhambi kwa Mungu, yeyote aliyejaribu kufanya hivyo alifariki, nafikiri ulishasikia kilichompata Shangazi yako yulee marehemu, alijaribu kutoa akafa" maneno mazito kutoka kwa mama yake yalijirudia kwenye akili yake kila mara.

Walipofika chumba anachoishi walikaa kidogo kisha Filbet akatoka na kwenda kumnunulia Chipsi akamletea akala na kisha akaaga na kuondoka akiahidi kurudi tena!

Jioni ya siku hiyo Filbet alirudi na wakati huu alikuwa mbogo sana, alitaka iwe isiwe Amina lazima atoe ule ujauzito

"Narudia kukwambia kuwa kukupenda isiwe sababu ya kuhatarisha maisha yangu, Babu yetu alishalaani hicho kitendo, nikitoa lazima nitakufa na siko tayali" alilalama Amina.

"Hayo ni maneno tu, huyo babu yako mwenyewe alishakufa sasa maneno yake ndiyo tuyaogope, na kumbuka hii ni dunia iliyoendelea hatuwezi kuendelea kukumbatia mila na imani za kipuuzi kama hizo, hii mimba lazima itolewe" akalazimisha Folbet

Amina alibaki analia sana.

"Ngoja nikuulize, hivi Amina unanipenda kwa dhati na uko tayali kwa lolote kwa ajili yangu?" akauliza

"Nakupenda tena zaidi ya sana, na niko tayari kwa lolote kwa ajili yako ila si kwa ajili ya uhai wangu" akajibu

Jibu hilo lilimuudhi sana Filbet na kwa sababu ya hasira akajikuta akianza kumpiga Amina,

Alimpiga sana tena sana mpaka amina akawa anavuja damu

"Amina umeumia? Nisamehe mpenzi ni hasira tu jaman" aliongea Fil

"Fil kweli unataka kuniua, kaninunulie dawa hali yangu sio nzuri ndipo unipeleke, hospital" akajibu

Hii ndiyo nafasi pekee aliyoisubilia Filbet akambembeleza sana Amina na kisha akatoka kwenda kununua dawa, akiwa njiani akapiga simu

"Oyaaa..... Tayari....ninunue dawa gani?......poa" akakata simu na kwenda kununua dawa anazozijua

Aliporudi akampa Amina dawa ameze

Baada ya kumeza dakika tano baadae tumbo likaanza kumuuma sana!

"Te teh teh teh! Ulijiona mjanja Amina sasa mimba inatoka" aliongea kwa kejeli!

Maumivu yalizidi kiuwa makubwa sana kwa Amina,alijalibu kumbembeleza sana Filbet ampeleke hospitali ila Fil akakataa

"Ngoja nikwambie Amina, ukweli mimi siwezi baba sasa hivi, na siyo hivyo tu, nimetoka familia tajiri sana ambayo haiwezi kuniruhusu kuoa msichana maskini kama wewe, pia kiwango chetu cha elimu ni tofauti, baba yangu alishaniambia nisioe familia maskini kwa sababu sitakuwa nimeoa mke peke yake bali na matatizo ya ukoo mzima, kwa sababu hiyo sitaendelea, nitabaki kuwa nazalisha kwa ajili ya ukoo wenu huo wa kimaskini, nimekupiga makusudi ili uniombe dawa na nimekuletea dawa ya kutoa mimba, we tulia tu mpaka mimba itoke" alimaliza Filbet



Amina aliendelea kulia huku damu zikianza kumtoka ukeni kwake,hali iliyoongeza maumivu makali sana tumboni kwake.

Baada ya kupita saa nzima aliamini kuwa tayali mimba itakuwa imetoka,Filbet alimchukua moja kwa moja mpaka kwa daktari wake ambayae huwa anamsaidia katika shuguli zake hizo za kutoa mabinti mimba!

Alipomfikisha walimuingiza kwenye chumba cha kazi.

"Nilifanya kama ulivyoniagiza,na yametoka mabonge mengi sana,na uhakika itakuwa imetoka" Filbet alimwambia Dokta James

"Kama umeyaona basi tayari itakuwa imetoka, cha msingi tumuweke hapa siku chache mpaka apone kisha utaondoka naye" akajibu Dokta James

Filbet alimuacha pale Amina akipewa matibabu na kusafishwa!

Matibabu yake hayakughalimu pesa nyingi na siku chache baadae alipewa ruhusa ya kumchukua Amina kutoka pale.

Filbet alimchukua amina kwenye gari lake na moja kwa moja akampeleka kwenye nyumba yake ya siri

"Hujapona vizuri, itabidi ukae hapa kwa siku chache mpaka utakapokuwa sawa ndipo nitakuruhusu urudi kwako" alimwambia Amina

Amina alikaa katika nyumba ile ambayo hakuruhusiwa kutoka nje hata mara moja kwa muda wa siku tatu akiwa analetewa chakula na Filbet

"Nafikili utakuwa umepona, mimi nina hamu ya kufanya mapenzi bana" akaongea

"Fil sijapona vizuri, lakin nakumbuka ulinambia huwezi kuwa na mimi hivyo naomba uniache nirudi kwangu niendelee na maisha yangu" akajibu Amina

"Sikukwambia sikutaki, nilichosema ni kuwa siwezi kukuoa kutokana na wewe kuwa maskin, wewe ni mpenzi wangu,nimetumia pesa yangu kwako haiwezi kupotea bure" akaongea kwa kujiamin.

Amina alipotaka kuleta ubishi Filbert akatumia nguvu na kumwingilia kimwili

Amina aliumia sana wakati wa tendo lenyewe ila hakuwa na jinsi kwani Filbet alitimiza alichokitaka

Baada ya kumaliza kitendo cha kumbaka Amina,

Amina alianza kutokwa na damu ukeni, alishangaaa sana na si yeye peke yake bali hata Filbet naye akashangaa

Ikambidi ampigie simu daktari wake na kumweleza kinachoendelea,daktari akashauli ampeleke pale aone kinachoendelea.

Walipofika pale alifanyiwa vipimo na uchunguzi kidogo kisha akaruhusiwa kurudi naye nyumbani huku daktari akimwambia kuwa ni damu ya mzunguko wa mwezi ndiyo inayotoka, kosa moja walilofanya ni kutokupima kama mimba ilitoka kweli

Maisha yalianza kubadilika kwa Amina pale aliporudi nyumbani aliendelea kutokwa na damu kwa siku kadhaaa

Kitendo cha kutokwa na damu kilimkela sana Filbet na ndipo alianza kuwa mnyama sana kwake

"Amina mimi nina hamu ya kufanya mapenzi, sasa tufanyeje?” akauliza

"Fil lakini si unaona hali yangu jaman, sa tutafanyaje?" akajibu Amina

"Itabidi unipe nyuma bwana" akajibu kwa kujiamin Fil

INAENDELEA

Powered by Blogger.