KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Shida Sehemu Ya Nne (4)

Hadithi nzuri ya kusisimua ya shida
MTUNZI JR. BAITA -0755 957515
Mshangao mkubwa ukamkumba Amina, hakuwahi kutarajia kitu kama hicho katika maisha yake,kwanza alipokuwa akisikia alidhani watu wanatunga,ila sasa yeye ndiye aliyetakiwa kufanya hivyo.

Pamoja na jitihada kubwa za kupinga alizoonesha ila hakuweza kupambana na Filbet,alifanikisha azma yake kwa binti huyu

Mchezo haukuhishia siku hiyo uliendelea kila siku huku akinyimwa ruhusa ya kutoka ndani na damu nayo iliendelea kutoka!

Cha ajabu baada ya miezi mitatu, siku moja Filbet alimkuta Amina akiwa anaoga pale ndani, alishangazwa na alichokiona.

"Amina, mbona tumbo lako ni kubwa? Ina maana mimba haikutoka?" aliuliza kwa mshangao!!!!!

Filbet alihamaki sana kwa kile alichokishuhudia kwani hakutegemea kukiona tena! Aliamin ile mimba ilitoka kwani alithibitishiwa na daktari kuwa ilitoka sasa anashangaa kuiona tena!

"Ina maana bado una mimba Amina?" akauliza

"Mimi sijui ila hata mimi najishangaa kwani tumbo linazidi kuwa kubwa na kuwa gumu" akajibu Amina

Filbet alizubaa kwa muda akimtazama Amina, alishindwa afanye nini, kwani tayali alikuwa na mchumba aliyekuwa nje ya nchi kimasomo na hakutaka kutia doa uchumba ule kwa sababu ya huyu binti,alitafakari mwishowe akapata wazo

"Amina naomba ukojoe mkojo wako unipatie tafadhali" akaomba

Amina alifanya kama alivyoagizwa na Filbet kisha akamkabidhi,na Yeye akaondoka nao moja kwa moja mpaka kwa yule daktari wake na kumweleza mkasa mzima ulivyo

"Sasa dokta,inakuwaje hili liwe hivi?" akauliza

"Ningekuomba uwe mtulivu mpaka niupime huu mkojo" akajibu Dokta

Dokta alichukua ule mkojo na kwenda moja kwa moja mpaka maabara na kuupima, baada ya muda mfupi alirudi na majibu

"Dah! Kijana, siamini ninachokiona hapa, huyu binti ile mimba haikutoka, na sasa hali si shwari" akasema Dokta

"Inawezekana vip dokta? Na hali mbaya kivip?" akajibu Fil

"Unajua kwa kumbukumbu zangu nahisi kuna kosa moja tulifanya, hatukumpima kipindi kile ili kuhakikisha kuwa mimba ametoka, na sasa hali iliyopo ni mbaya, mimba ina miezi mitano, kumbuka kipindi kile ilikuwa na wiki saba na imepita miezi mitatu na kwangu mimi nisikudanganye siwezi kujalibu mchezo wa kutoa mimba kubwa hivyo" akahitimisha dokta



Walibishana kwa muda mrefu bila maelewano juu ya swala la kufanya juu ya ule ujauzito, Filibet alilazimisha utolewe huku dokta akimsihi asijalibu kufanya hivyo kwani ni hatari kubwa



"Sikia dokta siko tayali kumpoteza Lily wangu kisa huyu demu fala,9iko tayali kwa lolote,nakupamuda mfupi sana nitakupa majibu" akajibu kwa jeuri kisha akaondoka

Filbet aliondoka pale akiwa na hasira kubwa sana alijua alichotaka kukifanya hivyo alipofika nyumbani hakumwambia Amina kilichotokea huko, Alichokifanya ni kuanzisha ugomvi usio na sababu.

"Hivi wewe ni mwanamke wa aina gan? Huna kazi unafanya hapa kazi kukaa tuu na kutoka dami?" akaanzisha maongezi ya kishari shari

Amina hakujua kinachotokea hivyo alijibu kiungwana tu na hapo ndipo alipopataka Filbet

"Unanijib? Nani kakwambia mwanamke ana haki ya kumjibu mmewe?"

Na pale pale akaanza kumshushia Amina kipigo kikali sana, alikuwa akijua anachokifanya hivyo hata upigaji wake ulienda sehemu husika

Tumbo, hapo ndipo lilipokuwa lengo lake halisi,alimpiga Amina ngumi na mateke mengi sana tumboni mpaka Amina akaanza kutokwa na damu sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kipigo kilizidi mpaka Amina akapoteza fahamu huku damu zikizidi kumtoka ukeni kwa wingi, Filbet alipohakikisha kuwa kazi aliyofanya ni nzuri na italeta majibu anayoyataka alitoka nje na kufunga mlango

"Hakikisha huyo malaya hatoki humo ndani mpaka nikirudi" alimuamrisha Alex mlinzi wake wa getini

Sio kila mwanamme ana roho mbaya na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwa Alex mlinzi wa Filbet

Tangu yule mwanamke aletwe pale alijua yatakayomkuta ni makubwa kwani haikuwa mara ya kwanza kwa Filbet kuleta mwanamke pale ndani na kumtesa kisha kumtelekeza

Kwa huyu hali ikawa tofauti alionekana binti mdogo sana na mwenye shida kubwa, moyo wa huruma ukamwingia, akapanga kumsaidia, kila alipojaribu alishindwa kwani funguo zilifichwa na bosi wake,

Hapo ndipo alipoanza kumchunguza bosi wake ili ajue pale funguo zinapofichwa, alifuatilia sana na siku ya tukio la Amina kupigwa sana ndipo akaona zikiwa zinafichwa

Filbet alipoondoka pale ndani Alex akaenda na kuchukua zile funguo na kuingia ndani

Alimkuta Amina katika hali mbaya sana,alipoweka mkono wake kwenye kifua chake akakuta mapigo ya moyo yamesimama!!



Alex alihangaika kumpulizia pumzi kutoka katika mdomo wake Amina,na kwa muda mtefu hatimaye alisikia mapigo yake ya moyo yakipiga kwa mbali,alichokifanya ni kumeba mzima mzima na kuondoka naye katika mazingira yale,

Alipofika nje alitafuta tax na kupanda moja kwa moja akaelekea mtaa aliokuwa kapanga wa airport

Alipofika alimuingiza ndani na kuchukua maji akayapasha na kuanza kumkanda sehemu mbali mbali za mwili wake na alipoona vidonda vina angalau alienda kwenye duka la dawa za binadamu na kununua dawa ya kukausha vidonda akaja na kumpaka seemu zote zenye vidonda!

Alex alikaa na kufikiria kwa makini, akaona kajiingiza kwenye vita kubwa sana, alimjua Filbet alivyokuwa katili na pia alijua baba yake alivyokuwa na pesa ambazo angeweza kufanya chochote kwa ajili ya mwanae, akaona uwezekano wa yeye kuendelea kuishi pale Dodoma mjini ni mgumu



"Hawa wameniajiri kwa kukutana hapa hapa mjini, hawanijui kwa namna yeyote ile, nikajifiche kule kwetu mpaka haya mambo yatulie na huyu binti apone ndipo nitajua cha kufanya" alipitisha uamuzi.

Na moja kwa moja akachukua akiba aliyokuwa amejiwekea pale mjini na akakabidhi chumba kwa mama mwenye nyumba kisha akaaga na kuondoka na Amina kuelekea kijijini kwao huko Hombolo nje kidogo ya mji huu wa dodoma.

Alifika kwao jioni sana ili watu wasimuone yule binti na kuleta maneno pale kijijini, alipokelewa na mama yake na baadhi ya ndugu zake waliokuwepo na moja kwa moja akampeleka Amina kwenye nyumba yake ( kwa sababu vijijini kila kijana huwa ana nyumba yake anayolala) akamlaza kitandani pake na kutoka kwenda kumwona mama yake.

"Vip baba? Huko kwema kweli? Naona na mkwelima juu" akauliza mama yake

"Huko ni kwema na pia si kwema,huyu binti ana matatizo ingawa siyajui kiundani ila nimeona nimsaidie" akajibu na kuanza kumweleza mkasa ule kwa jinsi anavyoujua mwanzo mpaka mwisho

"Jaman! Kuna watu wana roho mbaya sana,kama ndiyo hivyo acha nikamwone mtaalamu aje aone namna ya kumsaidia baba" akashauru mama na wote wakakubaliana na wazo lile

Baada ya muda wakati usiku ulishaanza kuwa mkubwa mama yake Alex alirudi na mganga na kumpeleka ndani kumona yule binti

Mtaalamu alitengeneza dawa za kuponya maumivu ya ndani ya mwili na kuondoa uvimbe na damu iliyogandiana pale pale na wakamnywesha kwa nguvu Amina ambaye hakuwa na fahamu kwa wakati huo.

Asubuhi ya siku iliyofata mganga alifika tena na kuendelea na matibabu yake, kwa sababu mwanga ulikuwepo tofauti na usiku uliopita aliweza kugundua maeneo aliyoumia zidi na kumpatia matibabu vizuri

Mchana wa siku hiyo wakiwa wanakula Alex yeye alikuwa pembeni ya kitanda cha Amina kumwangalia maendeleo yake,ndipo aliposhangaa Amina akipiga chafya mara tatu kisha akaamka na kukaa

"Mama.....mama....kaamka...njoeni" alipiga kelele kwa furaha. Mama yake na ndugu zake wakaingia na kila mmoja akaonesha furaha yake pale

"Niko wapi? Na nyie ni nan?" aliuliza

"Tulia binti, sisi ni msaada kwako, tuko hapa kukusaidia, hivyo usijali, uko katika mikono salama" akamwambia Alex.

Waliondoka na kwenda kumwita mganga na baada ya muda mfupi akafika na kuanza kumpa matibabu kidogo kisha Amina akaonesha nafuu ambayo aliweza kuongea mwenyewe

Mganga akamuulizia kilichomtokea na sehemu yeyote yenye shida aweze kusaidia,ndipo Amina alipoeleza kisa chote kilichomtokea mwanzo mpaka mwisho,alipomaliza wenye moyo mwepesi walilia ila wakampa pole na kuwahidi kusaidia

Ikabidi na yeye aulize imekuwaje awe pale na pale ni wapi?

Alex akabeba jukumu la kumwelewesha kila kitu kilichotokea mwanzo mpaka mwisho

"Nashukuru sana Alex, wewe ni binadamu wa pekee, sina cha kukulipa ila elewa umeokoa maisha yangu, nakushukulu sana" alitoa shukrani zake.


*************


:: Unavyodhani nini kitaendelea?


:: Hii ni mojawapo ya riwaya kali sana kutoka kwa mwandishi chipukizi hapa uwanja wa simulizi.


:: Onesha ushirikiano wako katika kumpa sapoti mwandishi wa riwaya hii kwa ku LIKE, ku SHARE na hata ku COMMENT kuhusiana na hii riwaya hapo chini.


ITAENDELEA
Powered by Blogger.