KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Simulizi : Ndoa Yangu Inanitesa Sehemu Ya Kumi Na mbili (12)

simulizi nzuri ya maisha, ndoa yangu inanitesa
“Mume wangu amka basi tufanye.” Getruda alinihimiza huku akiwa amenishika mkono wangu kidogo akininyanyua .

“Subiri kidogo naumwa na homa”

“Imekuwa homa leo” kwa kweli mke wangu alichoka na idadi ya magonjwa niliokuwa nikimtajia kila leo.

“Eti homa, utashaa leo, sikusikilizi ninachotaka ni penzi tu, usiniletee hadithi za riwaya, zile hadithi ndefu za kubuni, sizihitaji kabisa!, wewe mwanaume gani? Hivyooo!” Getruda mke wangu alianza kunidharau baada ya kuona sina lolote. Nilianza kulia nikilaumu ugonjwa ulioniingia nikiwa na ndoa yangu, niliulaani ugonjwa huo nilitamani nikatwe vidole kuliko kuwa na udhaifu wa nguvu za kiume. Kilio changu kilikuwa chungu mwenye na roho yangu. Pamoja na kunywa dawa za mitishamba kutoka kwa wamasai aina ya mchuma mbele bado nizidi kupata mateso ya unyumba.

“Mke wangu unadiriki kunikashifu. Kunitukana mtusi ya nguoni!, kweli umenichoka” nilijaribu kumlaumu mke wangu, lakini haikusaidia kitu.

“Ndio, nimekuchoka, naomba talaka yangu asubuhi hii hii, longolongo sitaki” mke wangu alibadilika ghafla na kunitizama kwa hasira kali, kama kungekuwa na uwezekano wa kuniadhibu basi angeniadhibu ipasavyo. Niliona bila kuwa mpole ndoa ingekuwa ndoano, ingesambaratika na ningekuwa mseja.

“Mke wangu naomba upunguze jazba nikueleze…” niliongea kwa sauti ya unyonge iliyona lengelenge la machozi kunitoka, nikiwa na wasiwasi mkubwa wa kumkosa Getruda. Sikupenda niachane na Getruda mke niliyepewa na wazazi, mke mwenye hali ya ubikira, ambaye hajawahi kuguswa.

“Nimeshachoka na mambo yako ya ajabu, unataka kunieleza nini?”

“Najua utanichukia nikikueleza kilichonisibu pia hutaamini yaliyonikuta mwenzio”. Niliongea machozi yakinilengalenga machoni, roho iliniuma na kujiona nisiye na faida wala umuhimu kuishi duniani, nilitamani kufa ilinisiendelee na mateso. Kilio changu kilikuwa cha huzuni mno!, moyo wa huruma ukamuingia mke wangu, masikini akaniomba nimuelezee.

“Mume wangu haya nielezee kilicho kusibu, usiogope kuwa wazi usinifiche chochote kama kuna uwezekano nitakusaidia mpenzi” sauti ya mke wangu niliisikia na kuifananisha na sauti ya malaika wa neema. Nikajikaza huku nikiwa na churuzika machozi yaliyolowanisha kope machoni.

“Mke wangu hujafa hujaumbika, nisikilize kama mtu asikilizavyo maneno ya Mungu, nilikuwa kiwandani kwenye uchanganyaji wake Kemikali, bahati mbaya kemikali yatindikali ilinidondokea kwenye ngozi karibu na uume wangu na kunisababishia udhaifu mwilini, naomba usiniache mpenzi, naomba unisamehe kama nimekukosea mpenzi, naamini nimekukosea. Sikuyataka bali yametokea bahati mbaya” Niliongea uwongo uliofanana na ukweli, kadri nilivyozungumza ndivyo nilivyozidi kulia, sikupenda kuongea uwongo bali ilinibidi niongee uwongo mtupu ilikuinusuru ndoa na aibu yangu , sikumwangikiwa na tindikali, ni ugonjwa ulionitokea ambao sikujua ulitokea wapi na nani aliyeniletea ugonjwa huo, je ni Jenipher au ni nani?”

“Sasa kama ulikuwa unajua unamatatizo kwanini ulinioa mpenzi?, unanitesa, umepoteza muda wangu bure” Getruda alizidi kulalamika japo alinionea huruma.

“Kumbe ndio maana kila siku ana lalamika na kunitajia magonjwa mengi yote hayo ni kukwepa…” Getruda aliwaza akilini.

“Mke wangu matatizo yalitokea siku tatu kabla ya ndoa, wala sikujua nimeadhirika na tindikali hiyo, ningejua ningehairisha kufunga ndoa ili upate mume rijali” maneno yangu yalimuingia Getruda mke wangu na kuamini kuwa ni kweli nilipata ajali ya kumwagikiwa na tindikali.

“Nitaishi vipi bila kupata matunda ya ndoa, naomba uniambie nitaishi vipi?, nitaishi hivi mpaka lini, sijawahi kukutana na mwanaume, nilitegemea wewe ndiye ungevunja boma langu, sasa itakuwa vipi? Naomba mawazo yako” macho ya huruma yalitua usoni mwangu, niliyekuwa nimetulia kama mtuhumiwa aliyesubiri hukumu ya kunyongwa.

“Mke wangu hilo usitie shaka. Hakuna kinachoharibika nivumilie kidogo”

“Siwezi kukuvumilia tena mume wangu. Naomba talaka haraka”Nilitamani kuondoka , ikiwezekana kuihama nyumba yangu,nikifikiri jambo hilo lingenisaidia lakini nikajikuta nikikatisha mawazo na nafsi.Nilitulia kama sekunde kadhaa hivi nikijaribu kuganga maumivu.



“Uliapa mbele ya mchungaji kwamba utaishi na mimi kwa uvumilivu…”Kabla sijamalizia maneno yangu , nikakatishwa na sauti ya ukali .

“Ndio. Nimevumilia nimechoka, naomba uelewa kwamba namimi nina homoni”Getruda akasema akinitizama kama mtu alieniandalia tusi.

“Nataka niende nchi za nje kwenda kufanyiwa uchunguzi zaidi”

“Nchi gani?”

“Uingereza….” Nilipumua kidogo kisha nikaendelea kumweleza, wakati huu nikimueleza, nilikuwa siamini kwamba angeweza kulielewa lile nililotaka alifahamu na kulitii “Getruda nakupenda na kiliwaahidi wazazi wangu nitaishi na wewe hadi mungu atakapo chukua roho zetu”

“Sweedy unajua maana ya ndoa kweli?”Getruda akaniuliza akiwa amenitumbulia macho.

“Ndio”Nikajibu kwa sauti ndogo na ya upole kabisa,nikiwa nimeinamisha kicha kama kondoo.

“Kama unajua maana yake.Mbona sioni nini maana ya ndoa kati yangu na wewe?”Hapo nikavuta pumzi ndefu na kuziachia kwa nguvu, “Ooooopphhhh”.Ikafikia wakati mwingine hata kujionea mwenyewe huruma.

“Si nishakuambia tatizo langu?”Nilizidi kutukutika moyoni.

“Basi kama unataka nisivunje ndoa yetu nitafutie ndugu yako aniridhishe kimapenzi mpaka utakapo pona”

“Sina ndugu yangu wakiume mke wangu.Kwa nini usiwe na subira?”Machozi sasa yakaanza kunidondoka kama maji ya dripu, nilihisi kudhulumiwa haki yangu , ingawa nilitaka njia ya amani kati yangu na mke wangu.

“Ngoja ngoja yaumiza matumbo”nilimtizama Getruda, mke wangu nikagungua hakuwa na nafasi tena ya kunisubiri. Macho yake tu, yalikuwa jawabu tosha kwamba angeondoka kwenda kutafuta mume mwingine.

“Nasubiri unijibu upesi, sitaki mzaha tena. Ushanipotezea muda mwingi sana Sweedy”Sauti ya kupaza niliisikia ikigonga ngoma za masikio yangu, nilijaribu kumtupia macho ya huruma,kuwa pengine angepunguza maneno. Sikuweza kumjibu chochote,badala yake nikabaki kimya kama niliyeletewa habari ya msiba wa ndugu yangu wa karibu.

“Dharau yako itakuponza. Wala sitaki talaka yako.Naondoka, narudi kwetu mwili wangu bado unaniruhusu kuolewa.Kama ni bikra bado ninayo kama ni kuzaa ndio kabisaa.Kwanini nikose mume.Uzuri wangu tosha nishahidi kwamba sitokaa kwetu mwezi bila kuolewa”Getruda aliongea na kunyanyuka kitini ambako alielekea chumbani. Nilibaki nikimtizama bila kunena neno juu yetu.Sikutarajia kuona kile kilichopo mbele yangu wakati huo.Nilimuona Getruda akiwa kabeba begi kubwa languo akitoka nalo nje varandani.

“Mke wangu tafadhali naomba uweke begi chini tuongee.Unapochukua uamuzi huo si suluhisho. Ni busara kusuluhisha mgogoro ili kuhuisha uhusiano mwema ,tangu kuumbwa kwa familia hakuna hata moja isiyopata ubishi na mgogoro ndani ya nyumba…..”nilivuta pumzi ndefu na kuzishusha taratibu ,ni dhahiri nilichoka kuitetea ndoa yangu isianguke.Wakati huo Getruda alinitupia jicho, begi lake akiwa kalishikilia mkononi.Nikavuta hatua na kumfikia karibu, nilimshika mkono nikijaribu kumbembeleza, “Tafadhali usinishike.Muda wa kuishi nawewe umeisha.Mume gani usiye…”Nilimkatisha maneno yake, “Ni samehe mke wangu,nitaendelea kukuita mke wangu kwa sababu nakupenda, naomba uwe na subira. Unyumba nikuvumiliana, kuna leo na kesho, kumbuka hujafa hujaumbika, jambo hili linaweza kukukuta hata wewe,pengine ukapata ajali.Sikupenda kuwa hivi mpenzi…. hili ni jambo la kawaida, muhimu ni jinsi ya kutatua mikwaruzo hii.Mfano ungekuwa wewe mwenye matatizo haya ungelifanya nini?”

Niliongea taratibu na kwa busara nikijaribu kumshauri Getruda , mke wangu. Alivuta pumzi na kuzishusha.

“Naomba unipe uhuru.Utakubali niwe naingiza mume mwenzio ndani?”

“Hapana. Utakuwa ni unyanyapaa wakijinsia.Getruda unataka kuniumiza moyo wangu.Nakupenda na nimekuomba uwe na subira,pengine nimajaribu ya mungu”Nilivumilia kulia ikashindikana,machozi yalinitoka bila kutegemea.Nilitamani nibaki peke yangu ,ingawa sikuweza kuamini kama kweli Getruda angenihifadhia siri yangu.Angeenda kuwaeleza nini wazazi wake.Kuna mtu anaweza kuvunja ndoa bila kufarakana, migogoro ya kiunyumba?.Mawazo hayo yalizidi kuniumiza na kunikera moyoni.

“Chagua moja….”Alitulia , akalamba midomo yake kisha kunitizama kwa dharau.Dharau hiyo niliigundua kwamba nikwa vile aliniona si lolote si chochote kwake.

“Unasema unanipenda sana?”

“Kwani hujui hilo?”

INAENDELEA
Powered by Blogger.