KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Kivuruge Wa Tandale Sehemu Ya Ishirini na Nne (24)

hadithi nzuri ya kivuruge wa tandale
“Nitamwambia siku nyingine,” niliwaza na angalau tabasamu lilirudi na kuwa halisi kwa sababu muda wote nilikuwa na wasiwasi mkubwa ndani ya moyo wangu kuhusu jinsi anavyoweza kupokea taarifa hizo.

“Nataka upone haraka bwana, unajua mume wangu anakaribia kurudi kutoka Sweden alikokuwa ameenda kimasomo sasa najua akija nitakuwa nakosa uhuru wa kukufaidi,” alisema, nikashtuka sana kusikia maneno hayo.

“Mbona unashtuka? Kwani nimeongea jambo lolote baya?” aliniuliza, nikatingisha kichwa kuonesha kwamba hakuna lolote baya aliloliongea. Akaniambia kwamba mumewe alisafiri kwenda nje ya nchi miaka minne iliyopita na walikuwa wakiwasiliana karibu kila siku japokuwa hakuwahi kurudi kutokana na kubanwa na masomo.

“Lakini nakuhakikishia wewe ndiyo utakuwa mume wangu mkubwa, yeye mume mdogo, unamzidi kwa kila kitu maana hata shughuli unayonipa, yeye hafikii hata robo,” alisema na kunifanya nicheke.

Moyoni nilifurahi kutokana na kauli yake hiyo kwa sababu alikuwa amenirahisishia sana kazi ingawa kwa upande mwingine nilijisikia wivu sana kugundua kwamba kumbe alikuwa na mume wake.

“Kwani unanipenda eeh, maana naona umebadilika nilipokwambia masuala ya mume,” aliniuliza, na mimi nikapata sehemu nzuri ya kumdanganya. Nilimwambia kwamba nampenda sana na sijawahi kukutana na mwanamke kama yeye, nikawa nampamba kwa maneno matamu.

Ukweli ni kwamba nilikuwa nataka kumuweka sawa tu ili aendelee kunibeba kazini na kunipa fedha maana alikuwa mhongaji mzuri.

“Umeongea maneno matamu sana jamani, mpaka nahisi kusisimkwa mwenzio,” alisema huku akianza kubana miguu yake mizuri kuonesha kwamba tayari wadudu walishaanza ‘kumnyevua’.

Ajabu ni kwamba nilipokuwa namtazama akifanya vile, na mimi nilianza kuhisi haki isiyo ya kawaida, nikashtukia tu tumegusanisha ndimi zetu huku mikono yake laini ikiperuzi na kudadisi kuelekea kwa mkuu wa kaya.

“Nimeambiwa nisubiri mpaka baada ya siku sa..ba,” niliongea huku nikifumbafumba macho kutokana na msisimko niliokua naupata.

“Sawa usijali, mi nataka nikuimbie tu kidogo mgonjwa,” alisema kwa sauti ya kudeka, sijakaa sawa nikashtukia amekamata ‘mic’, si akaanza kuimba bwana! Alikuwa akiimba kwa ufundi wa hali ya juu kiasi cha kunifanya nitupilie mbali masharti ya daktari, nikamsogeza mpaka kwenye sofa kubwa lililokuwa mle ndani ya ofisi yake.

Wakati akiendelea kuimba, nilifanya utundu wa kujipindua kama mwanasarakasi, nikavamia mzimamzima kwenye chungu chake cha asali, nikatoa mfuniko na kuanza kuilamba taratibu, akawa anatoa ukelele fulani huku akiendelea kuimba, hali iliyoyaamsha mno mashetani yangu.


Muda mfupi baadaye tayari tulikuwa kwenye ulimwengu mwingine tofauti kabisa, na japokuwa bado sikuwa na stamina za kutosha, lakini niliweza kwenda naye sawa na kweli ilionesha alikuwa amenimisi kisawasawa.

Sikukumbuka kabisa kwamba daktari alinisisitiza kukaa wiki moja bila kushiriki kwenye sanaa hiyo ya kikubwa.

Muda mfupi baadaye, Madam Bella alipasua madafu mawili kwa mkupuo, akanikumbatia kwa nguvu na kunipiga kabali kama wale vibaka wa kwetu Tandale, akashusha pumzi ndefu na taratibu akawa ananiachia, nikamsaidia kulala pale kwenye sofa.

Miongoni mwa udhaifu mkubwa aliokuwa nao Madam Bella, ilikuwa akishafanikiwa kupasua dafu hata moja, lazima kausingizi kampitie bila kujali yupo wapi.

Hicho ndicho kilichotokea na ili kumsaidia asije akathubutu kukutwa na mtu mwingine, niliyaweka vizuri ‘magwanda’ yake ikiwa ni pamoja na kumsogezea kufuli lake ili akiamka alione kwa urahisi, kisha nikatoka kimyakimya na kufunga mlango kwa nje kwa kutumia funguo, kisha funguo hizo nikazipitisha chini ya mlango kama nilivyofanya siku ya kwanza aliponiruhusu nilambe asali yake.

Nilirudi ofisini kwangu na kukaa, nikashtukia mapigo ya moyo yakianza kuongezeka kwa kasi huku mwili ukiishiwa nguvu. Zile dalili nilizokuwa nazo siku ile nilipozidiwa na kukimbizwa hospitali, zilianza kujirudia.

“Mungu wangu, nimefanya nini sasa,” niliwaza huku nikihofia mno kitakachotokea. Kwa bahati nzuri kwenye begi langu la laptop ambalo huwa natembea nalo kulikuwa na Glucose, nikaitoa na kuanza kuilamba harakaharaka.

Kwa kawaida Glucose huwa na uwezo mkubwa wa kumuongezea mtu nguvu ndani ya muda mfupi. Ilinisaidia sana, nikaona niongeze na Redbull. Nilimuita Salma ambaye harakaharaka alikuja na kunisogelea mwilini. Nikamueleza kwamba sijisikii vizuri na naomba akaninunulie Redbull na maji makubwa.

“Umepatwa na nini tena?”

“Naona mwili unaishiwa nguvu na mapigo ya moyo yananienda mbio,”

“Ooh, maskini pole! Inaonekana bado hujapona wewe,” alisema huku akinishika kwenye mashavu yangu kwa mikono yake laini, nikataka kutoa hela ya kwenda kununulia vitu nilivyomuagiza lakini aliniambia nisijali, atatumia hela yake.

Basi alitoka na muda mfupi baadaye, alirejea akiwa na vitu nilivyomuagiza lakini pia alikuwa na bakuli la supu mikononi mwake, akaniandalia kila kitu vizuri. Nilimshukuru sana kwani alinionesha upendo mkubwa sana. Nilianza kwa kugonga ile supu, nikafuta bakuli lote, nikahamia kwenye maji, nikapiga karibu nusu nzima ya chupa kisha nikawa nashushia na Redbull taratibu.

“Hapo vipi?”

“Hapo sawa!” nilimjibu, akacheka kisha tukagongesheana mikono, tangu mara ya kwanza nilipofanikiwa ‘kuona ndani’, Salma alikuwa amebadilika sana jinsi anavyozungumza na mimi.

Kama nilivyowahi kueleza, kabla hatujaanzana, Salma alikuwa na nyodo kwelikweli, muda wote anajifanya yupo siriasi, kila anachoongea anatanguliza jazba na hasira lakini sasa hakuwa tena na ujanja wa kunifanyia mambo hayo. Sijui kama kwa watu wengine alikuwa anaendelea kuwakazia lakini kwangu mimi alibadilika mno.

“Hapo ukipewa mchezo unaweza kweli?”

“Unataka kunijaribu si ndiyo? Mimi sijaribiwi!” nilisema huku nikibadilisha lafudhi na kuongea kama Wasukuma wanavyokandamiza maneno, akacheka mno na kuja kunikumbatia. Katika hali ambayo sikuitegemea, alinibusu, tena mdomoni huku akipitisha mikono yake nyuma ya shingo yangu.

Sijui nini kilinishawishi, na mimi nikajikuta nikipeleka mikono yangu kwenye kiuno chake kama dondola, akashtuka kidogo kama aliyechomwa na mwiba huku mihemo yake ikibadilika, tukagusanisha ndimi zetu na kuanza kubadilishana ‘juisi ya miwa’ huku akijiweka vizuri na kunikalia kwenye mapaja yangu.

“Nilikumisi mno mpenzi wangu,” aliniambia huku akinitazama kwa macho yake yaliyojaa aibu za kikekike, ambayo sasa yalikuwa yamelegea mithili ya mtu anayesikia usingizi, akanibusu tena mdomoni.

“Nilikumisi pia kipenzi cha moyo wangu, nikiwa mbali kidogo na wewe nazidi kuumwa,” nilimwambia. Kauli yangu hiyo ilikuwa ni kama imeamsha mashetani kwani alinikumbatia tena kwa hisia zaidi, akalegeza vifungo vya blauzi yake kisha katika hali ambayo sikuitegemea kabisa, alisimama akiwa ni kama amesahau kitu.

Alitembea harakaharaka mpaka pale mlangoni, akafunga kwa funguo kisha akarudi pale nilipokuwa nimekaa kwenye kiti, akalishusha kufuli lake na kulitoa kabisa, akalitupia pembeni, mapigo ya moyo yakanilipuka paah! Nikameza mate kama fisi aliyeona mfupa huku nikishangazwa na ujasiri wake wa kucheza na sharubu za simba.

Yaani kama kuna mtu aliyenilogezea kwenye haya mambo, basi alikuwa ameniweza kwelikweli.

Kuna wakati huwa naamini kwamba ile haikuwa akili yangu kwa sababu inawezekanaje nimetoka kumvuruga Madam Bella mpaka nimeishiwa nguvu, lakini muda mfupi baadaye baada ya kunywa supu na kunywa Redbull kisha Salma kujilengesha, najikuta tena nikiwa na uchu kama mtu aliyetoka jela?

Basi Salma alinisogelea akiwa anatembea kama miss, akijinyonganyonga huku na kule, akanisogelea pale nilipokuwa nimekaa na kukaa kama vile alivyokuwa amekaa mara ya kwanza, kwenye mapaja yangu.

‘Mkuu wa kaya’ alikuwa amefura kwa jazba kali, akawa anahisi kama namchelewesha. Nilichokifanya, nilimuelekeza Salma kuinuka kidogo, nikamtoa nyoka pangoni, Salma akawa anachekacheka kama mtoto aliyeona Ice cream huku na yeye akijilamba midomo yake.

Hata sijui nini kiliendelea, nilijikuta tu napiga mashuti marefu huku Salma akitoa miguno ya hapa na pale, mikono yake ikiwa imeshika vidole vya miguu yake na kunipa mgongo huku akiwa ni kama anayegoma kwenda mbele, eneo la katikati lote likiwa juu.

Basi niliendelea kupiga mashuti kwa nguvu, naye akawa anaendelea kulalama huku akilitaja jina langu na kunisihi nisiwe na kasi uwanjani kama yule mchezaji kinda wa Ufaransa, Mbappe aliyechukua tuzo ya mchezaji bora chipukizi kwenye kombe la dunia.

Haukupita muda mrefu, nilimbabatiza na shuti la kushtukiza, akajifunga bao moja matata sana na kuanza kushangilia ushindi huku akitetemeka mwili wote wakati kiuhalisia mimi ndiye niliyetakiwa kushangilia. Alitaka kunyanyuka lakini nikamzuia, nikapiga pasi ndefu kwa namna ile ambayo wataalamu wa soka wanaita ‘counter attack’, yaani unapiga mpira juu kidogo kuelekea mbele halafu na wewe unatimua mbio kuufukuzia ukiwaacha wachezaji wa timu pinzani wanakanyagana.

Niliwahi na bila kupoteza muda, nilifumua shuti lingine kali zaidi, likajaa moja kwa moja wavuni, kipyenga kikapulizwa kuashiria kumalizika kwa ngwe ya kwanza.

“Halafu wewee! Yaani hapo unaumwa ndiyo umenifanyia hivi, ungekuwa mzima si ungeniua kabisa? Mgonjwa gani una miguvu kama faru aliyejeruhiwa?” alisema Salma kwa sauti iliyokuwa inatokea kwenye matundu ya pua zake, akanikumbatia na kunibusu kisha akaninong’oneza sikioni.

“Unajua sana namna ya kuitii kiu yangu ndiyo maana nakupenda na kukuheshimu sana kivuruge wangu,” nilijikuta nacheka baada ya kauli hiyo, akawa ananiambia eti nisicheke kwa sababu anachokisema anamaanisha.

Basi aliendelea kunishukuru huku akinimwagia misifa kibao, mara simu ya mezani ikaanza kuita mapokezi ambapo kimsingi ndipo ilipokuwa ofisi yake. Harakaharaka alikurupuka na kwenda kufungua mlango, akaenda kupokea simu hiyo huku akiliacha kufuli lake palepale alipokuwa amelitupa.

Kwa kuogopa linaweza kuonwa na mtu mwingine na kuleta picha isiyofaa, nililiokota na kuliweka kwenye mfuko wa pembeni wa begi langu la laptop. Mara alirudi akiwa anatembea kwa kuyumbayumba kama mlevi, nadhani dozi aliyoipata ilikuwa imefika mahali pake.

“Bosi amepiga simu anasema uende ofisini kwake na laptop yako,” alisema huku akinitazama kwa macho yaliyobeba ujumbe mzito ndani yake.

Salma alishaanza kuwa ananipenda kwa dhati na hakuweza kujificha, angejua jinsi mwenzake nilivyokuwa na mambo mengi kichwani, wala asingekubali kunikabidhi moyo wake kiasi kile, kwa sababu mtu anaweza kukutazama kikawaida lakini pia anaweza kukutazama huku uso wake na macho yake vikizungumza lugha nzito kutoka ndani kabisa ya moyo, kama yeye alivyokuwa akifanya kwa wakati huo.

“Ok poa,” nilisema huku nikiinuka na kukimbilia maliwatoni kwani nisingeweza kwenda nikiwa na hali ile, Madam Bella ni mtu mzima kwa hiyo lazima angenishtukia, tofauti na Salma ambaye alishindwa kabisa kugundua kwamba muda niliokuwa nampa haki yake, nilikuwa nimetoka pia kumvuruga Madam Bella.

Nilijiswafi fastafasta kisha nikatoka na kurudi ofisini kwangu, yaani siku ya kufa nyani miti yote huteleza na za mwizi arobaini, waliosema misemo hii hawakukosea kabisa.

Sijui nini kilitokea kwani nilijikuta nimesahau kabisa kwamba lile kufuli la Salma nimeliweka kwenye begi la laptop, nikainuka huku na mimi nikipepesuka kwani miguu haikuwa na nguvu kabisa, nikabeba begi langu la laptop na kuelekea kule ofisini kwa bosi.


“Jamani ndiyo nini umenifanyia?” Madam Bella alisema baada tu ya mimi kuingia, akajizoazoa maana bado alikuwa amekaa pale kwenye sofa kichovu, akaenda kufunga mlango kwa ndani, akachomoa kabisa funguo kisha akanisogelea na kunikumbatia na kunibusu sehemu mbalimbali za mwili wangu.

Akalivua lile begi la laptop nililokuwa nimelivaa, akaliweka mezani na kunikumbatia kwa uhuru zaidi, tukagusanisha ndimi zetu huku na mimi mikono yangu nikiipeleka kwenye kiuno chake na kukishika kwa ustadi wa hali ya juu, akawa anajikunjakunja kama nyoka. Tulikaa kwenye hali hiyo kwa dakika kadhaa.

“Ahsante kwa kunitoa chozi la utamu!” nilikuwa siyajui mimi mambo haya,” aliniambia huku akinitazama kwa macho yake ambayo yalikuwa yamelegea kwelikweli, nikamwambia asijali, nipo kwa ajili yake.

“Unisamehe sana, mwenzio nikishafika kwenye ‘naniliu’ mwili unachoka sana na najikuta tu napitiwa na usingizi,” alisema huku safari hii akinitazama kwa aibu za kikekike kama mwari.

“Halafu wewe huwa unafanyeje? Mbona mume wangu hajawahi kunifanya nijisikie hivi hata mara moja? Kabla sijaolewa pia niliwahi kuwa na wanaume wawili kwa nyakati tofauti lakini hakuna aliyenifanya nikaweza kupanda juu ya mnazi na kuangua madafu kama wewe,” alisema huku akicheka, na mimi nikacheka, tukakumbatiana tena.

Taratibu Madam Bella alinikalisha kwenye lile sofa, moyoni nikawa najiambia asije akataka tena maana nitakufa.

Bado nilikuwa kwenye kipindi cha uangalizi maalum kama daktari alivyoniambia na sikutakiwa kabisa kufanya hayo mambo, sema tu uroho wangu na mitego niliyokumbana nayo asubuhi hiyo kutoka kwa Madam Bella na Salma vilinifanya nipuuzie ushauri wa daktari.

Nilichokihisi ndicho kilichotokea, Madam Bella aliponikalisha pale kwenye sofa mle ndani ya ofisi yake, nilimuona akilichomoa tena kufuli lake ambalo hata sijui alilirudisha sehemu yake muda gani, akalitupa na kwa bahati mbaya, lilidondokea pale kwenye mkoba wangu wa laptop, tena palepale nilipokuwa nimelificha lile la Salma.

Alitoa kipaza sauti na kama kawaida yake akaanza tena kuimba na safari hii, alikuwa akiimba kwa mtindo wa tofauti kidogo, nikajikuta mawazo juu ya lile kufuli lake yakiyeyuka ghafla, sasa nikawa nasikiliza utamu wa mashairi aliyokuwa akighani.

Tatizo langu jingine ni kwamba mkuu wangu wa kaya, huwa hana kabisa subira! Ule msemo wa subira yavuta heri yeye ulimpitia mbali kabisa kiasi kwamba nikifanyiwa uchokozi kidogo tu, yeye anafura kwa jazba kama nyoka koboko anayetaka kutema sumu.

Kile alichokuwa akikifanya Madam Bella, kilimfanya azidi kututumka kadiri muda ulivyokuwa unaenda, nadhani na yeye alikuwa akifurahia muziki laini uliokuwa ukiimbwa na bosi wetu, Madam Bella.

Aliendelea na alichokuwa anakifanya na muda mfupi baadaye, alifanya kama wakwezi wanaoangua nazi na madafu juu ya mnazi wanavyofanya. Mguu mmoja aliukanyaga juu ya sofa, pembeni kidogo ya kiuno changu, ule mwingine akaupitisha upande wa pili kisha akaukwea mnazi kwa pupa, akaanza kujisevia.

Kwa jinsi alivyokuwa na papara, hakuchukua muda akawa ameshafika juu kabisa ya mnazi, akaangua madafu mawili na kuyapasua mfululizo! Kama nisingewahi kumshikilia, pengine angedondoka na kujiumiza kwani alikuwa akipaparika kama kuku aliyekatwa kichwa.

Ilibidi pia nitumie mkono wangu kumziba mdomo wake kwani alikuwa akipiga ‘nduru’ kwa sauti ya juu, nikamshikilia mpaka alipotulia, nikamsaidia kulala vizuri pale juu ya sofa. Haukupita muda akapitiwa na usingizi mzito. Hiyo ndiyo ilikuwa ponapona yangu kwani sasa nilikuwa na nafasi ya kutatua utata juu ya yale makufuli.

Harakaharaka nilimrudisha mkuu wa kaya kwenye himaya yake, nikasogea pale kwenye begi la laptop, nikalitoa lile kufuli la Madam Bella, yakatoka yote mawili pamoja na lile la Salma. Kwa jinsi yalivyokuwa yakifanana, nilipata wakati mgumu wa kuyatenganisha, baadaye nikapata wazo la kupima ukubwa.

Kimwili Madam Bella alikuwa mkubwa kwa kila kitu kwa Salma, kwa hiyo ‘nikajiongeza’ kwamba lazima lile kubwa ndiyo litakuwa la kwake, nikajiridhisha pia kwa harufu ya manukato!

Baada ya kumaliza zoezi hilo, nilijiweka sawa, nikabeba laptop na kwenda kufungua mlango. Kama nilivyofanya mwanzo, nilitoka na kufunga mlango kwa nje kisha nikaingiza funguo kupitia chini ya mlango lakini wakati nikiinama kuingiza funguo hiyo, nilisikia kitu kama kimenichoma kwenye mgongo wangu, yakafuatia maumivu makali kwelikweli ambayo hata siwezi kuyaelezea.

Nilijikaza na kuondoka nikiwa na laptop yangu, nikaenda ofisini kwangu kimyakimya na baada ya kuweka laptop, nilienda ‘washroom’ kujiswafi kuondoa ushahidi lakini mgongo ulikuwa unaniuma kwelikweli. Nikarudi ofisini kwangu na kwenda kukaa huku nikijisikilizia maumivu.

Muda mfupi baadaye, Salma alinifuata, akanikuta nimekaa kichovu huku nikiwa naichezea laptop yangu.

“Vipi baby!”

Alisema huku akija mwilini mzimamzima na kunikumbatia, akanibusu!

“Mh! Mbona kama unanukia harufu ya pafyumu ya bosi,” aliniuliza swali ambalo sikulitegemea, nikamdanganya kwamba kuna kazi nilikuwa namuelekeza bosi kwenye laptop kwa hiyo muda muda mwingi tulikaa karibu na kugusana, akashusha pumzi ndefu akionekana kuukubali uongo wangu.

“Umeona ulichonifanyia?” alisema huku akipandisha juu sketi yake laini aliyokuwa ameivaa, macho yangu yakatua kwenye kiota cha ndege tetere kilichokuwa na mvuto wa aina yake machoni.

“Umeondoka na ‘naniliu’ yangu, unaona mwenzio nimebaki hivi hata kutoka nje nilikuwa naogopa,” alisema kwa aibu za kikekile huku akinisogelea vilevile, ikabidi nivunge kwani mgongo ulikuwa unaniuma kwelikweli, nikanyoosha mkono na kutoa kufuli lake kwenye begi la laptop, nikataka kumpa lakini akaniambia eti ananipa adhabu ya kulirudisha mahali pake.

“Please Salma, mwenzio naumwa ujue, nitakufa uju...” kabla hata sijamalizia kauli yangu, tayari alikuwa ameshanivaa mwilini, akapitisha mikono yake ndani ya shati nililokua nimevaa na kushika kifua changu kwa ustadi wa hali ya juu, nikahisi kama nimepigwa na shoti ya umeme.

“Kwa ni..ni..ni una..ni..cho..ko..za,” nilisema kwa sauti ya kugugumia, akawa ananitazama kwa uchu, mdomo wake ukajaa mate kama mtu aliyeona kipande cha ndimu.

Alichokifanya, alinisogezea kopo langu la Redbull ambalo nilikuwa nimekunywa nusu! Akaninywesha ile iliyobaki mpaka ikaisha. Akanipokonya lile kufuli lake na kulitupa chini, nikajua kazi ipo.

Aliilegeza ile sketi yake upande wa kiunoni, alipoiachia ilidondoka mpaka chini, nikawa namtazama utafikiri ndiyo mara yangu ya kwanza kumuona. Hata sijui alifunga mlango saa ngapi, akaja kunikumbatia kwa hisia za hali ya juu huku mapigo ya moyo wake yakienda mbio na pumzi zikimtoka bila mpangilio.

Ni kweli nilikuwa najisikia maumivu makali ya mgongo na sarakasi nilizozifanya muda huo zilikuwa zimenimaliza kabisa nguvu lakini sikuweza kuvumilia majaribu aliyokuwa ananifanyia Salma.

Hata kama ningesema navunga, mkuu wa kaya kama kawaida yake, kiherehere chake kilimfanya ashindwe kutulia sehemu yake, Salma naye akatumia fursa hiyo kutimiza lengo lake, akamchomoa pangoni na bila ajizi, alimuelekeza sehemu anayotakiwa kuwepo muda huo, akamsindikiza kwa mbwembwe za hali ya juu zilizonifanya niwe kama nimepandwa na mashetani.

Unajua wasichokijua watu wengi ni kwamba japokuwa wanawake wanaweza kuonekana sawa kwa macho ya nje, ukweli ni kwamba kila mmoja yuko tofauti kabisa na mwingine. Japokuwa nilikuwa nimetoka kuliamsha dude kwa Madam Bella, Salma na yeye alikuwa tofauti kabisa.

Cha ajabu ni kwamba hata yale maumivu ya mgongo sijui hata yaliishia wapi, ikawa ni piga nikupige katika lango la timu pinzani, yeye alileta ujuzi wake na mimi nikawa nampelekea ‘machejo’ yangu, kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele ndivyo ushirikiano kati ya akili na mwili ulivyokuwa unapungua, ikafika mahali nikawa hata sielewi niko wapi na nafanya nini.

Ninachokumbuka ni kwamba Salma alijifunga goli la kushtukiza na mimi nikapachika lingine lililotingisha nyavu zake, kisha nikadondoka kama mzigo, giza nene likatanda kwenye upeo wa macho yangu.

Sikuelewa tena kilichokuwa kinaendelea, baadaye nikaanza kusikia sauti kwa mbali, watu wawili walikuwa wakijadiliana, mmoja akimuuliza maswali na mwingine akijibu.

“Huyu ni nani yako?”

“Ni mume wangu.”

“Mh! Mume wako?”

“Ndiyo.”

“Nini kimetokea?”

“Kuanzia asubuhi alikuwa analalamika kwamba mwili unaishiwa na nguvu, ghafla tukashangaa amedondoka chini na kupoteza fahamu.”

“Hebu tusubirini nje.”

“Hebu mtundikieni dripu kwanza kwa sababu inaonesha ana upungufu mkubwa wa maji,” nilimsikia yule mwanaume akisema, nikaanza kuvuta picha kwamba lazima nitakuwa hospitali. Nilijaribu kufumbua macho mara kadhaa lakini nilikuwa nashindwa, kila kiungo katika mwili wangu kilikuwa ni kama kimekufa ganzi.

Basi nilisikia kama mkono wangu ukifutwafutwa na kitu chenye ubaridi, kisha nikasikia sindano ikiingia mishipani. Nilitamani kufumbua macho lakini sikuweza kwa hiyo ikabidi nitulie tu.

Baada ya kama dakika ishirini hivi, nilijaribu tena kufumbua macho, safari hii nilifanikiwa. Nilichokuwa nakihisi ndicho kilichotokea, kweli nilikuwa nimelazwa kwenye kitanda kilichotandikwa mashuka meupe huku dripu ikiwa inatiririka kwa kasi kuingia mishipani mwangu.

INAENDELEA

Powered by Blogger.