KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Kivuruge Wa Tandale Sehemu Ya Kumi Na Tisa (19)

hadithi nzuri ya kivuruge wa tandale
Kama mtu angeingia haraka, angeweza kudhani mimi na yeye ni wapenzi, mkononi alikuwa ameshika simu yake na ile chaja niliyompa.

“Simu yangu haiingizi chaji halafu nilikuwa naomba ukanisaidie kitu, unajua bado sijapanga vizuri vitu ndani kwangu kwani sina mtu wa kunisaidia, leo nimekuona upo nyumbani nimefurahi,” alisema huku akinitazama kwa macho fulani hivi, na mimi nikawa namtazama huku nikimuitikia kwa kutingisha kichwa tu kwani akili zangu zilishaanza kuhama.

Moyoni nikawa najisemea ‘hawa wanawake’ wataniua sasa, yaani hata sipati muda wa kupumzika! Basi nilimuuliza anataka nimsaidie nini, akaniambia kwanza anataka nikamchomekee simu yake kwenye chaji kule ndani kwake halafu nimsaidie na kupanga baadhi ya vitu.

Kitu kisicho cha kawaida kilitokea, kwa kuwa nilikuwa nimejifunga taulo tu, kitendo cha kuendelea kutazamana naye kihisia, kilisababisha ‘Ashrafu’ aamke tena kwa fujo na kwa kuwa hakukuwa na kizuizi, yule msichana aliweza kuona kila kitu, akawa ni kama ameshtuka hivi na kujiziba usoni eti ili asione kilichotokea.

Hata sijui nilipata wapi ujasiri kwa mtu ambaye hatujazoeana, nilimgusa shingoni na kumsogeza kwangu, naye bila kikwazo chochote akasogea mzimamzima, nikajisemea ‘liwalo na liwe’, nikamkubatia kwa nguvu huku mikono yangu ikienda moja kwa moja kwenye ‘chura’ wake, akashtuka kidogo na kuanza kunitazama kwa macho ya kurembua.

“Unataka kuni..fanya ni..ni,” aliuliza kwa sauti ya kudeka kama mtoto mdogo.


Sikumjibu kitu, nikamsogeza zaidi na kugusanisha ndimi, tukawa tunawaigiza njiwa wanavyoyalisha makinda yao. Khazija alikuwa mtundu sana, yaani ilionesha wazi kwamba alikuwa mtoto wa mjini kwani alikuwa akijinyonganyonga kama chatu aliyemeza mbuzi na kuzidi kunipandisha mizuka.

Sijui alifanyaje, nikashtukia lile taulo limedondoka, akajikunja kama mwanasarakasi na kuikamata ‘microphone’, akaipeleka usawa wa mdomo na kuanza kurap kwa staili ya kufokafoka huku akiwa ameishika kwa mikono yake yote miwili.

Huwezi kuamini, mimi huwa mgumu sana kupiga kelele tuwapo kwenye sanaa hiyo ya kikubwa lakini umahiri wake ulinifanya nishindwe kujizuia na mimi nikawa namfuatisha anavyorap, sauti yangu ilikuwa ikizidi kuongezeka kadiri muda ulivyokuwa unasonga mbele.

Waliosema kila mjanja na mjanja wake hawakukosea, Khazija alikuwa mjanja wangu, ndani ya dakika chache tu za kupasha misuli, tayari alikuwa ameshaibuka mshindi kwa sababu mambo aliyokuwa ananifanyia ama kwa hakika yalikuwa mageni kabisa.

Kuna wakati alikuwa anarap mpaka anailamba ‘microphone’ upande wa nyuma, nyaya za kupeleka sauti kwenye spika zinapoanzia, basi nikajikuta macho yanapoteza utulivu wake, yakawa yanazunguka kama goroli, mdomoni nikawa kama natafuna ‘bablish’ wakati ukweli ni kwamba hakukuwa na chochote, nilikuwa nimepatikana.

“Shhh!” alisema Khazija huku akinioneshea ishara ya kuacha kupiga kelele, nadhani mayowe niliyokuwa napiga sasa yalikuwa yamekolea kiasi cha kumfanya hata yeye awe na hofu.

Ilibidi harakaharaka niinuke na kwenda kuongeza sauti ya redio, nikaufunga mlango vizuri kwa ndani ili kusitokee usumbufu wa aina yoyote.

Niliporudi kwa Khazija, tayari alikuwa ameitoa ile ‘pensi nyanya’ aliyokuwa ameivaa na sasa alikuwa akimalizia kuitoa blauzi. Kwa sababu ya udogo wa kifua chake, wala hakuwa na ulazima wa kuvaa ‘bra’, kwa hiyo alipomaliza alikuwa saresare na mimi, mimacho ikanitoka nikiwa ni kama siamini nilichokuwa nakiona mbele ya macho yangu.

Khazija alikuwa na umbo zuri mno, nikawa namtazama kuanzia juu mpaka chini, mimate ikawa imenijaa mdomoni kwa uchu. Yaani usingeamini kama ni mimi ndiye ambaye muda mfupi uliopita nilikuwa ‘msambweni’ na mama mwenye nyumba mpaka mwenyewe akaomba ‘poo’.

Alitembea kwa maringo huku akijitingisha na kunisogelea pale nilipokuwa nimesimama, nikaendelea kubabaika mwenyewe, ‘Ashrafu’ akiwa amefura kwa hasira na kuongezeka ‘saiz’.

Basi alinishika mkono na kunielekeza nini cha kufanya, basi nikawa namfuata kama kondoo anayepelekwa machinjioni.

Chumba kilikuwa changu lakini nilikuwa kama mgeni, akanipeleka mpaka chumbani na kunitaka nilale kifudifudi, hata sijui ilikuwajekuwaje, nikashtukia amekamata ‘microphone’ tena na kuanza kuimba ila safari hii hakuwa akirapu bali alikuwa akiimba nyimbo za taratibu zilizonifanya niwe najinyonganyonga kama nacheza ‘mabreka’.

Nikiwa nimeshakolea kisawasawa, alimkamata ‘Ashrafu’ aliyekuwa amefura kisawasawa na kumuelekeza njia ya kupita, raha niliyoisikia ilinifanya niwe nataka kufumbua macho lakini muda huohuo nataka kuyafumba, kwa hiyo yakawa hayajafumbuliwa wala hayajafumbwa, hebu vuta picha!

Nadhani na yeye aligundua kwamba alikuwa amenipatia kisawasawa, akawa ni kama anaendesha baiskeli hivi, kwa mara nyingine nikajikuta naanza kubwabwaja kwa sauti ya juu, hata sijui nilikuwa nazungumza nini ila ninachojua ni kwamba nilikuwa natoa sauti.

Alipoona nimezidiwa, naye aliongeza kasi, basi akili zangu zikawa nusu zipo eneo la tukio na nusu nyingine sijui ziko wapi, nikawa naweweseka tu na haukupita muda, tayari nilishaanza kuiona theluji juu ya Mlima Kilimanjaro, nikaongeza kasi ya kukwea juu na sekunde chache baadaye, tayari nilishakuwa juu kabisa ya kilele.

Kumbe kile kitendo cha kuongeza kasi Khazija hakukitegemea, kwa hiyo kikamfanya na yeye aongeze kasi ya kuifuata ile theluji kule kileleni na katika hali ambayo hakuna aliyeitegemea, wote tulifika kwa wakati mmoja, mimi nikatoa sauti nzito na yeye akapiga ukelele fulani ulioleta raha ya ajabu masikioni mwangu, nikajitupa pembeni na haukupita muda, nilianza kuhisu usingizi mzito kuliko kawaida.

Muda huohuo nilimsikia Khazija akiinuka na kuchukua nguo zake, baada ya muda kidogo nikasikia mlango ukifunguliwa, sikumbuki nini kiliendelea lakini nilikuja kuzinduka baadaye sana na kujikuta nimelala peke yangu pale kitandani.

Niliinuka nikiwa nimechoka sana, harakaharaka nikachukua taulo na kujifunga kiunoni, nikatoka sebuleni na kukuta msosi umewekwa pale mezani na bila hata kuuliza, nilijua lazima umetoka kwa mama mwenye nyumba.

Sikumbuki alileta saa ngapi lakini kwa kuwa ulikuwa kwenye ‘hotpot’ bado ulikuwa wa motomoto.

Kwa jinsi nilivyokuwa na njaa niliufakamia harakaharaka na ndani ya muda mfupi tu, vyombo vilikuwa vitupu, nikashushia na glasi mbili za maji kisha nikatoka na kwenda bafuni kuoga. Angalau sasa nilirudiwa upya na nguvu lakini kuna kitu cha tofauti nilikuwa nakisikia ndani ya mwili wangu.

Nilikuwa mwepesi sana, yaani kuna wakati nilikuwa nahisi kwamba hata upepo mkali ukija unaweza kuniangusha. Nilijizoazoa mpaka ndani, nikajilaza pale sebuleni na kuwasha runinga, nikawa naendelea kutazama huku akili zangu zote zikiwa kwa mtoto Khazija.

Japokuwa jana yake nilikuwa naamini kwamba Ruqaiya ni mwanamke wa kipekee sana ambaye sijawahi kukutana na mtu kama yeye maishani mwangu, Khazija alikuwa ni habari nyingine! Tofauti yao ni kwamba Ruqaiya alikuwa na ile ladha ya asili wakati Khazija yeye alikuwa ‘fundi’ kwelikweli.

Kila nilipokuwa navuta picha jinsi alivyonipelekesha, nilikuwa naishia kucheka mwenyewe, nikawa nakarudiarudia kale kamsemo ka wahenga kwamba kila mjanja na mjanja wake.

Kwa kuwa watoto wa mama mwenye nyumba walikuwa wamesharudi shuleni, nadhani mwenyewe alishindwa kuja kuvifuata vyombo vyake, kwa hiyo nilichokifanya nilivichanganya na vyombo vyangu na kuvitoa nje, nikaviweka kwenye karo la vyombo.

Nilirudi ndani na kukaa mkao wa kutazama kwenye mlango wa Khazija, nilitaka japo nimuone tu sura yake ili roho yangu ifurahi kwa sababu alikuwa ameniweza kisawasawa lakini huwezi kuamini mpaka giza linaanza kuingia, sikumuona.

Nilitamani kwenda kugonga mlango wake lakini moyo ukawa unasitasita kwa sababu kiukweli kila mtu angenishangaa.

Japokuwa nilikuwa napigiwa sana simu siku hiyo kuanzia na Salma, Madam Bella, Ruqaiya na Nancy, wote nilikuwa nawajibu kimkatomkato isipokuwa Ruqaiya peke yake, muda wote macho yangu yalikuwa kwenye mlango wa Khazija.

Muda ulizidi kuyoyoma, kwenye majira ya kama saa tatu hivi, nilisikia mlango wa chumba cha Khazija ukifunguliwa, harakaharaka nikainuka na kufungua pazia, nikamuona akitoka.

Nilifungua mlango wangu harakaharaka na kutoka nje.

“Jirani vipi, naomba nipitishie chaja yangu,” nilizuga kwa sababu nilijua lazima mama mwenye nyumba na wapangaji wengine wanatusikia, basi alipomaliza kufunga mlango wa chumba chake, akaja mlangoni kwangu.

Alikuwa amejipodoa na kupodoka kisawasawa, kinguo alichokuwa amevaa, kigauni fulani hivi chenye rangi za kung’aa, kilimfanya aonekane kama malaika, ukizingatia na ile shepu yake ya kukata na shoka, alipendeza mno na uzuri wake kuongezeka maradufu.

Yote tisa, kumi alikuwa akinukia sana na begani alikuwa na mkoba mdogo wa kisasa.

“Umependeza sana jamani,” nilimwambia, akanijibu kwa kifupi ‘ahsante’.

“Wapi mida hii?”

“Naenda kwa rafiki yangu, ana bethidei yake.”

“Wapi?”

“Masaki.”

“Nikusindikize?”

“Hapana, tutaonana kesho.”

“Kesho? Ina maana hurudi leo?”

“Hapana, mpaka kesho,” alisema huku akigeuka na kuanza kutembea kwa maringo kuelekea getini, huwezi kuamini kwa mara ya kwanza nilijisikia wivu wa kupindukia kwenye moyo wangu, nikatamani nimfuate lakini nikaona nishai, nikabaki nimeduwaa tu pale mlangoni kama msukule. Mara nikasikia mlango wa mama mwenye nyumba ukifunguliwa.

“Vipi ulikuwa unaongea na nani?”

“Huyu dada mgeni alikuwa ananiomba nifunge mlango anatoka,” nilimdanganya mama mwenye nyumba, akasogea mpaka getini na kuhakikisha kama kweli ametoka.

“Mbona sasa hujafunga?”

“Nilikuwa nataka kuja kufunga ndiyo nikakusikia unafungua mlango,” nilizidi kuutetea uongo wangu, akaufunga mlango na kunisogelea.

“Mtoto mshenzi huyu, anaenda kwenye biashara zake saa hizi kurudi mpaka asubuhi!”

“Biashara gani?”

“Hee! Kumbe hujui... anafanya biashara ya kujiuza pale Kona, Sinza Afrika Sana, kila siku asubuhi mimi ndiyo namfungulia mlango, alisema mama mwenye nyumba, moyo ukanilipuka paah! Japokuwa kulikuwa na baridi, kijasho chembamba kilianza kunitoka.

“Changudoa?” niliuliza nikiwa ni kama siamini.

“Ndiyo, hawa wasichana wa siku hizi mchana ukimuona utadhani mtu wa maana kweli, ngoja giza liingie,” alizidi kushindilia msumari mama mwenye nyumba.

Hata sikumbuki tuliagana naye vipi, nilikuja kujikuta nimekaa sebuleni nikiwa nimejikunyata, mawazo tele yakipita ndani ya kichwa changu.

Pamoja na ujanja wangu wote, hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa kama kutoka na machanguoa, kibaya zaidi ni kwamba nilipokutana na Khazija nilikuwa nimeuza mechi. Niliingia mzimamzima bila tahadhari yoyote.

Kama umewahi kupiga gemu na mtu halafu baadaye ukaanza kuwa na hofu kuhusu usalama wako, unaweza kuelewa ni hofu kiasi gani niliyokuwa nayo. Nilibaki nikiwa nimejikunyata kwa muda mrefu, yaani nimekaa tu! Sitazami runinga wala sisikilizi redio, muda wote natetemeka tu.

Mpaka inafika saa saba za usiku, nilikuwa nimekaa tu pale sebuleni, mawazo mengi yakiendelea kukisumbua kichwa changu. Nilikuwa nikipiga picha jinsi nitakavyokonda, jinsi nitakavyokuwa nakohoa na kutokwa na madonda mwili mzima. Hakika yajayo yalikuwa yakitisha.

Hata sijui nilipitiwa na usingizi saa ngapi, nilipokuja kuzinduka ilikuwa ni tayari saa kumi na mbili alfajiri na kilichoniamsha ni baada ya kusikia mlango wa geti ukifunguliwa, nikakurupuka na kusogea dirishani, nikawa nachungulia nje.

Kweli alikuwa ni Khazija, alikuwa akitembea kwa kuyumbayumba, mkononi akiwa ameshika chupa ya pombe kali. Nilimuona mama mwenye nyumba akipita haraka na kurudi kwake, Khazija akawa anahangaika kufungua mlango wa chumba chake.

“Kwa nini umeniua Khazija? Kwa nini? Why?” nilijikuta nikijisemea huku machozi yakianza kunitoka, donge kubwa lilinikaba kooni, machozi yakawa yanamwagika kwa wingi na kuulowanisha uso wangu.

Niliona kama nitaendelea kukaa ndani naweza hata kuchukua uamuzi wa kujidhuru, nikaona bora nijiandae na kwenda kazini labda kidogo nitachangamka. Basi nilitoka na kwenda bafuni kinyonge, nikajimwagia maji huku nikiendelea kuumia mno ndani ya moyo wangu.

Nilijikuta namchukia sana Khazija na nikajiapiza atakapokuja kunishibokea tena, naweza hata kumtia makofi.

Nilirudi ndani na kujiandaa, muda mfupi baadaye nikatoka kimyakimya, sikutaka hata mtu yeyote anione, nafsi yangu ilikuwa inanisuta mno na nikiri kwamba sijawahi kuwa kwenye majuto kwenye moyo wangu kama kuanzia nilipopewa taarifa kwamba Khazija ni changudoa.

Kwa kawaida kila ninapoondoka kwenda kazini nawasalimu majirani zangu, washkaji na watu wote ninaowafahamu lakini siku hiyo tangu natoka ndani mpaka nafika kituoni, sikuwa nimemsemesha mtu yeyote, muda wote nilikuwa natembea huku nimeinamisha kichwa chini, machozi yakinilengalenga.

Hakuna kitu nilichokuwa nakiogopa kama kufa kwa Ukimwi, nikawa natamani kila kilichotokea kiwe ndoto. Nilijuta kumfahamu Khazija na kubwa zaidi nilijuta mno kumvamia mtu nisiyemjua, tena bila kutumia kinga.

nilipofika kazini, ilibidi kwanza nitafute sehemu na kutulia kabla sijapanda ngazi kuelekea juu ofisini, kwa sababu nilikuwa na hali mbaya sana. Nilinunua maji na kunawa usoni ili hata mtu akinitazama asijue kwamba nilikuwa nalia.

Baada ya kuhakikisha nipo sawa, nilipanda ngazi mpaka juu, mtu wa kwanza kukutana naye alikuwa ni Salma wa mapokezi. Aliponiona tu, aliacha kila kitu alichokuwa anafanya, akanikimbilia na kunikumbatia kwa nguvu huku akinibusu shingoni.

“Kwa nini hupatikani hewani? Halafu hata ukiwa unapatikana mbona unakuwa mzito kupokea simu zangu?” Salma aliniuliza kwa sauti ya chini iliyojaa mahaba na upole, tofauti kabisa na jinsi alivyokuwa siku zote.

“Bado naumwa, nimejikaza tu kuja kazini!”

“Ooh! Maskini pole, hata uso wako unaonesha unaumwa,” alisema huku akiniachia, mwili wangu wote ukabaki na harufu ya pafyumu aliyokuwa amejipulizia. Sikuzungumza naye mambo mengi, nikapita na kwenda ofisini kwangu.

Bado kazi nilizoziacha zilikuwa palepale, kompyuta kadhaa zilizokuwa zinahitaji marekebisho, simu za ofisi na vifaa vya kuunganishia intaneti, vyote vilikuwa vinanisubiri. Nikaweka begi langu sehemu yake na kuchukua vifaa vyangu vya kazi. Niliamua kuelekeza nguvu kwenye kazi nikiamini nitasahau majanga niliyokuwa nayo.

Niliifungua kompyuta ya kwanza na kuanza kuitengeneza, nilibadilisha ‘hard drive’ na kuweka nyingine mpya, nikarekebisha na vitu vingine muhimu kisha nikaichomeka kwenye umeme, nikaiwasha lakini haikuwaka.

Nilirudia kuikagua tena na tena, nikarekebisha kila nilichokuwa nadhani ndiyo tatizo lakini kila nilipokuwa naiwasha, bado ilikuwa ikigoma. Nikaachana nayo na kuanza kuitengeneza nyingine, nayo nikarekebisha kila kitu lakini nilipoiwasha, haikuwa ikiwaka.

Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kichwa changu hakipo sawa kwa sababu kwa jinsi nilivyobobea kwenye masuala ya teknolojia ya mawasiliano, hata kama kompyuta ni mbovu kiasi gani, ikishafika kwangu lazima itapona. Nilivyoona kompyuta zote mbili zimenishinda, niliamua kuachana nazo, nikawa nafanya kazi nyingine.

Niliingia kwenye website ya kampuni na kuanza kukagua baadhi ya mambo kama ilivyokuwa kawaida yangu, vitu vingi havikuwa sawa na kila nilichokigusa kwa lengo la kurekebisha, nilijikuta nazidi kuharibu, nikaamua kuachana nayo.

“Sasa nitafanya kazi gani leo?” nikiwa nado najiuliza, simu ya mezani iliita. Nilipoipokea alikuwa ni Salma, akaniambia bosi ananiita ofisini kwake, nilishusha pumzi ndefu na kujifuta jasho, nikaacha kila kitu na kwenda mpaka ofisini kwa Madam Bella.

Nilipofungua mlango tu, aliacha kila alichokuwa anakifanya na kusimama, akaja mbiombio na kunikumbatia kwa mahaba, tukagusanisha ndimi zetu huku mikono yake ikifanya utalii wa ndani kwenye maeneo mbalimbali ya mwili wangu.

“Nimekumiss jamani mume wangu,” alisema baada ya kuniachia, akanibusu tena na kunikaribisha kiti.

“Mbona umepooza namna hiyo, tatizo nini?” alisema Madam Bella huku akinikazia macho, nikamuungia humohumo kwamba nilikuwa naumwa sana na kwamba nimejilazimisha kuja kazini.

“Pole mume wangu, nakuona kabisa hauna furaha! Basi we nenda tu kapumzike, tutawasiliana baadaye, nikitoka naweza kuja kukuona nyumbani mgonjwa,” alisema Madam Bella, akanibusu mdomoni na kuifuata pochi yake. Alitoa noti tano za shilingi elfu kumikumi na kuniwekea kwenye mfuko wa shati, akanibusu tena.

Nilimshukuru na kutoka, nikaenda ofisini kwangu na harakaharaka nilichukua begi langu na kutoka mpaka mapokezi. Nikamuaga Salma ambaye alibaki ananishangaa.

“Naenda hospitali, nisije nikakufia bure,” nilimtania, akacheka na kunibusu kwa mbali, nikateremka kwenye ngazi na muda mfupi baadaye nilikuwa nimeshafika chini.

“Ebwana kuna mgeni wako anakutafuta kwelikweli.”

“Nani?”

“Yule dada uliyekuwa naye siku ile mkakaa pale, anasema hupatikani hewani kila akikupigia,” alisema mlinzi.

“Dah! Yuko wapi kwani?”

“Yule amekaa pale mlipokuwa mmekaa siku ile, tena naona amekuona maana anasimama,” alisema mlinzi, nikageukia kule alikokuwa ananionesha. Alikuwa ni Nancy, nilimfuata na kuzungumza naye juujuu, nikamwambia naumwa sana na naenda hospitali.

Kwa jinsi uso wangu ulivyobadilika, kweli aliamini naumwa, akataka anisindikize lakini nilimkatalia, nikaondoka huku akionesha wazi kwamba hakufurahishwa na nilichokifanya. Niliingia kwenye Bajaj na kumuelekeza dereva sehemu ya kunipeleka.

“Nipeleke Muhimbili.”

“Hospitali au?”

“Ndiyo,” nilisema huku nikishusha pumzi ndefu. Niliamua liwalo na liwe, lazima nikapime nijue mbivu na mbichi.

Basi tulielekea mpaka Muhimbili, kwa kuwa sikuwa nimewahi kwenda kupima ‘ngoma’ sehemu yoyote, hata sikuwa najua utaratibu ukoje, ikabidi niende mpaka kwenye jengo la ‘emergency’.

“Samahani nesi, naomba kuuliza.”

“Bila samahani, halafu wewe kama nakujua vile? Wewe si unaitwaa... unaitwaa...” alisema nesi niliyemsimamisha na kutaka kumuuliza kuhusu taratibu za kupima Virusi vya Ukimwi, akawa anajaribu kunikumbuka jina langu.

Kiukweli sikuwa namjua na sikukumbuka kama nimewahi kukutana naye mahali, basi akawa anahangaika kukumbuka jina langu. Alinikata sana ‘stimu’ kuniambia kwamba ananijua kwa sababu kama alikuwa ananijua, hata nitakapomueleza kilichonipeleka pale maana yake lazima atafuatilia majibu kutaka kujua kama ninao au la!

“Sasa akijua kama ninao si atanitangaza huyu?” nilikuwa nikijiuliza huku nikimtazama machoni akijaribu kukumbuka jina langu.

“Baada ya kuona ameshindwa kabisa kunikumbuka, aliniuliza swali ambalo lilinifanya niamini kama kweli ananijua.

“Si unaishi Tandale wewe?”

“Ndiyo.”

“Unamfahamu Jemima?”

“Aah! Jemima tena, nitaachaje kumfahamu mke wangu wa zamani?”

“Kwani mlishaachana? Mimi naitwa Penny, rafiki yake Jemima.”

“Aah! Unajua tena pilikapilika za maisha zinatutenganisha,” nilibabaika kwa sababu ukweli ni kwamba Jemima alikuwa miongoni mwa wasichana ambao nilivunja sana mioyo yao.

Huyu alikuwa mpenzi wangu wa kwanzakwanza wakati natoka chuo na kuyaanza maisha ya kujitegemea na huyu nesi aliyekuwa amesimama mbele yangu, sasa nilikuwa nimemkumbuka.

Alikuwa rafiki yake mkubwa Jemima, kipindi hicho wote wawili wakiwa wanasomea unesi na kuna siku aliwahi kuja naye nyumbani kwangu usiku na kumtambulisha kwangu. Sikuweza kumkumbuka kwa sababu kwanza siku hiyo nilikuwa nimelewa sana.

“Umeacha pombe siku hizi?”

“Nimeacha, mimi na pombe wapi na wapi?”

“Lakini mbona kama umekonda na kuchakaa kiasi hicho? Kwani unaishi na nani siku hizi?” alizidi kunidadisi maswali yaliyozidi kunichanganya kichwa.

“Eh! Mpaka nimesahau kama unataka kuniuliza kitu naona nimenogewa kukuuliza maswali. Ulikuwa unasemaje shemeji yangu wa zamani? Kwa nini lakini umeachana na Jemima?” aliniuliza huku bado akiendelea kupachika swali juu ya swali.

INAENDELEA

Powered by Blogger.