KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo: Mwajuma Utamu Sehemu Ya Kumi Na tatu (13)


Vyombo vya habari navyo havikuwa mbali, viliendelea kuripoti taarifa za muuaji huyo ambaye alisumbua sana na mpaka kufikia wakati huo hakukuwa na dalili zozote za kupatikana kwake.


Kipindi hicho ukurasa wangu ya Mwajuma Utamu ulikuwa umefikisha wafuatiliaji 500,000. Ulikuwa ni ukurasa ambao baadae niliutumia kwa kuwauza machangudoa wengine.

Suzie huyu alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu lakini pia alikuwa ni changudoa, alikuwa akiishi hostel. Nilifahamiana naye kipindi ambapo tetesi za jini mweusi zilivuma.
Suzie alipofahamu nimepata mwanaume tajiri ambaye alininunulia gari pamoja na nyumba ya kifahari maeneo ya Msasani, hakutaka kuamini, alionekana kunishangaa kupita kawaida.
Kwa jinsi alivyokuwa akiniangalia usoni, macho yake yalionyesha kuniuliza kwanini niliendelea kufanya biashara ya uchangudoa wakati nilipata mwanaume ambaye alikuwa na pesa na tayari alinifanyia mambo makubwa katika maisha yangu. Kama tatizo ni biashara alinifungulia tena zaidi ya moja.
“Kwanini usitulie tu na Martin, anaonekana kweli nakupenda?” aliniuliza Suzie.
“Hapana siwezi,” nilimjibu
“Kwanini au hujampenda?”
“Sijazoea kuwa na mwanaume mmoja katika maisha yangu, nisipofanya mapenzi na wanaume zaidi ya wawili najiona kama sijakamilika.”
“Jitahidi kwa Martin, anaonekana kuwa mtu mwema kwako.”
“Nitatulia lakini sio sasa, acha niendelee na uchangudoa wangu mpaka pale nitakaposema basi.”
“Sawa ila kuwa makini maana siku akigundua kuwa wewe ni changudoa nadhani huo ndiyo unaweza kuwa mwisho wa mahusiano yenu.”
“Hilo haliwezi kutokea na hata kama likitokea siogopi kitu kwanza nishamchuna sana,” nilimwambia.

Urafiki wangu na Suzie uliendelea kila siku, nilimshauri ajipige picha za utupu kisha nikamuweka katika ukurasa wangu, huko nilimtafutia wateja, nikamuunganisha nao, safari ya kupiga pesa mitandaoni ikaendelea.
Nilifanya mambo yote hayo lakini Martin Sepeku hakufahamu kilichokuwa kikiendelea, alikuwa ni mtu wa kusafiri mara kwa mara. Safari zake nyingi zilikuwa ni za nje ya nchi hivyo ilikuwa ni vigumu kugundua lolote.
“Nataka kukuoa Mwajuma uwe mke wangu kabisa,” aliniambia Martin siku moja kabla ya safari yake ya kwenda Dubai.
“Unafikiri itawezekana?” nilimuuliza.
“Kwanini isiwezekane kwani ugumu uko wapi?”
“Dini.”
“Dini sio tatizo mpenzi wangu ninachokitaka ni kufunga ndoa na wewe, nakupenda sana Mwajuma.”
“Nakupenda pia Martin lakini….”
“Nipo tayari kubadilisha dini kwasababu yako, nikirudi kutoka Dubai nataka nihalalishe mahusiano yetu au hupendi kuona siku nakuwa baba wa watoto wako na wewe unakuwa mama wa wanangu?”
“Napenda.”
“Basi nikubalie hili litimie kwanza.”
“Sawa litatimia,” nilimjibu.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Kichwa kilianza kuniuma baada ya kumsikia Martin alihitaji kufunga ndoa na mimi kipindi atakaporudi kutoka safari yake ya Dubai. Kiukweli sikuwa nimejipanga katika hilo wala moyoni mwangu sikuwa nina mapenzi ya dhati na Martin.

Nilichokuwa nimekifuata kwake ni pesa pamoja na mali alizonimilikisha. Suala la kufunga ndoa nililiona kuwa gumu hasa kwa mtu kama Martin ambaye sikumpenda kutoka moyoni mwangu.
Nilipomueleza Suzie habari hizo alionekana kufurahi, aliniambia nisikubali nafasi hiyo ipotee, alienda mbali zaidi na kuniambia kama angekuwa ni yeye angekubali tena bila kipingamizi chochote.

“Ungekubali?” nilimuuliza.
“Ndiyo mimi ningekubali shoga yangu, embu angalia jinsi maisha yalivyokuwa magumu, angalia tunavyoteseka katika biashara hii, wakati mwingine tunakutana na wanaume wenye maumbile makubwa, kwasababu tunahitaji pesa tunakubali kufanya nao mapenzi, tunapata maumivu makali sana, hivi hii biashara tutaifanya mpaka lini?” aliniuliza Suzie kwa uchungu kisha akaendelea.
“Kama huyo mwanaume anakupenda na ana malengo na wewe naomba utulie naye, hii biashara ni bora ukaachana nayo tu,”aliniambia.
Maneno ya Suzie yalianza kuniingia, niliyatafakari na kuona kuwa yalikuwa na ukweli mtupu lakini tatizo lilikuja sehemu moja, sikumpenda Martin kutoka moyoni mwangu, kwake nilifuata pesa na maslahi mengine ambayo nilikuwa tayari nimeshayapata.
Nilipoona Suzie ananig’ang’aniza nikubali kuolewa na Martin ilibidi nilimueleze ukweli kuwa sikumpenda kama alivyokuwa akiamini, nilimpendea pesa zake na hiyo ndiyo ilikuwa tamaa yangu.


Suzie aliendelea kunishauri nikubali kuolewa na Martin kwasababu alikuwa na pesa na pia alionekana kuwa na malengo na mimi, hakutaka kuona nikiipoteza bahati hiyo. Kwake ulionekana kuwa kama wimbo wa taifa.
“Hata kama humpendi lakini angalia jinsi alivyojitoa kwako hivi ni mwanaume gani ambaye anaweza akakubali kufanya mambo yote hayo hata kama anakupenda?”
“Usiuzungumzie moyo wangu Suzie, nimeshakwambia kuwa simpendi Martin mbona hunielewi na sioni sababu ya kuolewa naye.”
“Mwajuma unajua unaichezea bahati, wasichana wengi wanaitafuta bahati hiyo wanaikosa halafu wewe unaipata lakini unaichezea.”
“Suzie hivi hakuna stori zingine za kuzungumza?”
“Utakuja kuijutia bahati hii unayoichezea.”
“Sidhani kama kuna siku nitakuja kuijutia, kwanza hilo haliwezi kutokea halafu nimekumbuka baadae ninatakiwa nikameet na Damian.”
“Who is Damian?” (Damian ndiyo nani?)
“Mpenzi wangu, mume wangu mtarajiwa,” nilimjibu.
Suzie alibaki akinishangaa baada ya kumwambia nilikuwa katika mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine aliyejulikana kwa jina la Damian.
Hii ilionyesha picha ya umalaya, yaani sikutulia na mwanaume mmoja, maisha yangu yalikuwa ni ya kudangadanga leo nilikuwa kwa mwanaume huyu kesho nilikuwa kwa mwanaume mwingine.
Huyu Damian nilikutana naye kwenye klabu moja iliyojulikana kwa jina la La Charz ambayo ipo Sinza Mori.CHANZO : http://deusdeditmahunda.blogspot.com/
Mahusiano yetu yalianza mara baada ya kunichukua usiku mmoja na kwenda kufanya naye mapenzi nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Beach.
Alikuwa ni mwanaume mwenye uwezo mkubwa wakati wa kufanya mapenzi, ingawa nilishawahi kujiapiza kuwa sintokuja kujihusisha na mahusiano na mwanaume aliyenichukua kwa lengo la kwenda kufanya mapenzi lakini kwa Damian ilikuwa tofauti na kiapo hicho, nilijikuta nikianzisha mahusiano naye ya kimapenzi bila kutarajia.

Baada ya kupita kipindi fulani penzi likawa tayari limeota mizizi, nilikuwa sisikii wala sioni kwa Damian, wakati huo nilikuwa tayari nipo katika mahusiano na Martin.
Hata hivyo sikuacha biashara ya uchangudoa mitandaoni, niliendelea nayo kama kawaida.
Nilipomwambia Suzie kuwa nilikuwa katika mahusiano na Damian alionekana kunishangaa sana, alihitaji kumfahamu mwanaume huyo zaidi na hata nilipomwambia maisha yake alimuona kuwa wa kawaida sana.


ITAENDELEA

Powered by Blogger.