KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Kivuruge Wa Tandale Sehemu Ya Ishirini na moja (21)

hadithi nzuri ya kivuruge wa tandale
Usingeweza kuamini kwamba ndiyo mimi ambaye siku moja iliyopita nilikuwa nahaha, nikiwa nimekata tamaa kabisa na kuamini kwamba tayari nilikuwa nimenasa ‘ngoma’, kweli akili ya binadamu ina uwezo wa kusahau jambo kwa haraka sana.

“Umejisikiaje kulala na mimi mpaka asubuhi?”

“Nimejisikia poa sana, lakini naomba nikuulize, kwani jana hukwenda kazini?”

“Sikwenda kwa sababu nimeshamaliza shift yangu ya usiku, wiki yote hii nitakuwa naingia mchana,” alisema huku akijinyoosha, akaamka na kujifunga upande wa khanga, akaendelea kujinyoosha huku akipiga miayo.

Nilishindwa kuvumilia kumuona katika hali ile, nikamvutia kwangu na muda mfupi baadaye, tulikuwa uwanjani, tukapelekeshana puta na japokuwa asubuhi ile kulikuwa na kaubaridi fulani, wote wawili tulijikuta tukitokwa na kijasho chembamba.

Baada ya hapo, nilijikuta nikilala tena, nilipokuja kushtuka tayari ilikuwa ni kama saa tatu hivi za asubuhi. Haikuwa kawaida yangu kuchelewa kuamka kiasi hicho kwa sababu siku zote saa kumi na mbili nakuwa nimeshaamka lakini siku hiyo mpaka saa tatu asubuhi! Haikuwa kawaida yangu.

Nilipoamka, yeye hakuwepo pembeni yangu, nadhani alishaamka na kwenda kwake, basi nikatoka nikiwa na mswaki wangu, kiunoni nikiwa nimejifunga taulo, ile natoka tu nikakutana uso kwa uso na mama mwenye nyumba, akanikata jicho mpaka nikawa najiuliza ‘nimemkosea nini huyu mama?’.

Nilimsalimu lakini hakunijibu, nikaenda mpaka bafuni huku nikijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu. Nilioga na angalau mwili ukapata nguvu, wakati natoka, nilikutana na baba mwenye nyumba ambaye kimsingi huwa tunaheshimiana sana na hakuwepo hapo nyumbani kwa muda kwa sababu yeye ni mtu wa kusafirisafiri sana.

Alinichangamkia vizuri na nadhani alirudi usiku maana bado alionesha kuwa mchovu, basi nikaingia zangu ndani huku moyoni nikijisikia kuwa na hatia sana, nikawa najiuliza siku akigundua kwamba akiwa hayupo natia mkono kwenye chungu chake cha asali itakuwaje?

Akili nyingine ikawa inaniambia kwamba eti mimi sina kosa kwa sababu mkewe ananishobokea mwenyewe. Basi nilipoingia ndani tu, mara nilisikia mlango ukifunguliwa, kutazama alikuwa ni Khazija, mkononi akiwa na chupa ya chai na sahani ya vitafunwa, nikamkaribisha akaingia mpaka ndani.

Aliandaa chai, tukakaa na kuanza kunywa huku tukipiga stori za hapa na pale, nikajikuta nikizidi kumpenda. Tulipomaliza kunywa chai, Khazija alinisaidia kufanya usafi mle ndani kwangu kwa sababu huwa sina kawaida ya kufanya usafi mara kwa mara.

Nyumba ikabadilika na kuanza kuwa na hadhi katika suala zima la usafi, alitoka na kwenda kwake akiwa amebeba vile vyombo, muda mfupi baadaye akarudi akiwa na kitezo kilichokuwa na mkaa, akafungua kikopo kidogo kilichokuwa na udi maalum nasikia kutoa Uarabuni, akauweka juu ya mkaa kwenye kitezo na kufukiza chumba kizima, harufu ikabadilika.

Kiukweli sikuwa nimeyazoea kabisa mambo hayo, kwa kifupi mimi nimekulia bara na huko kwetu mambo kama hayo hayapo kabisa! Nimewahi kusikia kwamba maeneo kama Tanga, Pemba na Mombasa ndiyo kwenye mambo hayo ya kufukiza nyumba nzima marashi, ukiingia utadhani upo kwenye dunia nyingine ya tofauti.

Basi tulishinda na Khazija mpaka majira ya kama saa saba hivi ambapo aliniaga kwamba anaenda kazini, lakini tayari alikuwa ameshaniandalia chakula na kuniwekea kwenye ‘pot’, kabla hajaondoka tukaingia tena uwanjani ‘kuagana’ ambapo kama kawaida yake, alinitoa jasho kisawasawa.

Alipoondoka kwenda kujiandaa, nilijikuta nikitamani kwenda ndani kulala, nikainuka kichovu na kuingia chumbani, nilipojitupa kitandani, sikuamka mpaka ilipofika majira ya kama saa kumi na moja jioni na kilichoniamsha, ilikuwa ni njaa.

Haikuwa kawaida yangu kulala hovyo kiasi hicho, basi nikaamka na kwenda tena bafuni kuoga, nikakutana tena na mama mwenye nyumba lakini safari hii alikuwa amekaa na mumewe kwenye jamvi pale uani wakicheza karata.

Japokuwa alikuwa na mumewe lakini bado nilimuona akinitazama kwa macho yaliyobeba ujumbe wa mahaba mazito ingawa ilionesha wazi kwamba moto mkali wa wivu ulikuwa ukikiunguza kifua chake.

Nilioga na kurudi ndani harakaharaka, nikakaa na kuanza kuufakamia msosi alioniandalia Khazija. Nilichokigundua hata aina yake ya upishi ilikuwa tofauti kabisa kwani chakula kilikuwa kimewekwa viungo vilivyokifanya kiwe kizuri sana, nikajikuta nazidi kumpenda Khazija.

Ni mpaka nilipomaliza kula ndipo nilipoishika simu yangu na kuiwasha maana tangu jana yake nilikuwa nimeizima, meseji mfululizo zikaanza kumiminika. Nyingi zilikuwa ni za kutoka kwa bosi wangu, Madam Bella ambaye alikuwa akitaka kujua naendeleaje pamoja na meseji nyingine za kimapenzi.

Lakini pia zilikuwepo meseji za kutoka kwa Ruqaiya naye akitaka kujua naendeleaje, zilikuwepo nyingine kutoka kwa Nancy na kwa Salma, basi ilikuwa tafrani. Ndani ya muda mfupi tu simu yangu ilikuwa imeingia meseji karibu thelathini na muda huohuo ilianza kupigwa.

Wa kwanza alikuwa ni Ruqaiya ambapo nilipoona namba yake tu, uso wangu ulijawa tabasamu, nikapokea yake ambapo kitu cha kwanza alianza kunilaumu eti kwa nini namuweka roho juu kiasi hicho, meseji sijibu na simu haipatikani wakati naumwa. Kwa jinsi alivyokua akilalama kwa hisia nzito, nilijikuta nikitamani nimuone ili kama ni kunilaumu, anilaumu nikiwa namuona.

Kabla hata sijasema chochote, alianza mwenyewe kwa kuniambia kwamba anahitaji sana kuonana na mimi, nimuelekeze mahali popote alipo atanifuata. Nilijua nikisema nimlete nyumbani, naweza kugonganisha ‘magari’, nikamwambia nitajitahidi anikute Magomeni Kanisani, akaniambia anakuja muda si mrefu.

Nilipomaliza tu kuzungumza na simu, mara nilisikia mlango ukigongwa, niliinuka na kwenda kufungua, katika hali ambayo sikuitegemea, nilikutana uso kwa uso na Madam Bella ambaye naye alionesha kama amekuja akiwa na manung’uniko yake moyoni kwamba kwa nini sijamjibu meseji na hewani sipatikani, akaingia na kwenda kitandani moja kwa moja.







“Kwa nini unakuwa Mswahili kiasi hicho,” Madam Bella alianza kuwaka huku akisaula viwalo vyake, kimoja baada ya kingine. Sikutaka kuwa na maneno mengi kwani niliamini kwa shoo atakayoipata, mwenyewe atatulia na kunisamehe yote.

Nilimsogelea na kujifanya bado naumwa sana, akanidaka mzimamzima na kunivutia kwake, akanimwagia mvua ya mabusu huku akiniambia kwamba hapendi tabia yangu ya kutokuwa napokea simu anaponipigia.

Nilimdanganya kwamba nakunywa dawa kali sana kiasi kwamba nikishameza tu, napitiwa na usingizi ndiyo maana hata simu ikiita siisikii. Uongo huo ulionekana kumuingia kisawasawa, akanipa pole na kuniambia kwamba hata kama naumwa, anataka ‘nimvuruge’.

Tayari mwenzangu alishaonesha injini imeshachanganya, kilichotakiwa ni kuingiza gia namba moja ili safari ianze. Hata hivyo, tofauti kabisa na siku zote, kuna hali isiyokuwa ya kawaida ilikuwa inanitokea. ‘Mkuu wa kaya’ ni kama hakuwa na habari kabisa juu ya kilichokuwa kinataka kuendelea kwani hakuonesha ushirikiano kabisa.

Jambo hilo pia lilimshtua Madam Bella, ikabidi ajaribu kutumia mbinu zake ili kumrudisha mchezoni lakini ilikuwa ni kazi bure, aligoma kabisa.

“Una nini wewe?”

“Hata mimi sielewi.”

“Ulikuwa namwanamke humu ndani si ndiyo?”

“Mimiii?”

“Wewe ndiyo, kwa nini iwe hivi wakati mimi nakujua wewe ni mwanaume wa shoka?”

“Labda ni kwa sababu ya dawa ninazokunywa, wala usiwe na wasiwasi mambo yatakuwa mazuri.”

“Mambo yatakuwa mazuri saa ngapi bwana?” alisema huku akimvamia tena mkuu wa kaya na kujaribu kumfanyia kukurukakara lakini wapi... alikuwa amelala fofofo.

Kwa mara ya kwanza niliyaona machozi ya Madam Bella, alilia kwa uchungu, alinilaumu sana kwa kumfanyia ukatili wa kiasi kile, alilalama mpaka nikatamani nifanye kitu ili kumridhisha lakini sikuwa na namna.

Basi niliendelea kujitetea kwamba ni kwa sababu ya dawa lakini moyoni nilikuwa najua kilichotokea. Ni kweli muda mfupi uliopita nilikuwa na Khazija na kiukweli ni kwamba alinishughulisha sana, sasa nikawa nahisi pengine hali ile ndiyo iliyosababisha gari lishindwe kuwaka.

Madam Bella alisusa na kugeukia ukutani, akajilaza huku akiwa hataki kabisa kuzungumza na mimi. Mara simu yangu ilianza kuita, harakaharaka nikaichukua na kutazama namba ya mpigaji, alikuwa ni Ruqaiya na nadhani alikuwa akitaka kujua nimefikia wapi kama tulivyokubaliana.

Kiukweli sikuweza kuipokea, nilibonyeza kitufe cha kutoa mlio, nikaiacha iite mpaka ilipokata. Mara meseji ikaingia; Leo nimejiandaa kikamilifu, nimekunywa bakuli la supu ya pweza kwa ajili yako, kazi ni kwako!

Nilijikuta nikizidi kuchanganyikiwa, nikashusha pumzi ndefu na kuitoa simu mlio, nikaiweka chini ya mto na kuanza kutafakari ndani ya kichwa changu nini cha kufanya. Mara nilipata wazo la kutoka na kwenda dukani kwa Mangi ‘kubusti’ kama kawaida yangu.

“Naenda dukani mara moja, nikuletee nini?”

“Sitaki chochote,” madam Bella hakujibu chochote, nikajua kazi ninayo. Basi harakaharaka nilitoka na kwenda kwa Mangi, nikaagiza kinywaji ninachopenda kukitumia ili ‘kubusti’ mambo yetu yale, nikachukua na tangawizi, nikaitafuna nzimanzima mpaka machozi na kamasi vikawa vinanitoka.

Nilipojiona niko fiti, nilirudi nyumbani fasta, nikamkuta Madam Bella kajiweka kihasara pale juu ya kitanda, sikusubiri kuuliza, nikamvamia mzimamzima, ile kupiga ‘stata’ jino moja, gari likawaka.

Madam Bella naye hakutaka stori, alikamata kisawasawa na kuanza kuukwea mnazi kwa pupa huku akiendelea kunililia eti kwa sababu gani namnyanyasa. Sikumjibu chochote zaidi ya kuendelea kupiga mashuti ya mbali, akawa anatoa miguno ya hapa na pale iliyonizidisha munkari.

Hakuchukua raundi, akatangaza kuangua madafu mawili kwa mpigo, akanikamata kwa nguvu utafikiri tupo kwenye ule mchezo unaopendwa sana wa miereka. Aliponiachia, alijitupa pembeni kama mzigo na muda mfupi baadaye, alikuwa akikoroma.

Licha ya kufanikiwa kuitii kiu yake, bado nilikuwa na maswali mengi ndani ya kichwa changu juu ya kilichotokea, kwa nini hali kama ile inikumbe wakati haijawahi kunitokea hata mara moja? Mara nilisikia mlango ukigongwa, harakaharaka nikaamka na kwenda kuchungulia.

Mapigo yangu ya moyo yalishtuka mno baada ya kugundua kwamba alikuwa ni Khazija, mkononi akiwa na kisinia kidogo ambacho juu yake kilikuw ana glasi mbili za juisi. Kwa jinsi ilivyoonesha, moja ilikuwa yake na nyingine yangu, nikawa natetemeka nitafanyaje ili anielewe?

Basi nilijikaza kiume huku nikijiambia kuwa liwalo na liwe, nikafungua mlango. Nilitaka kuanza kumpanga Khazija lakini katika hali ambayo hata sikuitegemea, alinikatisha na kuniambia eti nisijali, anajua kwamba niko na mgeni na ndiyo maana ameniletea juisi glasi mbili.

Mwanzo nilikuwa nimetoa kichwa tu lakini mshangao ulinifanya niuachie mlango, akalitazama tauli nililokuwa nimelivaa huku akililazimisha tabasamu kwenye uso wake, akanikabidhi ule mzigo na kuondoka zake. Kiukweli nilijisikia vibaya kuliko kawaida, niliyahisi maumivu aliyoyapata Khazija kwenye moyo wangu.

Nilirudi ndani na kufunga mlango, nikaweka zile glasi mbili za juisi mezani, nikawasha runinga na kukaa, muda mfupi baadaye Madam Bella alitoka na kuja pale nilipokuwa nimekaa.

“Whaoo, umejuaje kama nahitaji juisi,” alisema huku akikaa na kuichukua glasi moja ya juisi, akaigida na alipoishusha chini, ilikuwa nusu. Nikazidi kujisikia vibaya ndani ya moyo wangu.

Basi tuliendelea na stori za hapa na pale, Madam Bella akaniambia kwamba alikuja mara moja kunijulia hali lakini ana ratiba ngumu siku hiyo, akanishukuru na kuniomba radhi eti kama alikuwa amenikwaza katika mazungumzo yake.

Moyoni nilikuwa nataka aondoke tu, basi nikawa najichekesha pale, akaenda kuoga na aliporudi, alivaa na kunitaka nimsindikize. Kabla hajatoka, alitoa bahasha iliyokuwa na noti kadhaa za shilingi elfu kumikumi na kuniambia eti hizo ni kwa ajili ya juisi ya mgonjwa.

Nilimsindikiza mpaka mahali alipokuwa amepaki gari lake, akaingia na kunitaka na mimi pia niingie na kukaa upande wa pili, tukawa tunapiga stori za hapa na pale na katika mazungumzo yake, aliniambia jambo ambalo lilinishtua sana.

Aliniambia eti anataka nimuoe ili awe mke wangu halali, amechoka kuishi kwa kuibia penzi langu wakati anaamini nampenda sana na yeye ananipenda sana, akaniambia nilifikirie hilo kisha tutaonana kesho yake.

Alinibusu kimahaba mdomoni kisha nikateremka, nikamsaidia kumuongoza kutoa gari na muda mfupi baadaye, aliondoka huku akinipungia mkono. Nilirudi haraka mpaka nyumbani kwangu na kabla sijaingia, nilienda kumgongea Khazija, akafungua mlango kidogo na kuchungulia.

“Unasemaje?” aliniuliza huku akionesha kutokuwa tayari kuzungumza na mimi.

“Samahani naomba tuongee Khazija,” nilimwambia, akajifikiria kwa zaidi ya dakika nzima kisha akashusha pumzi ndefu na kufungua mlango, lakini akawa anakwepa nisimuangalie usoni.

Na mimi niliendelea kukazania kumuangalia usoni huku nikimsemesha, aliponitazama, nilijikuta nikimuonea huruma kupita kiasi, macho yake yalikuwa yamebadilika rangi na kuwa mekundu sana kuonesha kwamba kumbe alikuwa analia, nikamsogelea na kutaka kumkumbatia lakini alikataa, nikatumia nguvu na kumkumbatia hivyohivyo, na yeye akanikumbatia huku akianza upya kuangua kilio.


“Kwa nini unanifanyia hivi lakini?”

“Nisamehe Khazija.”

“Unanipenda?”

“Ndiyo nakupenda.”

“Malengo yako ni nini kwenye maisha yangu?”

“Nataka nikuoe, nataka uwe mke wangu, mama wa watoto wangu,” nilijikuta nikiropoka huku nikiendelea kumbembeleza Khazija ambaye nikiri wazi kwamba alishaanza kuniingia moyoni.

Basi tulibembelezana pale kwa muda mrefu na mwisho tukajikuta tukiishia juu ya kitanda kikubwa kilichokuwa ndani ya chumba cha Khazija. Miongoni mwa vitu ambavyo Khazija alikuwa ananipatia, ilikuwa ni kwenye suala zima la mbinu na medani za aina yake tuwapo kwenye uwanja wa fundi seremala.

Nililigundua hilo kwa sababu muda mfupi tu uliopita nilikuwa nimetoka kuchoshana nguvu na Madam Bella, tena gari likawaka kwa mbinde kwelikweli lakini kwa Khazija ilikuwa tofauti kabisa. Mpaka kipyenga cha mwisho kinalia kuashiria kumalizika kwa mpambano, nilikuwa hoi bin taaban.

Nakumbuka kwa mara ya kwanza, nilishindwa kusimama kutokana na jinsi miguu ilivyokuwa inatetemeka huku mwili ukiwa umeishiwa kabisa nguvu. Basi harakaharaka akanirudisha pale kitandani na kunichanganyia ‘glucose’ kwenye maji na kuninywesha, kisha glasi ya juisi ikafuatia.

Nikiwa nimeanza kurejewa na nguvu zangu, yeye aliamka na kuanza kuandaa maakuli huku akinipigisha stori za hapa na pale. Nilikuwa nimefanikiwa kabisa kumuondolea huzuni aliyokuwa nayo ndani ya moyo wake, akawa ananihimiza kwamba nisirudie tena kumuumiza.

“Unajua kwetu Pemba kuna uchawi wa kumfunga mwanaume, ukiendelea na mambo yako itabidi nikakufunge maana nakupenda na nataka uwe wangu peke yangu,” alisema huku akiendelea kukaangiza.

“Unakuwaje huo uchawi!”

“Ukichepuka tu gari haliwaki, hata ufanyeje ila ukirudi ndani mambo yanakuwa safi,” aliniambia, nikashtuka sana kwa sababu ni kweli hicho ndicho kilichotokea nilipokuwa na Madam Bella na kama nisingefanya juhudi za ziada, huenda ningedhalilika.

Japokuwa mwenyewe alikuwa akizungumza kama masihara, tena akicheka, kwangu mimi niliona ‘nimepatikana’. Basi tuliendelea na mazungumzo na baadaye msosi ulipokuwa tayari, aliandaa, tukakaa mezani tayari kwa kula.

Kabla sijaanza kula, alianza yeye kunilisha kisha akanibusu! Kiukweli Khazija alikuwa anajua sana kunidekeza kiasi kwamba mpaka chakula kinaisha, sikutamani kutoka kurudi kwangu. Nilishasahau kama nina ‘appointment’ na mtu muhimu sana, Ruqaiya.

Huwezi kuamini, tuliendelea ‘kubebishana’ na Khazija mpaka usiku na kilichokuja kunishtua ni baada ya kugundua kwamba sikuwa nimefunga mlango wangu.

Khazija naye alivyo mjanja, akaniambia nimuelekeze ataenda kufunga mwenyewe, kidume nikalainika, akaenda kufunga harakaharaka na muda mfupi baadaye alirejea akiwa na funguo zangu.

Kilichoendelea hata sikumbuki ni nini lakini nilipokuja kuzinduka, tayari kulikuwa kumepambazuka, nikiwa juu ya kitanda kimoja na Khazija, tukiwa tumejifunika shuka moja na msichana huyo mrembo ambaye kiumri alikuwa ‘saizi yangu’.

Waliosema kwamba mchovya asali hachovyi mara moja, hawakukosea. Kwa Khazija ni kama nilikuwa nimechovya asali, huwezi kuamini kwamba siku iliyofuatia sikuwa na habari na kazi wala simu yangu, nilishinda kutwa nzima nikiwa ndani na Khazija!

Naye alikudanganya kazini kwao kwamba anaumwa kwa hiyo muda pekee aliotoka ulikuwa ni wa kwenda kununua vitafunwa pamoja na mboga, baada ya hapo tulijifungia kutwa nzima ndani.

Jioni majira ya kama saa kumi na mbili, ilibidi nitoke nikaangalie kama ndani kwangu kulikuwa salama, nikamuacha Khazija akiwa amejilaza kitandani. Ile natoka tu, niligongana macho na mama mwenye nyumba, akaachia msonyo mmoja mkali sana.

“Kuna nini kwani mke wangu,” sauti ya mumewe aliyekuwa ndani ilisikika, nadhani alishtuka kumsikia mkewe akiachia msonyo, akamdanganya kwamba eti kuna kitu kilikuwa kimemkwaza huku akijifanya hana habari na mimi.

Sikumjali, nilienda mpaka mlangoni kwangu na kufungua, nikawasha redio na taa maana kigiza cha jioni kilishaanza kisha nikachukua ndoo ya maji kwa ajili ya kwenda kujimwagia ili kupunguza uchovu. Mama mwenye nyumba aliendelea kunikata jicho lakini nikawa najifanya kama vile simuoni.

Baada ya kumaliza kuoga, nilitoka bafuni na kuelekea ndani. Ile naingia tu, nilisikia rafiki yangu Ras akiniita kwa bashasha.

“Ulikuwa wapi mwanangu, nimekutafuta kinoma kuanzia asubuhi,” alisema rafiki yangu huyo ambaye huwa anashinda stendi, pale kwa Mtogole.

“Dah, naumwa mwanangu, nimeshinda hapahapa nyumbani, sijatoka kabisa.”

“Aunt, ingia,” alisema Ras huku akimuoneshea ishara mtu aliyekuwa amesimama koridoni, nikashtuka kugundua kwamba alikuwa amekuja na mtu. Nikiwa bado nang’aang’aa macho, nilishtukia Ruqaiya akitokezea, mshtuko nilioupata almanusra nidondoke.

“Ooh! Karibu sana mgeni, daah! Karibu sana,” nilisema kwa kujibaraguza huku uso ukiwa umenishuka. Ruqaiya hakunionesha bashasha kama nilivyozoea, nikazidi kupata hofu ndani ya moyo wangu.

Ili kuepusha ‘kuuza gazeti’, harakaharaka nilimkaribisha ndani, nikamshukuru sana Ras kwa kuniletea mgeni wangu, nikachukua shilingi elfu mbili pale mezani na kumkabidhi.

“Dah, inabidi umuombe radhi aunt maana amekutafuta kinoma, tangu saa nne asubuhi tunahangaika kukutafuta,” alisema Ras huku akiniaga, akanipa ‘tano’ kisha akaondoka zake, Ruqaiya akawa amekaa juu ya kiti huku akiwa amejiinamia.

Nilijihisi kuchanganyikiwa, nilichokifanya nilienda kufunga mlango kwa ndani kisha nikaenda kuvaa bukta chumbani nakurudi pale sebuleni, nikaenda kukaa pembeni ya Ruqaiya. Nilishtuka sana kumuona akilia, ikabidi kazi ya kumbembeleza ianze.

“Nataka uniambie ulikuwa wapi ndiyo mambo mengine yataendelea, unajua ni kwa kiasi gani nimehangaika kukutafuta?”

“Sijaenda popote mke wangu, nimeshinda hapa nyumbani yaani nimekamatwa na tumbo la kuendesha tangu jana usiku mpaka nahisi kufa,” nilidanganya, akanitazama huku akiendelea kutokwa na machozi.

“Nimekupigia simu mara ngapi? Nimekutumia meseji ngapi? Kwa nini hunijibu? Kwa nini unanifanya niwe na wasiwasi kiasi hiki?” alisema huku akiendelea kulia, nikamkumbatia na kuendelea kumbembeleza.

Kitendo cha Ruqaiya kunililia kiasi kile kilinitisha kwa sababu kama nilivyowahi kueleza, alikuwa ni mwanamke wa nguvu haswaa! Kwanza alikuwa mzuri kuanzia sura mpaka umbo lakini kubwa zaidi, alikuwa na fedha za kutosha na aliolewa na mwanaume anayejimudu kwelikweli kimaisha!

Kwa hadhi yake, hakutakiwa kabisa kumwaga machozi kwa sababu ya ‘kivuruge’ mimi, nikajihisi kuwa na hatia kubwa ndani ya moyo wangu. Wakati nikimbembeleza, akili yangu nyingine ilikuwa ikimfikiria Khazija, maana nilipoondoka pale kwake nilimwambia nitarejea muda si mrefu, nikawa najiuliza akiamua kunifuata itakuwaje?

Yaani nishinde kutwa nzima nikiwa naye ndani kwake halafu atoke anikute na mwanamke mwingine ndani, tena siku moja tu baada ya kutokea kwa tatizo lingine kama hilohilo lililomliza sana! Itakuwaje?

“Inawezekana wewe una mwanamke mwingine ndiyo maana unanifanyia hivi, kwa nini lakini unanitesa jamani?”

“Ha..pana! Sina mwanamke mwi..ngine Ruqaiya, nisamehe mama, nakupenda sana,” nilijiumauma kwenye maelezo yangu.

“Sasa kwa nini unanitesa mwenzio kiasi hiki? Angalia nalia machozi kwa sababu yako,” alisema huku akianza kufungua ushungi aliokuwa amevaa kwa sababu alikuwa anapenda sana kujistiri mwili mzima.

Niliendelea kumbembeleza lakini akawa bado analalamika huku akiendelea kupunguza nguo kwenye mwili wake, moja baada ya nyingine huku akionesha kuwa na ‘kiu’ iliyopitiliza, moyo ukawa unanidunda kwelikweli.

Kilichofanya moyo unidunde ni kwa sababu Khazija alikuwa amekombeleza kila kitu kwenye chungu cha asali kiasi kwamba sikuwa na uwezo wa kumlambisha Ruqaiya asali kama alivyokuwa akitaka.

Nikiwa bado naendelea kujiuliza nini cha kufanya, nilimshuhudia akimalizia nguo ya mwisho kisha akasimama na kujinyonganyonga kimadaha mbele yangu kama wafanyavyo wanamitindo, akahamia kwenye bukta yangu na kuitoa, akamvamia ‘mkuu wa kaya’ kwa mbwembwe zilizopitiliza.


ITAENDELEA

Powered by Blogger.