KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Mwajuma Utamu Sehemu Ya Kwanza (1)

IMEANDIKWA NA : JUMA HIZA

Nakumbuka ulikuwa ni mwaka 2010, nilipata bahati ya kufanya kazi za ndani katika nyumba moja iliyokuwepo maeneo ya Kijitonyama. Ilikuwa ni familia ya Mzee Gidion pamoja na mke wake ambapo katika maisha yao walifanikiwa kupata watoto wawili, mtoto wa kwanza alikuwa ni wa kiume aliyejulikana kwa jina la Daniel na mwingine wa mwisho alikuwa ni wa kike aliyejulikana kwa jina la Naomi.

Mzee Gidion alikuwa akimiliki kampuni moja hapa mjini iliyomuingizia kiasi kikubwa cha pesa, aliishi maisha mazuri yeye pamoja na familia yake.
Baada ya kupita miezi mitatu tangu nilipoanza kufanya kazi za ndani katika nyumba hiyo Mzee Gidion alianza kunitamani, alichokuwa akikihitaji ni penzi langu tu, aliahidi kunifanyia mambo mengi sana katika maisha yangu endapo kama ningekubali ombi lake la kulala naye kitanda kimoja.

Kiukweli lilikuwa ni jambo gumu mno hasa ukizingatia mke wake ndiye aliyenileta katika nyumba hiyo kwa lengo la kufanya kazi, sikuwa tayari kumkubalia ombi lake lakini kutokana na tamaa za pesa zilizoniingia nikajikuta nikimkubalia na kuanzisha mahusiano naye ya kimapenzi.
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kushiriki mapenzi tangu nizaliwe, Mzee Gidion ndiye alikuwa mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu, alionekana kufurahishwa sana na kitendo hicho, kwanza hakutegemea kama angeweza kunikuta na usichana wangu mpaka kufikia umri wa miaka ishirini niliyokuwa nayo, hilo lilizidi kumfurahisha mno.

Niliendelea kuwa katika mahusiano ya kimapenzi na Mzee huyo ambaye aliniambia nilitakiwa kufanya siri, hakutaka mke wake afahamu kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Alinitahadharisha niwe makini kwani kama mke wake angeweza kufahamu mahusiano yetu ningejiingiza katika matatizo makubwa.

Hilo halikuwa tatizo, niliendelea kuwa katika mahusiano na Mzee Gidion huku penzi lake likizidi kuniteka. Ukumbuke kuwa Mzee Gidion ndiye alikuwa mwanaume wangu wa kwanza kunitoa usichana wangu, alikuwa amenifungulia dunia mpya ya mapenzi, hapo kabla nilikuwa ni mtu wa kuyasikia mapenzi jinsi ambavyo watu walivyokuwa wakiyasifia pamoja na utamu wake, sikuwa nikifahamu lolote kuhusu mhemko na raha ambazo mtu alikuwa akizipata wakati akifanya mapenzi.

Tangu nilipofanikiwa kufanya mapenzi kwa mara ya kwanza na Mzee Gidion nilijihisi kuwa kiumbe kipya, nilijiona kukamilika kuwa msichana.
Kipindi hicho Mzee Gidion alianza kunijali, alikuwa akinipa kiasi cha pesa chochote nilichokuwa nikikihitaji.
"Msichana mrembo kama wewe unatakiwa uwe na simu kali, upendeze yaani ubadilike, uishi kimjinimjini, nitahakikisha nayabadilisha maisha yako Mwajuma," aliniambia Mzee Gidion.

"Nitashukuru Baba," nilimwambia.
"Usiniite Baba, sifananii kuwa Baba yako mzazi hata wa kuchorwa, niite mpenzi au Gidion tu inatosha," aliniambia.
Kwa kumtazama Mzee Gidion alionekana kuwa Baba yangu kabisa, alikuwa ni Mzee wa makamo ambaye alifanikiwa kuwa na watoto wawili. Kipindi hicho Daniel ambaye ndiye mtoto wake wa kwanza alikuwa akisoma chuo kikuu cha Daresalaam, alikuwa akisomea sheria, ulikuwa ni mwaka wake wa pili.
Kwa upande wa Naomi alikuwa kidato cha tatu, alikuwa akisoma Morogoro katika shule moja ya bweni, maisha yake yote yalihamia huko mpaka wakati wa likizo ulipofika ndipo ambapo aliweza kurudi nyumbani.

Unaweza ukaona jinsi ambavyo maisha yalivyokuwa katika nyumba hiyo, kila mtu alionekana kuwa bize na mambo yake, kuanzia Mama, Baba na watoto, muda mwingi nilibaki peke yangu nyumbani.
Mzee Gidion aliitumia nafasi hiyo kuwa fursa ya kuwa karibu na mimi. Aliamua kuninunulia simu kwa lengo la mawasiliano, alihitaji kuwasiliana na mimi zaidi na zaidi.

Siku ziliendelea kukatika huku penzi kati yangu na Mzee Gidion likizidi kupamba moto. Alipanga kuninunulia nyumba pamoja na gari la kifahari kwa dhumuni la kunihamisha nyumbani hapo, hakutaka kuona mapenzi yetu yakiendelea kuwa siri, alinogewa na utamu wa penzi langu.

Nilijisikia furaha sana kusikia hivyo, niliamini huo ndiyo ulikuwa mwanzo wangu wa kusahau umasikini niliyotoka nao nyumbani kwetu Mtwara.

Kila kitu kilichokuwa kikiendelea kiliniweka katika wakati wa furaha sana, nilizidi kumpenda Mzee Gidion, nilisahau kama alikuwa ni mume wa mwanamke aliyenitoa kijijini na kunileta mjini kwa lengo la kufanya kazi, ahadi nilizowaahidi wazazi wangu pamoja na kiapo nilichokiapa mbele yao kwa wakati huo nilikuwa nipo kinyume kabisa.

INAENDELEAAA......
Powered by Blogger.