KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo: Mwajuma Utamu Sehemu Ya Tisa (9)


Baada ya sekunde chache wasichana wawili wakaondoka na kubaki msichana mmoja, mazingira niliyoyaona yalitafsiri wazi kulikuwa kuna biashara ya uchangudoa iliyokuwa inafanyika, kuna muda yule msichana nilimuona akiwa anajigeuza sehemu za nyuma ya maumbile yake. Haikuchukua muda, msichana yule akaingia ndani ya gari kisha likawashwa na kuondoka.

"Mwajuma," aliniita Savela baada ya yule muhudumu kuondoka.
"Abee," nilimuitikia.

"Umemuona huyu muhudumu?"
"Ndiyo nimemuona kwani amefanya nini?"
"Kuna mtu amemuagiza aje kuniambia kuwa ananiita."
"Mtu gani?"
"Ni mwanaume."
"Mmh!"
"Subiri nikaongee naye," aliniambia kisha akainuka na kwenda kwenye meza iliyokuwa jirani kidogo na sisi.

Katika meza hiyo alikuwa amekaa mwanaume mmoja ambaye alionekana kuwa na mwili wa miraba minne, pembeni yake alikuwa amekaa msichana mmoja ambaye alionekana kuwa katika mavazi yaliyomuweka nusu uchi.
Savela alipofika katika meza hiyo nikamuona akikumbatiana na yule mwanaume, walionekana kama ni watu wanaofahamiana muda mrefu hivyo sikutaka kujaji sana, niliendelea kunywa soda yangu huku nikiwa sina wasiwasi wowote.
Bado niliendelea kuwashuhudia wasichana wakifanya biashara ya uchangudoa, biashara ilikuwa ikifanyika waziwazi wala hakukuwa na mtu aliyeonekana kuogopa au kushangaa, ilionekana kuwa ni biashara ya kawaida ambayo watu walizoea kuiona.

Nilibaki peke yangu katika meza hiyo mpaka pale ambapo Savela alirudi, aliniambia kuwa nilitakiwa kwenda kukaa naye meza moja na yule mwanaume aliyekuwa akizungumza naye, nilimkubalia kisha nikaenda kukaa naye katika meza ya mwanaume huyo, tulihamisha na vinywaji vyetu.

Yule msichana niliyemuona mwanzo akiwa amekaa na mwanaume huyo akainuka na kutupisha halafu nikamuona akimpa ishara fulani Savela ambayo nilishindwa kuielewa maana yake.

"Mwajuma huyu anaitwa Ibra, the big boss. Ibra huyu anaitwa Mwajuma ni msichana wangu na yeye ndiyo anainza hii kazi," alinitambulisha kwa mwanaume huyo ambaye nilishikana naye mikono.
"Okay..anaonekana kuwa mrembo sana aisee nahisi hata yale mambo yetu yatakuwa mazuri," alisema Ibra huku akitabasamu.

"Ndiyo hapo ni wewe tu sema kingine," alisema Savela kisha Ibra akanitazama, Savela akaniambia nisimame, nikafanya kama alivyoniambia.
Unajua huwa sipendi kujisifia sana lakini kwenye ukweli acha niwaambie, nilikuwa nina chura, nadhani ninaposema nilikuwa nina chura mmeshanielewa nini ninachokimaanisha, nilikuwa nina kila sifa zinazoweza kumteka mwanaume rijali.

Ibra aliponiona alizidi kupagawa, alikosa neno la kuzungumza kwa wakati huo, muda wote huo macho yake yalikuwa yakiangalia chura yangu.
"Mimi nilikwambia chombo si cha nchi hii," alisema Savela huku akitabasamu, aliimimina pombe kwenye glas kisha akanywa.
"Duh! Hiki chombo si mchezo ni balaa," alisema Ibra, wakati huo tayari nilirudi kukaa.



ITAENDELEA

Powered by Blogger.