KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Ni Shiida! Sehemu Ya Kumi na Kumi na Tisa (19)

 LOVE STORY: ni shiidaI - 4
?Nakusikiliza uliza tu??
?Unanipenda kabisa kutoka moyoni au unanitamani embu niambie ukweli bebi wangu, samahani lakini!?
?Hapana sweet kama ningekuwa nakutamani mbona ningeshaachana na wewe siku nyingi tangu nilipomaliza shida zangu kwa mara ya mwisho.?


?Nafurahi kusikia hivyo lakini kuna jambo moja linanitatiza kweli.?
?Lipi hilo na mbona leo umeamka na maswali hivyo mpenzi wangu??
?Yote hiyo kwa sababu nakupenda, nakuwaza kila muda na sipendi kukupoteza hata siku moja.?
?Hata miye sipendi nikuache, haya niambie kinachokutatiza kipi hasa??


?Bebi niambie ukweli wako kabisa maana siku nikigundua nitaumia sana! Niambie ukweli umeoa ama hujaoa???Ningeoa mke si ungemuona? Uko peke yako mpenzi wangu na ndiyo maana hata tunavyokutana huwa sina wasiwasi wowote.?
?Kweli bebi wangu??


Juliana alimtega Bitungu kwa makusudi, lengo lake ni kummbana atambue kuwa anashiriki mapenzi na familia moja yaani yeye na mama yake. Kila alipokuwa akitaka kumwambia ukweli alikuwa akisita na kumfanya aongee mengine. Mateso aliyoyapata jana yake usiku yalikuwa yamesababishwa na Bitungu huyohuyo kwa kiasi kikubwa.


Moyo wake Juliana ulishamwambia kuwa aachie ngazi. Amwachie mama yake aendeleze mapenzi yao. Juliana alijikaza kwa muda akakaa kimya kisha akaikata ile simu aliyokuwa akiongea na Bitungu. Baada ya kuikata akaamua kutuma meseji ya hasira na ya mwisho kwa Bitungu.


?Naomba unielewe kwa makini! Kuanzia sasa sitakuita tena mpenzi, bebi wala honey. Mapenzi ya mimi na wewe Bitungu naomba yaishie hapa leo hii. Nilikupenda Bitungu lakini ukweli nilioujua ndiyo umenifanya kuchukua maamuzi haya magumu, ukweli wa wewe kuto....?

...Likishaondoka zake tu nitakwambia Bitu wangu wala usiwe na shaka!"
"Haya bebi wangu, nakupenda! Wewe ndo kila kitu moyoni mwangu.."


ILIPOISHIA
...Likishaondoka zake tu nitakwambia Bitu wangu wala usiwe na shaka!"
"Haya bebi wangu, nakupenda! Wewe ndo kila kitu moyoni mwangu.."
SEREBUKA NAYO SASA...

Baba Juliana aliisoma meseji ile aliyoituma Bitungu kwa hasira kali. Akaizima kabisa simu ile na kuiweka pembeni kisha akainamisha kichwa chake chini na kujikaza kiume. Moyoni alikosa raha, hakuwa na amani tena.

"Hivi mama Juliana wa kunifanyia hivi? Kitu gani ambacho simridhishi mwanamke huyu?"
Alijiongelea na kujijibu mwenyewe. Aliamua kutoka nje ya ofisi lengo likiwa kwenda kupata hewa zaidi. Kile kiyoyozi kilichokuwa kimefungwa ofisini kwake alikiona hakitoi hewa yoyote.
***
Siku nzima mama Juliana alikuwa kama mtu aliyechanganyikiwa, kila muda alikuwa akimuita Juliana bila kumwambia chochote. Wakiwa wametulia jikoni mara simu ya Juliana ikaita.
"Haloo!"

"Mama yako yupo wapi?"
"Niko naye hapa!"
"Nipe niongee naye."
Bado hasira za maneno kutoka kwa Bitungu aliyokuwa ametumiana naye kwa njia ya meseji hazikuwa zimemuisha.

"Mama! Simu yako, baba anataka kuongea na wewe!"
"Haloo!""Nisikilize kwa makini mama Juliana! Nina jambo zuri nataka kukwambia mke wangu!"
"Nakusikia mume wangu!""Nitachelewa kurudi leo lakini ikifika saa moja nitakuhitaji uje sehemu sawa?"
"Haya niambie ni wapi?"

"Kuna sehemu nitakuelekeza baadaye tukishaambiwa rasmi hapa ofisini kwani bosi wetu ametushtukiza kuwa leo mke wake amewasili mchana na jioni tutajumuika naye katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa.""Haya utaniambia mume wangu ngoja niandae nguo ya kuvaa kabisa!"

Baba Juliana akawa ameshacheza na akili ya mkewe. Akaikata simu kwa makogo huku akiamini mtego wake utanasa kwa asilimia zote. Akamtumia na meseji ya msisitizo.
"Usisahau kunibebea na koti langu la suti nililisahau!"
"Haya, umesema saa moja!"
"Ndiyo?"

"Sasa simu yangu unayo nitakujaje mume wangu?"
"Tumia simu hiihii ya Juliana!"
"Haya baadaye basi!"
"Sawa usisahau mke wangu uwepo wako ni muhimu sana kwa siku ya leo.
***
Ilipofika saa kumi na mbili baba Juliana alikuwa bado kazini. Malengo yake ni kuwakutanisha Bitungu pamoja na mama Juliana ili aujue ukweli. Hakuwa ameiwasha ile simu ya mama Juliana tangu mara ya mwisho wamalize kutumiana meseji.

Kitendo cha kuwasha tu simu ya mama Juliana aliyokuwa nayo, meseji mfululizo zikaanza kuingia, zote zikiwa ni lawama kutoka kwa Bitungu."Sweet, kwa nini unanifanyia hivi? Mbona unanizimia simu lakini muda wote nakutafuta?"

Baba Juliana akamjibu meseji karibia zote.
"Sorry bebi wangu jamani, huku kwetu umeme ulikatika na hapa nilipo ndiyo kwanza simu nachati na wewe huku ikiwa kwenye chaji.

INAENDELEAH
Powered by Blogger.