KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Ni Shiida! Sehemu Ya Kumi na Ishirini (20). Mwishoo

 LOVE STORY: ni shiidaI - 4
"Haya muda si umeshafika jamani fanya basi tukutane mwenzio nina hamu na wewe kweli!"
"Tena una bahati nimeshatoka Bagamoyo tangu saa saba za mchana, nipo maeneo ya Tegeta."
"Huko unafuata nini bwana njoo tukutane baa ya Sweet Mama hapa karibia na Sinza Mori kuna gesti moja nzuri sana."

"Basi nipe nusu saa sweet wangu."
Bitungu alikuwa na pupa. Hakutaka kuambiwa chochote, meseji kutoka kwa baba Juliana kwa kutumia simu ya mama Juliana zilimchanganya. Asilimia zote alijua anachati na mama Juliana.
Shangwe zilimtawala baba Juliana na kujiona zoezi lake linaenda kukamilika ndani ya muda mchache. Tayari alikuwa ameshamteka akili Bitungu na kumsubiria ajilete tu.

"Nimeshafika sweet wangu uko wapi?"
"Nitachelewa bebi ila chukua chumba kabisa kisha niambie namba ngapi nitakuja moja kwa moja."
Muda wote baba Juliana alikuwa eneo la nje ya Baa ya Sweet Mama akimsubiri Bitungu. Bitungu alifika na kuchukua chumba namba 32 kisha akatuma meseji.
"Nimeshafika! Nipo chumba namba 32."

"Haya bebi wangu nipo maeneo hayahaya nikute mlango wazi huko!"
Mama Juliana naye alikuwa amewasili. Alikuwa ameongozana na Juliana lakini alipofika alishikwa na mshangao baada ya kumkuta mumewe akiwa amekaa mwenyewe huku kukiwa hakuna dalili yoyote ya sherehe.

"Juliana amefuata nini hapa?"
"Mume wangu si umeniambia sherehe nikaona bora tuwe wote!"
"Ok, sasa tunaelekea kwenye chumba namba 32 kwenye sherehe yenyewe."

Hofu kubwa ilianza kumjaa mama Juliana. Mapokezi hakukuwa na mhudumu hivyo wakaongoza moja kwa moja wote watatu huku akisitasita lakini baba Juliana alikuwa nyuma yake akimsukuma.
"Sherehe ipo humu ndani ingia!"
Baba Juliana akamsukuma mkewe, akafungua kitasa na kuingia huku akibaki nje ya mlango na Juliana.
"Sweet wangu!"

Haraka Bitungu akamuwahi mama Juliana.
"Nani?"Kabla Bitungu hajamalizia, baba Juliana akiwa na Juliana wakaingia chumbani. Bitungu akashangaa zaidi."Bitungu?"

Juliana uzalendo ukamshinda akasimulia yote kuhusu Bitungu alivyowachanganya na mama yake huku mama Juliana akibaki hajielewielewi.

"Nimejua yote kuanzia mwanzo kisha wewe mama kuanzia leo mimi na wewe ndiyo basi baki na huyo mpumbavu wako. Meseji zote hizi hapa kama ushahidi kwa ndugu zako."

************************MWISHOOOOOO*******************?
Powered by Blogger.