KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Ni Shiida! Sehemu Ya Kumi na Kumi na Nane (18)

 LOVE STORY: ni shiidaI - 4
"Halafu wewe mshenzi wewe? Kwanza una bahati sana baba yako kasahau kuhusu pafyumu hii. Haya niambie ukweli umeitoa wapi hii pafyumu ya kiume?""Mama si nilishakwambia kuwa nilijibanabana nikanunua!""Unasemaje? Ukanunua siyo?"


Hasira za mama Juliana zilimwishia Juliana. Tayari alishajiona amempoteza Bitungu kwa jinsi mumewe alivyoondoka kwa hasira akiwa na simu yake mbaya zaidi aliposema atakula nayo sahani moja kuhakikisha anamjua na kumpata. Alimshika Juliana kwa nguvu kisha akamwachia."Nakupa nusu saa, naenda chumbani huko alipo baba yako, nikirudi nataka uiniambie ukweli wote hii pafyumu umeitoa wapi?"


Kitendo cha mama Juliana kuondoka huku nyuma kamwacha Juliana na maswali ya sintofahamu. Cha kwanza mama yake alivyojichanganya kwenye jina la Bitu lililokuwa kwenye simu ya mama yake na pili ni kumjibu mama yake juu ya ile pafyumu alipoitoa.


"Nitamweleza pafyumu ya Bitungu akinipiga namwambia baba ukweli wote hadi nilivyomshuhudia gesti kule Bagamoyo kama kukosa tukose wote tu."Juliana alijiongelea na kujijibu mwenyewe. Aliiweka ile pafyumu pembeni kisha akajipindua pale kitandani na kuanza kuutafuta usingizi akiwa na maswali kibao kichwani.
***
Muda wote Bitungu alibaki na bumbuwazi asijue lipi la kufanya. Maneno ya mwisho aliyoyasikia kwenye simu yalimpagawisha zaidi. "Ina maana atakula sahani moja na mimi? Hapana mimi kidume kwanza atakuwa ni hawara wake tu."


"Lakini bado picha haijanijia! Kweli sweet wangu ndiyo aniingize kwenye matatizo? Na kwa nini simu alimpa mume aipokee kama kweli ananipenda?"Alichokifanya Bitungu ni kutoka moja kwa moja hadi bafuni na kuoga kwa mara nyingine kisha akavaa nguo na kulipia mule gesti na kuondoka.


"Kama anajijua ni mke wa mtu basi na mimi ni mume wa mtu, naenda kuusema ukweli wote kwa huyo mumewe anayetaka kula sahani moja na mimi."



Hakujali giza lililokuwa limefunika. Muda wa saa nne za usiku wala haukumtisha ndiyo kwanza alielekea moja kwa moja hadi kituo cha daladala ambapo napo alikuta patupu. Daladala nyingi zilikuwa zimeshakwenda kupaki lakini hilo halikumuuza kichwa Bitungu.


?Haiwezekani nikaingia matatizoni eti kisa mwanamke!?
Alijiongelea mwenyewe Bitungu huku akisubiri usafiri wa daladala. Hadi nusu saa inakatika bado hakukuwa na dalili zozote za kutokea kwa daladala zaidi ya Bitungu kuendelea kujiegesha kwenye eneo maalum la kukaa abiria.


?Lakini? Hivi kwa nini nisirudi kulala halafu asubuhi nikadamkia huko? Hapana ila nisubiri kwanza tu.?
Bado akili ya Bitungu haikuwa imekaa sawa. Baada ya kukaa kwa muda moyo wake ukaingiwa na furaha. Furaha baada ya kuiona daladala ikiingia kituoni hapo ikitokea katikati ya jiji la Dar.
?Haipakizi tena hii, inaenda kulala.?


Aliongea kondakta wa ile daladala baada ya Bitungu kupitisha mguu wake akitaka kuingia ndani.
?Kama haipakizi sawa nitaenda kulala hukohuko inapolala.?


?Mwana mbona husikii! Hii inalala hapo pembeni mpaka asubuhi saa kumi na mbili ndiyo inahamsha tena.?
?Lakini nyie makonda mnajifanyaga wajanja sana, mnasema haipakizi halafu baada ya muda inapakiza tuwaeleweje??

Aliongea Bitungu kwa jazba. Lengo lake akilini lilikuwa ni kutoka tu maeneo yale ya Bagamoyo hata kama atafika mjini usiku mnene ingekuwa sawa tu ili mradi atoe dukuduku lake kwa baba Juliana.


Ile daladala ilipomaliza kushusha ilijisogeza hadi pembeni na kupaki. Bitungu alinyong?onyea ikambidi akubaliane na ukweli kuwa muda ule alikuwa amechelewa. Alichokifanya ni kurudi mpaka kwenye ile gesti kwa mara ya pili na kuchukua chumba kingine kwa lengo la kudamkia asubuhi na mapema kwa mama Juliana akauseme ukweli kwa mumewe.
***
Hadi asubuhi kunakucha, si mama Juliana wala baba Juliana ama Juliana aliyekuwa ameamka. Wote walikuwa wamepitiwa na usingizi. Haikuwa kawaida ya baba Juliana kupitiwa na usingizi kiasi kile ila ilimtokea kwa kuwa alikuwa bado hajisikii vizuri kiafya.


Juliana alikuwa mtu wa kwanza kushtuka chumbani kwake. Alitoka hadi sebuleni ambapo saa yao ya ukutani ilimuonyesha kuwa tayari ilikuwa imetimia saa mbili za asubuhi. Kumbukumbu za kichapo cha jana yake usiku bado zilimtawala akilini. Kikubwa kilichomuuma zaidi ni kuendelea kuchanganywa kimapenzi na Bitungu. Aliiwasha simu yake na kumpigia Bitungu.


?Bitungu mpenzi!?
?Niambie sweet, vipi mzima jamani!?
?Bitu miye naumwa na nataka uje unione nyumbani??
?Unaumwa? Nini tatizo??


?Bitu naumwa kwa kukuwaza wewe, unaniweka kwenye wakati mgumu wakati unajua fika kuwa nakupenda!??Sijakuelewa? Nakuweka katika wakati mgumu kivipi wakati wajua fika bado nipo huku Bagamoyo na wafanyakazi wenzangu na huku semina iliyonileta itaisha baada ya wiki.?
?Nikuulize kitu bebi??

INAENDELEA
Powered by Blogger.