KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Tipwatipwa Tetema... Ooh Tetema! Sehemu Ya Tatu (3)


“Aah! Mam’dogo! Mambo gani tena hayo ya kuchoreshana?”

“Mh! Umetoka kwa mwanamke looh! Halafu hebu njoo nikwambie kitu.”

“Usimwambie baba mdogo nakuomba, mtu mwenyewe si unamjua? Anaweza kunirudisha bush,” nilimwambia kwa staili ya kumbembelea, basi akawa ananitazama machoni, akatabasamu.

“Enhe niambie ulichotaka kuniambia.”

“Ujue baba ako mdogo mi simuelewi siku hizi, nahisi kama ana mwanamke wa nje!”

“Mh! Mamdogo bana, itakuwa unamuhisi vibaya tu baba mdogo, sijawahi kumuona akiwa na mambo hayo, siyo kweli.”

“Mi nakwambia! Yaani kuna dalili hizo anazionesha kwa muda mrefu sana sasa hivi, isitoshe mimi bado sijazeeka mama ako mdogo kama unavyoniona, damu bado inachemka kwa hiyo kuna baadhi ya mambo nisipoyapata nitalazimika kuyatafuta.”

“Unamaanisha nini mamdogo?”

“Ina maana hujanielewa mpaka hapo?”

“Sijakuelewa kwa sababu mbona baba mdogo anawahi tu kurudi nyumbani na akirudi haondoki mpaka asubuhi, siku nyingine anashinda kutwa nzima hata hatoki?”

“Mh! Yaani we acha tu, mambo mengine hadi yanatia aibu kuyazungumza. Ngoja nitakuja baadaye tuongee kwa kirefu zaidi. Lakini niambie ukweli, umetoka kwa mwanamke wewe eeh! Mbona umelegealegea namna hii,” alisema mama mdogo huku eti akinishika begani na kujaribu kunitingishatingisha.

Nilicheka na kumpita mama mdogo, nikaelekea chumbani kwangu ambapo kabla ya kuingia, nililibwaga kapu langu lililokuwa linanuka shombo kisha nikaingia na kuvua nguo, nikaelekea bafuni kujimwagia maji.

Wakati naendelea kuoga, nilijiuliza maswali mengi kuhusu mama mdogo! Hatukuwa tumezoeana naye kiasi hicho na mara zote nilikuwa namuona kama mnoko kwa kuwa alikuwa akimwambia baba mdogo mambo yangu, hasa ninapovusha ‘mizigo’ na kuiingiza magetoni, sasa iweje leo aoneshe kuzoeana na mimi kiasi kile?

Kuna tatizo gani kati yake na baba mdogo mpaka afikie hatua ya kuniambia mambo mazito kiasi kile? Amesema anataka kuja chumbani kwangu ili tuongee zaidi, tuongee kuhusu nini? Nilijiuliza maswali mengi yaliyokosa majibu.

Basi niliendelea kujimwagia maji, nikawa pia namkumbuka Mimah, nikajikuta naishia kutabasamu tu mwenyewe. Nilimaliza kuoga, nikatoka na kurudi chumbani kwangu, nikawa najifuta maji kwa taulo.

Kwa kawaida mimi ninapokuwaga ndani, huwa najiachia sana kwa sababu nalala peke yangu halafu ni nadra sana kwa watu kuingiaingia ndani kwangu. Basi kama kawaida yangu, nilikuwa nikijifuta maji huku nikiwa naimba nyimbo za hapa na pale, nikawa najikausha kichwani kwa taulo langu, ghafla nikasikia mlango kama umefunguliwa hivi.

Nilishtuka kwelikweli na kugeuka, katika hali ambayo sikuitegemea, mama mdogo alikuwa ameingia chumbani kwangu. Haikuwa kawaida yake kuingia ndani kwangu, na hata kama alikuwa na shida yoyote, basi ilikuwa ananiitia nje, iweje leo aingie ghafla kiasi hicho? Yote tisa, kumi ni hali aliyonikuta nayo.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Nilikuwa kama nilivyoletwa duniani, nikamuona mama mdogo akinitazama hapa maeneo ya chini ya tumbo, nilijisikia aibu sana. Cha ajabu zaidi ni kwamba aliendelea kukazia macho kama vile hakuona kosa lolote alilolifanya, sijui na mimi akili zangu zilienda wapi, nikajikuta nikizubaa kujisitiri kwa lile taulo kiasi cha kuacha sinema ya bure iendelee.

“Ooh! Samahani, daah, samahani sana,” alisema mama mdogo huku eti akijifanya kugeukia pembeni, basi na mimi ndipo nilipopata akili ya kujifunga taulo langu, nikashindwa kabisa kumtazama mama mdogo, nikageuza shingo pembeni huku nikiwekaweka vitu vizuri kwenye meza yangu.

“Mh! Samahani sana mwaya, ujue sikutegemea kukukuta katika hali kama hii, nisamehe sana hata sijui nisemeje,” aliniambia huku akipita na kukaa kitandani kwangu.

“Ni kuhusu ile ishu niliyokwambia kwamba nitakuja tuongee vizuri, nimeona niwahi kabla baba’ako mdogo hajarudi, si unajua hachelewi kurudi?” aliniambia huku akinitazama kwa macho fulani hivi yaliyojawa na aibu za kikekike.

“Mh! Sasa akirudi ghafla itakuwaje?”

“Mh! Tena umenikumbusha,” alisema mama mdogo na kuinuka, akawa anatembea kuelekea kwenye mlango lakini ile tembea yake haikuwa ya kawaida, niligundua kwamba alikuwa akijitingisha kwa makusudi kabisa, kengele ya hatari ikalia ndani ya kichwa changu.

Undugu wetu jinsi ulivyokuwa, huyu baba yangu mdogo alikuwa ni rafiki yake kipenzi na baba waliyekuwa pamoja kule kijijini kiasi kwamba baadhi ya watu wasiowajua walikuwa wakihisi kwamba ni mtu na mdogo wake wa kuzaliwa tumbo moja.

Tangu nikiwa mdogo nilikuwa nikimheshimu sana kwa sababu kwa macho yangu nilikuwa naona alivyokuwa akiishi vizuri na baba, wakisaidiana kwa mambo mbalimbali huku pia familia yao na yetu, zikiwa ni kama ndugu.

Baadaye, ndipo alipopata nafasi ya kuja jijini Dar es Salaam ambapo baadaye alijijenga na kuanzisha familia yake. Kutokana na ukaribu wa familia zetu, kila aliyekuwa akifunga safari kuja Dar es Salaam, alikuwa akifikia kwake na mara kwa mara akija kijijini, alikuwa akija kwetu, wakati mwingine akilala palepale nyumbani.

Ni huyu ndiye aliyempa baba wazo kwamba badala ya mimi kuendelea kukaa kule ‘bush’, ni bora nije mjini kujaribu kutafuta maisha na akatoa na nafasi ya mimi kufikia hapo nyumbani kwake. Kwa hiyo sijui niseme nini kuhusu jinsi nilivyokuwa namheshimu, alikuwa mtu muhimu sana kwangu.

Hata hivyo, mke aliyekuwa amemuoa, hakuwa wa rika lake, yeye baba mdogo alikuwa mkubwa sana, makamo ya baba yangu mzazi lakini mkewe, alikuwa bado mbichi kabisa ingawa mwili wake wa ‘utipwatipwa’ ungeweza kufanya mtu akaamini kwamba na yeye ni mtu mzima sana.

Siku za mwanzo hata mimi nilikuwa najua ni mkubwa sana lakini baada ya kumzoea, niligundua kwamba hakuwa sawa na baba mdogo.

Tena kingine yeye alikuwa ni mtoto wa mjini haswaa, kuanzia mavazi mpaka mambo yake, yaani kwa kifupi ndiyo hivyo. Hata ongea yake ilikuwa ni ile ya kimjini mjini, akikutazama macho yake unayaona kabisa kwamba hayajatulia, akitembea wakati mwingine anajitingisha kwa makusudi kama alivyokuwa akifanya muda huo.

Nakumbuka baba mdogo aliwahi kuoa mke kule kijijini ambaye hata mimi nilikuwa namfahamu, wakazaa watoto wakubwa tu lakini sijui baadaye nini kilitoka, baba mdogo akaachana naye na kuja mjini ambako alioa mke mwingine ambaye ndiyo huyo sasa aliyekuwa mbele zangu.

Kwa kuhofia kumkaribisha pepo mchafu, niliamua kutomtazama mama mdogo alivyokuwa akienda pale mlangoni, nikamsikia akifunga mlango kwa ndani, akachomoa kabisa funguo, kisha akarudi na kukaa pale kitandani.

Alipokaa, upande wa khanga aliokuwa amejifunga kwa chini, ulifunuka na kusababisha paja lake moja lililonona kisawasawa, lionekane, nikajikuta nikikosa kabisa utulivu.

“Mbona ni kama unaniogopa? Hebu njoo basi ukae hapa nikueleze harakaharaka nilichotaka kukwambia kabla baba yako mdogo hajarudi,” alisema kwa sauti ya kunong’ona.

Haikuwa kwamba namuogopa kwa sababu muda mfupi tu uliopita nilitoka kupelekeshana kisawasawa na Mimah ambaye alikuwa na mwili mkubwa kuliko mama mdogo, lakini ile heshima niliyokuwa nayo kwa baba mdogo ndiyo iliyonipa kigugumizi.

Nilishaelewa alichokuwa anakitaka, kitendo cha yeye kumtazama ‘mkuu wa kaya’ kwa macho ya matamanio kama mama mjamzito aliyeona kipande cha ndimu, na yale masihara aliyonifanyia pale nje, nilishajiongeza ndani ya kichwa changu na kujua nini kitafuatia.

Basi nilisogea kwa tahadhari na kukaa pale pembeni yake, akanigeukia na kunitazama, na mimi nikajikaza kiume na kumtazama.

“Baba yako mdogo angekuwa na naniliu kama hii yako mbona ningefaidi mimi? Yake siyo kama hii, halafu akigusa kidogo tu, kwisha habari! Yaani kama jogoo, na hawezi kurudia tena mpaka kesho yake, mi nateseka mwenzio,” alisema mama mdogo na kuanza kujiliza, kitendo cha kutaka kumbembeleza kikawa kosa kubwa, sijui alifanyaje bwana, nikashtukia amemchomoa mkuu wa kaya na kumkamata.





“Hapana! Hapana,” nilisema huku ‘nikipaparika’ mithili ya kuku aliyekatwa kichwa. Kila kilichokuwa kikitokea kilikuwa kikitokea kwa kasi kubwa sana, sikuwahi kudhani hata siku moja kwamba naweza kuja kuwa na hali kama hiyo na mama mdogo.

Ulikuwa ni mtihani mgumu sana kwangu kuushinda, nilishindwa kuelewa natakiwa kufanya nini kwa wakati huo.

“Unaogopa nini bwana,” alisema kwa sauti iliyotokea puani, akawa ananitazama kwa macho ambayo yalizidi kunihamasisha mno. Sikuwahi kumuona mama mdogo akiwa ananitazama kwa macho yaliyokuwa yamebeba ujumbe mzito kiasi hicho, siku zote nilizoea kumuona akinitazama kwa macho makavu, wakati mwingine akinitazama kwa dharau lakini siku hiyo ilikuwa tofauti kabisa.

Aliendelea kumbinyabinya mkuu wa kaya huku akimeza mate mithili ya fisi aliyeona mfupa na nikiwa bado naendelea kujiuliza maswali mengi yasiyokuwa na majibu, sijui nini kilitokea bwana, nilishtukia tu mimi nimelala chini halafu yeye akaja kwa juu huku akiwa bado amemshika mkuu wa kaya kwa nidhamu ya hali ya juu.

Kwa kutumia mkono mmoja, alichomoa kufuli lake na kulitupilia mbali, akamshika tena mkuu wa kaya vizuri, taratibu akamuelekeza njia ya kupita, kisha akawa anamsindikiza huku macho yake akiwa ameyafumba.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Kiukweli akili zangu zilihama, ni kama nilipandwa na pepo mbaya, nikauweka ‘umama mdogo’ pembeni na sasa nikawa naonesha ushirikiano wa hali ya juu.

Aliendelea kuugulia mithili ya mtu anayefanyiwa jambo kwa kuonewa sana lakini ajabu ni kwamba akawa anaendelea kufanya ‘machejo’ pale juu huku akizidi kumsukumizia mkuu wa kaya kwenye mashimo ya Mfalme Solomon, hali iliyozidi kumkasirisha mkuu wa kaya ambaye sasa alikuwa amefura mithili ya nyoka koboko mwenye sumu kali.

Niliona ni kama ananichelewesha kwa sababu alikuwa akienda taratibu sana, basi nikajipindua kama mwanasarakasi, yeye akawa chini na mimi juu na papo hapo nilianza kufumua mashuti ya nguvu ambayo nadhani hakuyategemea.

Licha ya mwili wake kuwa mkubwa tofauti kabisa na mimi, niliweza kumpeleka puta kuliko kawaida.

“Taratibu bwanaa, kwani ugomvi... taratibu mpenzi wangu,” alisema mama mdogo huku akiendelea kugugumia ndani kwa ndani, eti leo hii nilikuwa nimegeuka na akuwa mpenzi wake, ilikuwa ni zaidi ya kichekesho.

Hata hivyo licha ya kunibembeleza, maneno yake hayo yaliingilia upande wa kushoto na kutokea upande wa kulia, nikazidisha mbwembwe na kusababisha azidi kugugumia, ilifika mahali ilibidi nimzibe mdomo kwa sababu nilihofia kelele zake zinaweza kusikika nje! Alikuwa amenichokoza mwenyewe.

Haukupita muda mrefu, alinikamata kwa nguvu shingoni utafikiri tuna ugomvi, nikafumua shuti lingine la nguvu na kusababisha atetemeke mithili ya jenereta, mwili wake ukakakamaa kwa sekunde kadhaa na muda mfupi baadaye, aliniachia na kuangukia upande wa pili, akiwa ni kama amepoteza fahamu.

Harakaharaka niliinuka na kujifunga taulo, nikasogea dirishani na kuchungulia nje kwa sababu nilihisi kelele za mama mdogo zinaweza kuwa zimesababisha watu wajae madirishani kutupiga chabo lakini kwa bahati nzuri, nje kulikuwa na utulivu mkubwa sana.

Baada ya kujiridhisha kwamba hakuna tatizo lolote, harakaharaka nilirudi pale kitandani, nikatupa taulo pembeni na kumkabili mamdogo kwa sababu bado sikuwa nimemalizana naye.

Nilimuweka sawa na kuendelea kufumua mashuti, safari hii akiwa hanipi kabisa ushirikiano na haukupita muda mrefu, nikawa nimeshawapita mabeki wote na kubaki mimi na nyavu tu, nikafumua shuti la nguvu lililozama moja kwa moja mpaka nyavuni, akashtuka kidogo na kunikamata kwa nguvu.

“We mtoto, kwani unatumia nini?”

“Mh! Hakuna chochote, kwani vipi?”

“Kwa mara ya kwanza tangu nipatwe na akili za kikubwa, leo umenitoa chozi la kikubwa, nilikuwa nasikia tuu kwa watu kuhusu habari sijui za theluji iliyopo juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro, lakini leo nimeshuhudia mwenyewe,” alisema kwa sauti ya kichovu, nikacheka sana.

“Kwa nini baba’ako hawezi kama hivi? Yaani mimi wewe ndiyo ungekuwa mume wangu, kamwe nisingeweza kukusaliti, amini nakwambia, mwanamke yeyote anayepata huduma kama hii, hawezi kuwa na mawazo na mtu mwingine yeyote,” alisema na kunibusu kwa hisia za hali ya juu.

“Baba mdogo akijua itakuwaje?”

“Atajuaje? Utamwambia wewe?”

“Hapana lakini si unajua mapenzi hayana siri?”

“Wala usiwe na wasiwasi, hayo niachie mimi.”

“Hapana mama mdogo, hiki tulichokifanya ni makosa makubwa, hatutakiwi kurudia tena.”

“Kama haya ni makosa basi nipo tayari kuendelea kukosea maisha yangu yote, sikuwahi kudhani kwamba unaweza kuwa na uwezo mkubwa kiasi hiki, nisamehe kwa mabaya yote niliyowahi kukukosea,” alisema mama mdogo na kunikumbatia tena, tukagusanisha ndimi zetu.

Kama kawaida yake, alipitisha mkono kijanja na kumshika tena mkuu wa kaya ambaye baada ya awamu ya kwanza, alikuwa amerudi kwenye hali yake ya upole, akawa anamfanyia fujo za hapa na pale huku akiendelea kunisifia sana.

Ghafla mam’dogo aliinuka kwa kasi kama aliyekumbuka kitu, sijakaa sawa si nikashtukia amekamata kipaza sauti bwana, lilikuwa ni jambo ambalo sikulitegemea kabisa, akaanza kughani tungo laini ambazo ziliniburudisha mno, alianza kwa nyimbo za taratibu, akawa anaongeza kasi taratibu na kunifanya nizidi kujihisi kama napaa.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Haukupita muda mrefu, alifanya kama alivyofanya awali na safari hii, alikuja na mpya, alimuelekeza mkuu wa kaya sehemu yake kisha akawa ni kama anaendesha baiskeli, nikafumba macho huku nikijisikilizia, nikapeleka mikono yangu kwenye eneo lake la katikati ili kumpa sapoti, basi akaendelea kupiga ‘peda’ kwa hisia za hali ya juu.

Ilifika mahali akawa ni kama amechanganyikiwa, alianza kutukana matusi mazitomazito, ikabidi nifanye kama nilivyofanya awali, nikamziba mdomo na nilipoona bado anaendelea, nilijipindua tena na kukaa kwa juu.

“Mume wangu ni.... (tusi), haiwezekani kwa kipindi chote tangu anioe hajawahi kunipa haki yangu kikamilifu, sasa si bora kuwa mjane tu lifahamike moja?” alisema mama mdogo, ikabidi nimzibe tena mdomo.

“Akawa anaendelea kuugulia ndani kwa ndani na dakika chache baadaye, alikwea tena mpaka juu kabisa ya mnazi, akaangua dafu na kulipasua kwa nguvu, huku akiwa mithili ya mwanariadha aliyetoka kukimbia mbio za mita mia moja.

Akili yangu yote nilikuwa nimeielekeza kumzuia asije akapiga kelele kwa sababu ilishaonesha kwamba mwenzangu hayupo sawa.

“Shikamoo baba,” nilisikia watoto wakimuamkia mtu nje ambaye bila hata kuuliza, niligundua kwamba ni baba mdogo.

“Marahabaaa, hamjambo watoto wazuri?”

“Hatujambo.”

“Mama yenu yuko wapi?”

“Yupo ndani,” nilimsikia mtoto wake wa kike akimjibu baba yao. Walichokuwa wanakijua watoto hao waliokuwa wakiendelea na michezo yao ni kwamba mama yao pengine alikuwa ndani kwa sababu hawakumuona akitoka tangu alipoingia.

Sauti ya baba mdogo ilimfanya mama mdogo akurupuke akiwa ni kama haamini alichokisikia.

“Mungu wangu, tumefumwa.”

“Tulia kwanza, wala usiwe na wasiwasi.”

“Tutafanyaje sasa? Na huyu akisharudi hatoki mpaka baadaye.”

“Ngoja, nitajua nini cha kufanya, unatakiwa kutulia, sawa eeh!”

“Sawa, nakupenda,” alisema huku akinibusu.

“Mbona mama yenu hayupo? Kwani ameenda wapi?”

“Yupo, mbona alikuwa ndani?”

“Hayupo! Mjomba wenu amesharudi kuuza samaki?” nilimsikia baba mdogo huku akisogelea kwenye mlango wa chumba changu.







“Hapana, bado hajarudi!” nilimsikia mtoto mmoja akimjibu. Wakati nikirudi, pale nje nilimkuta mama mdogo tu na kwa sababu nilipoingia nilienda kuoga na kuingia ndani kabla ya mama mdogo kuja kisha tukajifungia, hawakujua kama nimerudi.

“Mbona kapu lake la kuuzia samaki lipo hapa? Au leo hakwenda nalo?” aliuliza baba mdogo, nadhani ilikuwa ni baada ya kuliona lile kapu la kuuzia samaki ambalo nililibwaga pale nje. Alijaribu kuniita lakini nilijikausha, akashika kitasa na kutingisha mlango, alipoona umefungwa akaamini kweli bado sijarudi.

Mapigo ya moyo yalikuwa yakinienda mbio kuliko kawaida, sikujua nini kitatokea endapo atagundua kwamba nilikuwa chumbani na mkewe, tukilitafunilia mbali tunda la mti uliokatazwa.

Mama mdogo alikuwa akipaparika, akitafuta sehemu ya kujificha, nikamuonesha ishara kwamba anatakiwa kutulia.

“Vaa nguo zako kimyakimya,” nilimwambia kwa sauti ya kunong’ona, kweli harakaharaka akaanza kutafuta nguo zake ambazo hata sikumbuki zilikuwa zimevuliwa muda gani.

Alianza na ‘bra’, akaivaa harakaharaka, akavaa na blauzi yake kisha akajifunga upande wa khanga, akawa ananitazama huku akionesha kuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake, basi nikawa namuonesha kwa ishara kwamba anatakiwa kutulia.

“Natoka kidogo naenda hapo barabarani, nakuja sasa hivi!” nilimsikia baba mdogo akisema, basi wale watoto wakamuitikia, wote wawili tukashusha pumzi ndefu kwa sababu ama kwa hakika maji yalikuwa yameshafika kooni.

Hakukuwa na muda wa kupoteza, harakaharaka nilisogea pale mlangoni na kufungua kimyakimya, wale watoto walikuwa wakicheza jirani kabisa na mlango wangu kwa hiyo nikawa natafuta njia ya kuwatoa pale ili mama mdogo atoke.

Nilifungua mlango na kujifanya kama najinyoosha kwa uchovu.

“Shikamoo mjomba!” walinisalimia.

“Marahaba hamjambo?”

“Hatujambo, baba alikuwa anakuulizia!”

“Ameenda wapi?”

“Amesema ameenda barabarani.”

“Nilikuwa nimelala, nimechoka sana leo, nimetembeza samaki umbali mrefu sana,” nilisema, basi nikatoka na kuliweka kapu langu vizuri, nikawa natafuta ‘taiming’ ya kuwaondoa pale uani.

“Nani nimtume dukani?” niliwauliza, kila mmoja akajibu ‘nitume mimi’. Walikuwa wananijua kwamba nikimtuma mtoto dukani, basi lazima chenji na yeye apate pipi au chochote anachokitaka.

“Sasa kwa sababu mnagombania, nataka muende wote ila msichelewe kurudi, chenji itakayobaki mtanunua mnachokitaka,” nilisema huku nikitoa shilingi elfu moja na kuwapa chupa tupu na kuwataka wakaninunulie soda ya baridi dukani.

Waliondoka wakiwa wanakimbizana, basi huo ndiyo ukawa mwanya wa mimi kumtoa mama mdogo. Harakaharaka alitoka, akaelekea kwanza bafuni ambako alijimwagia maji kisha akaelekea ndani kwake. Nadhani alikuwa anatengeneza mazingira hata mumewe akimuuliza, asingizie kwamba alikuwa kuoga.

Alipotoka, nilishusha pumzi ndefu, nikafungua mlango na kuuacha wazi ili nionekane nipo, nikawasha redio na kuanza kuburudika, kawaida yangu nilikuwa napenda sana nyimbo za Bongo Fleva, tena za wasanii wanaotamba kama Diamond na Wasafi, Ali Kiba na wengine ambao wapo kwenye chati, si unajua tena ujana.

Wakati nikiweka mazingira vizuri mle ndani, ndipo nilipogundua kwamba mama mdogo alikuwa ameacha ‘kufuli’ lake, nadhani ule mchecheto ulimfanya achanganyikiwe kabisa.

Harakaharaka nililiokota na kuanza kulitazama vizuri, sijui akili gani ilinituma nilipeleka kwenye pua, nikajikuta nikitabasamu mwenyewe. Nililihifadhi chini ya godoro, nikaendelea kupangapanga vitu vyangu vizuri kisha nikatoka na kwenda tena bafuni kuoga.

Wakati narudi tayari watoto walikuwa wamesharudi, basi nikawapokea nilichokuwa nimewaagiza, wakaendelea kucheza huku wakichekelea zawadi niliyowapa maana chenji iliyobaki walikuwa wamenunua pipi na kugawana.

Niliigida ile soda kwa kasi kisha nikajilaza kitandani, nikawa nacheua tu huku hisia tamu zikiendelea kupita ndani ya mishipa yangu ya fahamu.

Ni kweli nilikuwa nimefanya dhambi kubwa kwa kutembea na mama mdogo lakini katika mazingira kama yale, mwanaume yeyote aliyekamilika, asingeweza kumlazia damu mama mdogo, hasa kutokana na jinsi alivyokuwa amejaaliwa.

Basi nikiwa nimejilaza, nilimsikia baba mdogo akija na breki ya kwanza ilikuwa mlangoni kwangu, akaniita kwa kilugha, nikatoka na kwenda kumsalimu kwa adabu. Aliniuliza kuhusu biashara, nikamjibu kwamba inaendelea vizuri kabisa.

Nilikuwa najua kwamba lazima ataniuliza nimerudi saa ngapi na wakati ananiulizia nilikuwa nimeenda wapi lakini cha ajabu wala hakuniuliza, nikamkabidhi fedha za mauzo, akafurahi na kuelekea zake ndani.

Bado moyoni nilikuwa na wasiwasi mkubwa, nikawa sijui nini kitatokea atakapoingia ndani na kuzungumza na mkewe. Hata hivyo, haukupita muda mrefu nikawa nawasikia wakipiga stori na kucheka.

Ujue wanawake wakati mwingine ni viumbe hatari sana, yaani nilipofikiria jinsi nilivyokuwa mle ndani na mama mdogo dakika chache tu zilizopita, tukifanya dhambi mbaya ya usaliti na sasa eti alikuwa akipiga stori na mumewe na kucheka!

“Nitachelewa sana kuoa,” nilijiambia mwenyewe wakati nikiendelea kutafakari mambo mbalimbali yaliyotokea siku hiyo. Kwa upande mwingine nilijipongeza kwa sababu kiukweli, ‘ubavu’ niliokuwa nao haukuwa wa kawaida, kuwagalagaza watu wawili ndani ya siku moja, na kuhakikisha kila mmoja amepata kile alichokuwa anakistahili, haikuwa kazi nyepesi.

Kwa upande mwingine, nilimshukuru sana mzee Mbaruku, Mpemba mmoja aliyekuwa akiuza supu ya pweza kule Feri. Ni yeye ndiye aliyenifundisha kuhusu mambo ya mchuzi wa pweza na kuniambia kwamba kila ninapoenda kuchukua mzigo, lazima nipitie kwenye meza yake na kupiga bakuli la supu.

Hata zile siku ambazo sikuwa na fedha, alikuwa akinipa bure huku akinitania kwamba ananilipia, tukawa tunacheka kwa sababu alikuwa ni mtu anayependa sana masihara. Ukweli ni kwamba nilikuwa nayaona matokeo ya kunywa supu hiyo kila siku.

Wakati mwingine huwa kunakuwa na maneno mengi mitaani kuhusu haya masuala ya upungufu wa nguvu kwa sababu ukweli ni kwamba wanaume wengi sana wanasumbuliwa na tatizo hilo lakini ukweli ambao hata mimi naweza kuwa shuhuda ni kwamba ukiamua kupambana na tatizo hilo, basi we jenga utaratibu wa kuwa unakunywa supu ya pweza kila siku.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Nakumbuka mzee Mbaruku alikuwa akiniambia kwamba wanaume wa bara wengi ni wavivu sana wawapo kwenye uwanja wa fundi seremala na ndiyo maana wengi huishia kuwa na mke mmoja na kuzaa watoto wachache, tofauti na kwao Pemba ambao mwanaume kuwa na wake wawili, watatu au wanne na watoto kibao ni jambo la kawaida sana.

Akawa ananiambia kwamba kama mtu mmoja anaweza kuwa na wake watatu kwa mfano, na wote akawa anawatimizia haja zao kikamilifu, kwa nini wengine unakuta ana mke mmoja tu ambaye naye anashindwa kumfurahisha wawapo faragha?

Akawa ananiambia kwamba kuna siri kubwa imejificha kwenye suala zima la vyakula na kwa kuanzia, akaniambia sitakiwi kukosa kunywa supu ya pweza kila siku.

Maneno aliyokuwa ameniambia yalikuwa ni ya kweli kabisa kwa sababu hata ukiangalia ishu iliyokuwa imetokea jioni hiyo kati yangu na mama mdogo, sababu kubwa ilikuwa ni ileile ya matatizo ya nguvu.

Kama baba mdogo angekuwa ‘ngangari’, wala mkewe asingekuwa anamzungumzia vibaya kama alivyofanya kwangu na wala asingeweza kumdhalilisha na kutoka na mimi hata kidogo.

Basi niliendelea kutafakari mambo mengi, hatimaye muda wa chakula cha usiku uliwadia.

Tofauti na siku zote ambapo huwa naitwa kwenda kula chakula na watoto sebuleni au jikoni, siku hiyo nilishangaa mtoto mkubwa wa baba mdogo akiniletea chakula chumbani kwangu na kuniambia eti mama yake amemtuma.

Ulikuwa msosi wa maana kwelikweli, ule ambao nimezoea kumuona baba mdogo akila, leo nilikuwa nimetengewa mimi.







Sikulaza damu, nilianza kuufakamia kwa kasi kubwa kwa sababu shughuli za siku hiyo zilinifanya niwe na njaa sana. Ndani ya muda mfupi tu, tayari nilikuwa nimefuta kila kitu, sahani zikabaki tupu, nikashushia na maji mengi, tumbo likawa ‘full’.

Hapa napenda kuwamegea siri wanaume wenzangu hasa vijana, haya mambo ya kula chipsi mayai, sijui juisi na kalimati halafu ndiyo inakuwa imetoka, ndiyo yanayosababisha vijana wengi wanakuwa na matatizo ya ukosefu wa nguvu za kiume wawapo faragha.

Mtoto wa kiume inatakiwa ‘unafukia’ kisawasawa, chipsi na vyakula lainilaini waachie wanawake, ukichanganya na vyakula vingine kama mchuzi wa pweza, karanga mbichi, mbegu za maboga, mihogo na asali, unakuwa na nguvu kama simba dume, bila kusahau kupiga ‘tizi’ kila siku, mambo yanakuwa safi.

Basi baada ya kumaliza kula, sikuweza hata kutoa vyombo, nilivisogeza pembeni tu, nikajilaza pembeni ili shibe ipungue, hata sikumbuki nilipitiwa na usingizi saa ngapi. Nilikuja kushtuka usiku mnene baada ya kuhisi kuna mtu ananitingisha pale kitandani.

Nilikurupuka kwa hofu kwa sababu siku zote nilikuwa nalala peke yangu, iweje mtu aingie usiku huo? Ni nani na anataka nini?”

“Shiiiii!” nilisikia sauti ya mwanamke ikinituliza, nikagundua kwamba kumbe alikuwa ni mama mdogo, nilishtuka sana kwa sababu usiku huo alitakiwa kuwa ndani na mumewe, iweje awe ndani ya chumba changu? Baba mdogo akitoka ghafla na kugundua kwamba alikuwa magetoni kwangu itakuwaje?

“Yaani umelala bila hata kufunga mlango? Umechoka sana eeh!” alisema mama mdogo huku akiinuka na kwenda kuzima taa, wakati akitembea nilimtazama upande wa nyuma, nikajikuta natabasamu mwenyewe kwa sababu alikuwa amejifunga upande wa khanga tu na kama ujuavyo tena, ubonge wake ulisababisha eneo la nyuma liwe linatetema kwelikweli.

“Ma’mdogo hapana bwana, tutafumwa bure!”

“Tutafumwa na nani? Nimeshindwa kulala, yaani kila nilipokuwa nikiikumbuka shughuli ya muda ule mwili ulikuwa ukinisisimka, one for the road please.”

“Kwani baba mdogo si yupo ndani?”

“Anakoroma kama jenereta bovu, hebu achana naye bwana, mwanaume wa Dar es Salaam huyo,” alisema mama mdogo huku akiuachia upande wa khanga aliokuwa amejifunga, ndani hakuwa na chochote na kwa sababu na mimi nilikuwa nimelala kizembe kama kawaida yangu, hakukuwa na muda wa kupoteza.

Kitendo cha mama mdogo ambaye mwili wake ulikuwa na joto fulani hivi ‘amaizing’ kunikumbatia, kilisababisha mwili wote usisimke mithili ya mtu aliyepigwa na shoti ya umeme, mkuu wa kaya akaanza ‘kufyumu’ na ndani ya muda mfupi tu, alikuwa amekasirika kwelikweli.

Kwa kuwa sasa mazingira yalikuwa hatarishi, hakukuwa na muda wa kuremba, mama mdogo alimkamata mkuu wa kaya na kumpapasa kwa upole, naye akazidi kuwa ngangari, taratibu akamuelekeza sehemu ya kwenda! Ama kwa hakika ilikuwa burudani nyingine ya aina yake.

Mama mdogo alijisevia harakaharaka kama anayeogopa kufumwa na kutokana na papara alizokuwa nazo, hakuchukua raundi, akawa ameshakwea juu kabisa ya mnazi na kuangua dafu kisha kulipasua kwa nguvu.

“Ahsante mume wangu, ahsante baba,” alisema huku akinikumbatia kwa nguvu, akanimwagia mvua ya mabusu, akawa ni kama anataka pambano hilo lisilo na refa wala jezi liishie hapo lakini sikukubaliana naye kwa sababu alikuwa ameyaamsha mashetani na sasa ilikuwa ni lazima atii kiu yangu.

Tulibadilishana nafasi, yeye akawa upande wa chini na mimi upande wa juu, nikamuelekeza mkuu wa kaya kuelekea kwenye chungu cha asali na haukupita muda mrefu, tukawa tunaelea kwenye bahari ya kina kirefu ya huba, huku kimo cha mkuu wa kaya kikionekana kutaka kumzidia ma’mdogo.

“Taratibu baba,” alisema kwa sauti ya kulalamika, akawa ni kama ananiambia ongeza kasi, nikawa nampeleka ‘mputamputa’ na kwa mara nyingine, aliangua dafu, kubwa kuliko lile la mwanzo. Akiwa ni kama amechanganyikiwa, alipiga yowe na kama nisingewahi kumziba mdomo, huenda tungesababisha maafa makubwa.

Na mimi nikaongeza kasi na hatimaye nikafanikiwa kuzifumania nyavu kwa shuti kali lililotinga moja kwa moja golini.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

“Utaniua wewe baba,” alisema mama mdogo huku akijizoazoa na kuinuka, akanibusu kisha harakaharaka akafungua mlango na kuchungulia kwa nje, alipohakikisha hakuna mtu, alitoka na breki ya kwanza ilikuwa bafuni, nikamsikia akifungulia maji ya bomba la mvua kwa wingi.

Niliinuka harakaharaka na kwenda kuufunga mlango kwa ndani, sikutaka kuwasha taa, nikarudi kitandani na kujibwaga kama mzigo. Muda huohuo, nilisikia geti la ndani kwenye chumba alichokuwa akiishi baba mdogo na mama mdogo likifunguliwa, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida, nikajua sasa ukweli wote unaenda kujulikana.

Kuna akili zilikuwa zinanituma kuamini kwamba huenda baba mdogo alikuwa akituchungulia na baada ya kupata uhakika sasa alikuwa ametoka kuja kumaliza kazi.

“Mke wangu!” nilimsikia baba mdogo akimuita mkewe huku akisogea kule bafuni ambako maji mengi yalikuwa yanaendelea kumwagika.

“Abee mume wangu!”

“Umenishtua! Umeanza lini tabia ya kutoka nje usiku peke yako?”

“Joto mume wangu, nimeshindwa kabisa kulala kwa sababu ya joto, nikaogopa kukusumbua baba, ingia na wewe uoge, au husikii joto mwenzangu,” alisema mama mdogo kwa sauti yenye ushawishi mno.

Asivyo na akili, baba mdogo naye alishindwa kugundua kwamba alikuwa akiibiwa, akaingia bafuni na kuanza kuoga na mkewe, nikawa nawasikia wakiwa wanacheka, ama kwa hakika mama mdogo alikuwa amefuzu kwa utapeli.

Hiyo ilikuwa ahueni kubwa kwangu, nikajua hawezi kugundua chochote kuhusu mimi, nikawa najikoromesha kwa sauti ili baba mdogo ajue kwamba nilikuwa kwenye usingizi mzito.

Walitoka na kuelekea ndani, nikawa nawasikia wakiendelea na stori za hapa na pale huku mama mdogo akijichekesha sana, ama kwa hakika kuna wanawake ni wasanii sijapata kuona.

Waliingia ndani na kufunga milango, nikashusha pumzi ndefu na angalau moyo wangu ukarudi sehemu yake. Haukupita muda mrefu nikapitiwa na usingizi mzito na nilipokuja kuzinduka, tayari kulikuwa kumepambazuka.

Mwili wangu ulikuwa na uchovu usioelezeka, harakaharaka nikaamka na kukimbilia bafuni kwa sababu ilikuwa ni lazima niwahi kutoka ili nikapate samaki wazuri. Baada ya kumaliza kuoga, nilitoka na kuingia chumbani kwangu, mara nikasikia baba mdogo akigonga mlango, nadhani alikuwa anajua kwamba bado sijaamka.

“Vipi umeamkaje?”

“Salama, shikamoo baba,” nilimsalimia kwa adabu huku nikikwepesha macho yangu maana nilijua kama tukitazama na anaweza kugundua ‘uhalifu’ niliokuwa namfanyia.

“Mama’ako mdogo anakusifia sana kwamba siku hizi umebadilika kitabia. Safi sana, hayo ndiyo mambo ninayoyataka, nimekuleta mjini kutafuta pesa, siyo kuhangaika na wanawake wa mabarabarani,” alisema baba mdogo, basi nikawa natingisha kichwa kuonesha kwamba namuelewa sana.http://deusdeditmahunda.blogspot.com/

Yaani wanawake bwana! Kama upo kwenye ndoa au uhusiano wa kudumu lakini ghafla ukaanza kuona mwenzi wako anamsifia sana mwanaume mwingine, bila kujali anayesifiwa ni nani, unatakiwa kuwa makini sana.

Anaweza kuwa anasifiwa ‘house boy’ ukapuuzia kumbe anasifiwa kwa sababu mkeo kampenda! Yaani eti mama mdogo leo ndiyo alikuwa mtu wa kunizungumzia mimi vizuri kwamba eti nimebadilika? Baba mdogo alitakiwa kujiongeza sana lakini ndiyo hivyo alishindwa.

Nilimalizia kujiandaa, baba mdogo akatoa fedha za kuchukulia mzigo na kunipa, nikamshukuru na bila kupoteza muda, nilitoka mbiombio na safari ya kuelekea feri ikaanza.







ITAENDELEA
Powered by Blogger.