KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Utamu Wa Shemeji Flora Sehemu Ya Kwanza (1)

SIMULIZI NZURI YA KUSISIMUA
IMEANDIKWA NA : ATHUMAN JAY

Ni asubuhi na mapema kijana Japhet akiwa amejilaza kitandani chumbani kwake ndipo mara ghafla anashtuka kutoka usingizini baada ya kuusikia mlango wa chumba alicholala ukigongwa. Kwa uchovu mwingi sana Japhet anaamka na kujiinua kutoka kitandani anachukua T-shirt yake na kuivaa vyema halafu anaenda kuufungua mlango huo. Kumbe ni kaka yake aitwae Lukasi ndie alikuwa anamgongea mlango. "Habari za asubuhi mdogo wangu, vipi umeamkaje?" Lukasi alimuuliza Japhet.

"Habari za asubuhi ni nzuri tu kaka, nashukuru nimeamka salama" Japhet alijibu huku akipiga miayo ya uchovu.

"Ok ni vizuri kama umeamka salama, sasa ni hivi mimi ndio naondoka ile safari yangu ya kibiashara, naenda Mwanza" alisema Lukasi akimwambia Japhet.

"Ooho kaka mimi nakutakia safari njema uende salama na pia urudi salama hapa nyumbani" alisema kijana Japhet.

"Sawa mdogo wangu, na nyinyi pia m'baki salama hapa nyumbani kumbuka ni wewe mdogo wangu ndie ninaekutegemea hapa muishi vizuri na Shemeji yako pamoja na Rozi huyu dada wa kazi" aliongea Lukasi akimsisitiza Japhet.

"Sawa kaka nimekuelewa tutaishi vizuri bila ya wasiwasi" alisema Japhet.

"Nafikiri safari yangu huko niendako nitakaa kwa muda wa wiki mbili, nikirudi ndio nitashughulikia suala lako la kukutafutia kazi" alisema Lukasi huku akifungua pochi yake (Wallet) na kutoa kiasi Fulani cha pesa kama shilingi elfu hamsini hivi na kumpatia mdogo wake. "Hizo zitakusaidia mdogo wangu kwa matumizi yako binafsi madogomadogo"

"Ahsante sana kaka nakushukuru" alisema Japhet huku akizipokea pesa hizo kwa adabu zote kutoka kwa kaka yake. Baada ya hapo Japhet akaongozana na kaka yake Lukasi mpaka sebuleni ambapo ndio kulikuwepo na begi lake kubwa lililojaa nguo na vitu vingine vidogovidogo kwa ajili ya safari. Pia alimkuta na Shemeji yake anaeitwa Flora ambaye ndie mke wa huyu kaka yake.

"Habari za asubuhi Shemeji" Japhet alimsalimia Shemeji yake.

"Nzuri tu Shemeji, vipi uko poa?" Flora aliyekuwa ameketi kwenye kochi aliitikia salamu ya Japhet na kuuliza hivyo.

"Mimi niko poa tu Shemeji yangu, nashukuru kumekucha salama" alisema Japhet huku akiketi kwenye kochi.

Mara ghafla nje ukasikika mlio wa honi ya gari iliyokuwa imepaki barazani.

"Sasa jamani mimi ndio naondoka hivyo Mungu akipenda tutaonana tena, bakini salama" alisema Lukasi huku akianza kutoka nje. Japhet akachukua lile begi la kaka yake na kulibeba akimsaidia. "Sawa mume wangu nakutakia safari njema uende salama baby, nitakumiss sana jamani" alisema Flora kwa huzuni huku akimkumbatia mumewe na kumuaga.

"Usijali mke wangu, wiki mbili sio mbali sana nitarejea" alisema Lukasi. Baada ya hapo wakaachiana na Lukasi akachukua begi lake kutoka kwa Japhet na kuingia ndani ya hiyo gari ambayo ni aina ya Taxi aliyokubaliana na dereva wake aje kumchukua hapa nyumbani kwake asubuhi hii ya leo na kumpeleka sehemu ambapo kilipo kituo kikuu cha mabasi. safari ya kuelekea kituo cha mabasi yaendayo mikoani (UBUNGO BUS TERMINAL) ili akapande basi la kuelekea jijini Mwanza huko anapoenda kwa ajili ya shughuli zake za kibiashara. Japhet na Shemeji yake Flora walisimama kwa barazani wakimpungia mikono ya kumuaga Lukasi aliyekuwà tayari ameshaingia kwenye hiyo gari na punde gari ikaondoka. Huku nyuma Japhet na Shemeji yake Flora nao wakaingia ndani.

Kwa kuwa ilikuwa bado ni mapema yapata kama SAA 11 : 30 za alifàjiri hivyo kila mmoja akaingia cgumbani kwake kwenda kuumalizia usingizi ule mwisho mwisho. Muda huo dada wa kazi wa hapa nyumbani kwa Lukasi aitwae Rozi ndio alikuwa ameshaamka na kuanza kufanya majukumu yake ya kila siku ikiwemo usafi na kazi nyinginezo za nyumbani.

Japhet akiwa amejilaza kitandani kwake mara baada ya kurudi chumbani akitokea kumuaga kaka yake Lukasi aliyesafiri.

Japhet akaanza kujihisi msisimuko wa kimapenzi kwenye sehemu zake za siri 'Gobole' lake lilianza kumsumbua likihitaji kupata sehemu yake ya kuachia Risasi.

"Daah mambo gani haya sasa? huku kukosa demu napo ni shida kwelikweli" alijisemea kijana Japhet huku akilala kifudifudi na kuzidi kujifunika shuka.

Lakini wapi 'Gobole' lake liliendelea tu kumsumbua lilidinda ile kisawasawa mpaka mishipa ikaanza kumuuma na ukizingatia ni asubuhi kiubaridi kinapuliza basi ilikuwa ni tabu kweli kwa kijana huyo. "Duuh hii sasa ni balaa hebu ngoja kwanza nikajaribu kukojoa labda itapoa" alijisemea mwenyewe huku akinyanyuka kitandani na kutoka humo chumbani.

INAENDELEA.
Powered by Blogger.