KARIBU USOME HADITHI NZURI ZA KUSISIMUA

Chombezo : Ni Shiida! Sehemu Ya Nne (4)

 LOVE STORY: ni shiidaI - 4
Bitungu alikaa kitandani akijifikiria. Alimuwaza Juliana akahisi kama anafaa kuwa mpenzi wake wa moja kwa moja…

"Sijui ndiyo awe mchumba wangu?" alijiuliza Bitungu. Mara simu yake iliita, alikuwa mama Juliana. Safari hii akaipokea…


"Jamani baby, mbona hukuwa unapokea simu yangu, ulikuwa na malaya gani leo?"

"Hamna baby bwana, nililala sehemu sikuwa najisikia vizuri."

"Ulilala sehemu wapi, ina maana si nyumbani kwako siyo?"

"Siyo."

"Wapi?"



"Nipo hapa Ilala Amana."

"Ilala Amana? Uko na nani?"

"Mwenyewe."

"We mwongo, kama kweli niruhusu nije."

"Njoo."



Mama Juliana alikata simu bila kutaka kuuliza Amana sehemu gani. Alimpigia simu mumewe kumuuliza anarudi saa ngapi, akamwambia atachelewa.

"Oke," mama Juliana alikata simu kwa mumewe. Akaondoka muda huohuo, anafika nje anapishana na Juliana…"Ndiyo unafika sasa, siyo?"



"Ndiyo mama."

"Mimi narudi muda si mrefu."

"Kwani unakwenda wapi?"

"We, koma ukomaye. Swali gani unaniuliza mimi mama yako?"

***

Mama Juliana aliposhuka Amana ndiyo akampigia simu Bitungu na kumuuliza aliko…

"Ukishashuka vuka barabara, mbele kuna mtaa umeingia, fuata huo hadi jirani na nyumba moja ina genge nje utaona gesti kwa mbele," alisema Bitungu akiwa anatoa maelekezo kwa mama Juliana.



Kwa jinsi mama Juliana alivyokuwa na hamu na kijana huyo, hakusema sawa baada ya maelekezo, yeye alikata simu tu na kuanza kutembea kuelekea alikoelekezwa.



Aliingia kwenye gesti hiyo akiwa amesahau kumuuliza Bitungu namba ya chumba. Mbaya zaidi simu yake ilizima chaji, hivyo aliamua kugonga kila chumba na kuuliza…

"Ngo ngo ngo!" aligonga mlango akasimama mwanaume…

"Nikusaidie?"



"Samahani, kumbe si hapa!"

Akaenda mlango mwingine….

"Ngo ngo ngooo!"



Akatoka msichana, akasimama mlangoni akiwa na taulo…

"Unamjua Bitungu?"

"Bitungu! Ndiyo nani?"

"Kijana mmoja hivi, nilidhani uko naye."



Yule msichana aligeuka kuangalia ndani, mama Juliana akaamini kweli msichana huyo alikuwa na Bitungu ndiyo maana aligeuka kuangalia ndani, akamsukuma msichana yeye akazama ndani…

"He! We mama vipi?"



"Bitungu unadiriki kuni…oooh! Sorry kijana, nisamehe bure nilidhani ni Bitungu."

Kijana aliyelala kitandani akiwa kama alivyozaliwa alimrukia mama Juliana akitaka ajue ni kwa nini aliingia bila maelewano…


"Huwezi kusema sorry halafu ukavamia hivihivi, nani amekwambia mimi ni Bitungu?" alihoji kijana huyo, akamshika mama Juliana na kumwangusha kitandani na kutaka kumwingia kwa mabavu…

"Noo, Bwakila usifanye hivyo," alisema yule msichana…

"Noo, huyu mama ndiyo dawa yake hii, ndicho alichotaka lazima akipate."

Ilibidi yule msichana amkabe kwa nguvu Bwakila ili amtoe mama Juliana ambaye wakati huo alishashindwa kwa pumzi na nguvu pia."Mwanangu nisamehe sana, kweli kabisa nilidhani wewe ni Bitungu, nisamehe sana baba."



ITAENDELEA
Powered by Blogger.